< 1 Samuel 27 >

1 and to say David to(wards) heart his now to snatch day one in/on/with hand: power Saul nothing to/for me pleasant for to escape to escape to(wards) land: country/planet Philistine and to despair from me Saul to/for to seek me still in/on/with all border: boundary Israel and to escape from hand: power his
Daudi akasema moyoni mwake, “Katika mojawapo ya siku hizi nitaangamizwa kwa mkono wa Sauli. Jambo lililo bora ni kutorokea kwenye nchi ya Wafilisti. Hivyo Sauli atakata tamaa ya kunisaka popote katika Israeli, nami nitakuwa nimeponyoka mkononi mwake.”
2 and to arise: rise David and to pass he/she/it and six hundred man which with him to(wards) Achish son: child Maoch king Gath
Hivyo Daudi akaondoka na hao watu mia sita waliokuwa pamoja naye na kwenda kwa Akishi mwana wa Maoki mfalme wa Gathi.
3 and to dwell David with Achish in/on/with Gath he/she/it and human his man: anyone and house: household his David and two woman: wife his Ahinoam [the] Jezreel and Abigail woman: wife Nabal [the] Carmelite
Daudi na watu wake wakakaa huko Gathi pamoja na Akishi. Kila mtu alikuwa pamoja na jamaa yake, naye Daudi pamoja na wakeze wawili: yaani Ahinoamu wa Yezreeli, na Abigaili wa Karmeli, mjane wa Nabali.
4 and to tell to/for Saul for to flee David Gath and not (to add: again *Q(K)*) still to/for to seek him
Sauli alipokuwa ameambiwa kwamba Daudi alikuwa amekimbilia Gathi, hakuendelea kumsaka tena.
5 and to say David to(wards) Achish if please to find favor in/on/with eye: appearance your to give: give to/for me place in/on/with one city [the] land: country and to dwell there and to/for what? to dwell servant/slave your in/on/with city [the] kingdom with you
Ndipo Daudi akamwambia Akishi, “Kama nimepata kibali machoni pako, unipe sehemu katika mojawapo ya miji katika nchi nikae huko. Kwa nini mtumwa wako akae pamoja nawe katika mji huu wa kifalme?”
6 and to give: give to/for him Achish in/on/with day: today [the] he/she/it [obj] Ziklag to/for so to be Ziklag to/for king Judah till [the] day: today [the] this
Hivyo siku hiyo Akishi akampa Daudi mji wa Siklagi, nao Siklagi umekuwa mali ya wafalme wa Yuda tangu wakati huo.
7 and to be number [the] day which to dwell David in/on/with land: country Philistine day: year and four month
Daudi akaishi katika nchi ya Wafilisti muda wa mwaka mmoja na miezi minne.
8 and to ascend: rise David and human his and to strip to(wards) [the] Geshurite (and [the] Girzite *Q(K)*) and [the] Amalekite for they(fem.) to dwell [the] land: country/planet which from forever: antiquity to come (in): towards you Shur [to] and till land: country/planet Egypt
Basi Daudi na watu wake wakapanda na kuwashambulia Wageshuri, Wagirizi na Waamaleki. (Tangu zamani haya mataifa yalikuwa yameishi kwenye eneo lililotanda kuanzia Telemu katika njia iteremkayo Shuri hadi kufikia nchi ya Misri.)
9 and to smite David [obj] [the] land: country/planet and not to live man and woman and to take: take flock and cattle and donkey and camel and garment and to return: return and to come (in): come to(wards) Achish
Kila mara Daudi aliposhambulia eneo, hakubakiza hai mwanaume wala mwanamke, lakini alichukua kondoo na ngʼombe, punda na ngamia, na nguo. Kisha akarudi kwa Akishi.
10 and to say Achish to(wards) to strip [the] day and to say David upon Negeb Judah and upon Negeb [the] Jerahmeelite and to(wards) Negeb [the] Kenite
Akishi alipomuuliza, “Je leo umeshambulia wapi?” Daudi humjibu, “Dhidi ya Negebu ya Yuda,” au wakati mwingine husema, “Dhidi ya Negebu ya Yerameeli,” au “Dhidi ya Negebu ya Wakeni.”
11 and man and woman not to live David to/for to come (in): bring Gath to/for to say lest to tell upon us to/for to say thus to make: do David and thus justice: custom his all [the] day which to dwell in/on/with land: country Philistine
Daudi hakumwacha hai mwanaume au mwanamke ili apate kuletwa Gathi, kwa maana Daudi aliwaza, “Wanaweza kujulisha habari zetu na kusema, ‘Hivi ndivyo alivyofanya Daudi.’” Hii ndiyo ilikuwa desturi yake wakati wote aliishi katika nchi ya Wafilisti.
12 and be faithful Achish in/on/with David to/for to say to stink to stink in/on/with people his in/on/with Israel and to be to/for me to/for servant/slave forever: enduring
Akishi akamsadiki Daudi na kuwaza moyoni mwake, akasema, “Daudi amekuwa kitu cha kuchukiza kabisa kwa watu wake, Waisraeli, hivi kwamba atakuwa mtumishi wangu milele.”

< 1 Samuel 27 >