< Proverbs 17 >

1 [is] good A morsel dry and quietness with it more than a house full sacrifices of strife.
Afadhali kula ukoko mkavu ukiwa na amani na utulivu kuliko kukaa kwenye nyumba ya karamu kukiwa na magomvi.
2 A servant [who] acts prudently he will rule over a son [who] acts shamefully and in among brothers he will share [the] inheritance.
Mtumishi mwenye hekima atatawala juu ya mwana aaibishaye, naye atashirikiana katika urithi kama mmoja wa hao ndugu.
3 A crucible [is] for silver and a smelting furnace [is] for gold and [is] testing hearts Yahweh.
Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu, bali Bwana huujaribu moyo.
4 An evil-doer [is] paying attention on a lip of wickedness deception [is] giving ear on a tongue of destruction.
Mtu mwovu husikiliza midomo mibaya; mwongo husikiliza kwa makini ulimi wa madhara.
5 [one who] mocks the Poor [person] he reproaches maker his [a person] joyful for calamity not he will go unpunished.
Yeye anaye mdhihaki maskini huonyesha dharau kwa Muumba wake; yeyote afurahiaye maafa hataepuka kuadhibiwa.
6 [are the] crown of Old [people] children of children and [are the] honor of children parents their.
Wana wa wana ni taji la wazee, nao wazazi ni fahari ya watoto wao.
7 Not [is] suitable for a fool a lip of excellence indeed? for for a noble [person] a lip of deception.
Midomo yenye uwezo wa ushawishi haimfai mpumbavu: je, ni mibaya kiasi gani zaidi midomo ya uongo kwa mtawala!
8 [is] a stone of Favor the bribe in [the] eyes of owners its to all that he turns he prospers.
Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho; kokote kigeukiapo, hufanikiwa.
9 [one who] conceals A transgression [is] seeking love and [one who] repeats a matter [is] separating a close friend.
Yeye anayesamehe kosa hudumisha upendo, bali yeyote arudiaye jambo hutenganisha marafiki wa karibu.
10 It goes deep a rebuke in