< 1 Samuel 26 >

1 and to come (in): come [the] Ziphite to(wards) Saul [the] Gibeah [to] to/for to say not David to hide in/on/with hill [the] Hachilah upon face: east [the] Jeshimon
Hao Wazifu wakamwendea Sauli huko Gibea na kusema, “Je, Daudi hakujificha katika kilima cha Hakila, kinachotazamana na Yeshimoni?”
2 and to arise: rise Saul and to go down to(wards) wilderness Ziph and with him three thousand man to choose Israel to/for to seek [obj] David in/on/with wilderness Ziph
Hivyo Sauli akashuka kwenda katika Jangwa la Zifu, akiwa na watu wake 3,000 wa Israeli waliochaguliwa, kumsaka Daudi huko.
3 and to camp Saul in/on/with hill [the] Hachilah which upon face: east [the] Jeshimon upon [the] way: road and David to dwell in/on/with wilderness and to see: see for to come (in): come Saul after him [the] wilderness [to]
Sauli akapiga kambi yake kando ya barabara juu ya kilima cha Hakila kinachotazamana na Yeshimoni, lakini Daudi alikuwa anaishi huko jangwani. Alipoona kuwa Sauli amemfuata huko,
4 and to send: depart David to spy and to know for to come (in): come Saul to(wards) to establish: right
Daudi akatuma wapelelezi na akapata habari kwa hakika kwamba Sauli alikuwa amewasili.
5 and to arise: rise David and to come (in): come to(wards) [the] place which to camp there Saul and to see: see David [obj] [the] place which to lie down: lay down there Saul and Abner son: child Ner ruler army his and Saul to lie down: lay down in/on/with track and [the] people: soldiers to camp (around him *Q(K)*)
Ndipo Daudi akaondoka, akaenda hadi mahali Sauli alikuwa amepiga kambi. Akaona mahali Sauli na Abneri mwana wa Neri, jemadari wa jeshi, walipokuwa wamelala. Sauli alikuwa amelala ndani ya kambi, jeshi likiwa limemzunguka.
6 and to answer David and to say to(wards) Ahimelech [the] Hittite and to(wards) Abishai son: child Zeruiah brother: male-sibling Joab to/for to say who? to go down with me to(wards) Saul to(wards) [the] camp and to say Abishai I to go down with you
Basi Daudi akamuuliza Ahimeleki Mhiti, na Abishai mwana wa Seruya, nduguye Yoabu, akisema, “Ni nani atakayeshuka pamoja nami kambini kwa Sauli?” Abishai akajibu, “Nitakwenda pamoja nawe.”
7 and to come (in): come David and Abishai to(wards) [the] people: soldiers night and behold Saul to lie down: lay down sleeping in/on/with track and spear his to bruise in/on/with land: soil (head his *Q(K)*) and Abner and [the] people: soldiers to lie down: lay down (around him *Q(K)*)
Hivyo Daudi na Abishai wakaenda kwenye jeshi wakati wa usiku, tazama Sauli, alikuwa amelala ndani ya kambi na mkuki wake umekitwa ardhini karibu na kichwa chake. Abneri na askari walikuwa wamelala kumzunguka Sauli.
8 and to say Abishai to(wards) David to shut God [the] day: today [obj] enemy your in/on/with hand: power your and now to smite him please in/on/with spear and in/on/with land: soil beat one and not to repeat to/for him
Abishai akamwambia Daudi, “Leo Mungu amemtia adui yako mikononi mwako. Sasa niruhusu nimchome mpaka ardhini kwa pigo moja la mkuki wangu; sitamchoma mara mbili.”
9 and to say David to(wards) Abishai not to ruin him for who? to send: reach hand his in/on/with anointed LORD and to clear
Lakini Daudi akamwambia Abishai, “Usimwangamize! Ni nani awezaye kutia mkono juu ya mpakwa mafuta wa Bwana na asiwe na hatia?”
10 and to say David alive LORD that if: except if: except LORD to strike him or day his to come (in): come and to die or in/on/with battle to go down and to snatch
Daudi akasema, “Hakika kama vile Bwana aishivyo, Bwana mwenyewe atampiga; au wakati wake utafika, naye atakufa, au atakwenda vitani na kuangamia.
11 forbid to/for me from LORD from to send: reach hand my in/on/with anointed LORD and now to take: take please [obj] [the] spear which (head his *Q(K)*) and [obj] jar [the] water and to go: went to/for us
Lakini Mungu na apishie mbali nisije nikainua mkono juu ya mpakwa mafuta wa Bwana. Sasa chukua huo mkuki na hilo gudulia la maji vilivyo karibu na kichwa chake, tuondoke.”
12 and to take: take David [obj] [the] spear and [obj] jar [the] water head-place Saul and to go: went to/for them and nothing to see: see and nothing to know and nothing to awake for all their sleeping for deep sleep LORD to fall: fall upon them
Hivyo Daudi akachukua huo mkuki na hilo gudulia la maji vilivyokuwa karibu na kichwa cha Sauli, nao wakaondoka. Hakuna yeyote aliyeona au kufahamu habari hii, wala hakuna hata mmoja aliyeamka usingizini. Wote walikuwa wamelala, kwa sababu Bwana alikuwa amewatia kwenye usingizi mzito.
13 and to pass David [the] side: beside and to stand: stand upon head: top [the] mountain: mount from distant many [the] place between them
Kisha Daudi akavuka upande mwingine na kusimama juu ya kilima mahali palipokuwa na nafasi pana kati yao.
14 and to call: call to David to(wards) [the] people: soldiers and to(wards) Abner son: child Ner to/for to say not to answer Abner and to answer Abner and to say who? you(m. s.) to call: call to to(wards) [the] king
Daudi akalipigia kelele jeshi na Abneri mwana wa Neri, akisema, “Je, Abneri, hutanijibu?” Abneri akajibu, “Nani wewe umwitaye mfalme?”
15 and to say David to(wards) Abner not man you(m. s.) and who? like you in/on/with Israel and to/for what? not to keep: guard to(wards) lord your [the] king for to come (in): come one [the] people to/for to ruin [obj] [the] king lord your
Daudi akasema, “Wewe si ni mtu shujaa? Ni nani aliye kama wewe katika Israeli? Kwa nini basi hukumlinda mfalme bwana wako? Mtu mmoja alikuja kumwangamiza mfalme, bwana wako.
16 not pleasant [the] word: thing [the] this which to make: do alive LORD for son: descendant/people death you(m. p.) which not to keep: guard upon lord your upon anointed LORD and now to see: see where? spear [the] king and [obj] jar [the] water which (head his *Q(K)*)
Ulichokifanya si kizuri. Kwa hakika kama aishivyo Bwana, wewe na watu wako mnastahili kufa, kwa sababu hamkumlinda bwana wenu, mpakwa mafuta wa Bwana. Tazameni hapo mlipo. Uko wapi mkuki wa mfalme na gudulia la maji ambavyo vilikuwa karibu na kichwa chake?”
17 and to recognize Saul [obj] voice David and to say voice your this son: child my David and to say David voice my lord my [the] king
Sauli akatambua sauti ya Daudi, na kusema, “Je, hiyo ni sauti yako, Daudi mwanangu?” Daudi akajibu, “Naam, hiyo ndiyo, bwana wangu mfalme.”
18 and to say to/for what? this lord my to pursue after servant/slave his for what? to make: do and what? in/on/with hand my distress: evil
Pia akaongeza, “Kwa nini bwana wangu anamfuatia mtumishi wake? Nimefanya nini, nalo kosa langu ni lipi nililolifanya niwe na hatia?
19 and now to hear: hear please lord my [the] king [obj] word servant/slave his if LORD to incite you in/on/with me to smell offering and if son: descendant/people [the] man to curse they(masc.) to/for face: before LORD for to drive out: drive out me [the] day: today from to attach in/on/with inheritance LORD to/for to say to go: went to serve God another
Sasa mfalme bwana wangu na asikilize maneno ya mtumishi wake. Kama Bwana amekuchochea dhidi yangu, basi yeye na aipokee sadaka yangu. Lakini hata hivyo, kama ni wanadamu waliofanya hivyo, walaaniwe mbele za Bwana! Wao sasa wamenifukuza kutoka sehemu yangu katika urithi wa Bwana wangu wakisema, ‘Nenda ukatumikie miungu mingine.’
20 and now not to fall: fall blood my land: soil [to] from before face: before LORD for to come out: come king Israel to/for to seek [obj] flea one like/as as which to pursue [the] partridge in/on/with mountain: mount
Basi usiache damu yangu imwagike kwenye ardhi mbali na uso wa Bwana. Mfalme wa Israeli ametoka kutafuta kiroboto, kama vile mtu awindavyo kware katika milima.”
21 and to say Saul to sin to return: return son: child my David for not be evil to/for you still underneath: because of which be precious soul: life my in/on/with eye: appearance your [the] day: today [the] this behold be foolish and to wander to multiply much
Ndipo Sauli akasema, “Nimetenda dhambi. Rudi, Daudi mwanangu. Kwa kuwa uliyahesabu maisha yangu kuwa ya thamani leo, sitajaribu kukudhuru tena. Hakika nimetenda kama mpumbavu na nimekosa sana.”
22 and to answer David and to say behold (spear *Q(K)*) [the] king and to pass one from [the] youth and to take: take her
Daudi akajibu, “Mkuki wa mfalme uko hapa. Mmoja wa vijana wako na avuke kuuchukua.
23 and LORD to return: pay to/for man: anyone [obj] righteousness his and [obj] faithfulness his which to give: give you LORD [the] day in/on/with hand: power and not be willing to/for to send: reach hand my in/on/with anointed LORD
Bwana humlipa kila mtu kwa ajili ya haki yake na uaminifu wake. Bwana alikutia katika mikono yangu leo, lakini sikuinua mkono wangu juu ya mpakwa mafuta wa Bwana.
24 and behold like/as as which to magnify soul: life your [the] day: today [the] this in/on/with eye: seeing my so to magnify soul: life my in/on/with eye: seeing LORD and to rescue me from all distress
Kwa hakika kama vile maisha yako yalivyokuwa ya thamani kwangu leo, vivyo hivyo maisha yangu na yawe na thamani kwa Bwana na kuniokoa kutoka taabu zote.”
25 and to say Saul to(wards) David to bless you(m. s.) son: child my David also to make: do to make: do and also be able be able and to go: went David to/for way: journey his and Saul to return: return to/for place his
Ndipo Sauli akamwambia Daudi, “Mwanangu Daudi na ubarikiwe; utafanya mambo makubwa na hakika utashinda.” Basi Daudi akaenda zake, naye Sauli akarudi nyumbani.

< 1 Samuel 26 >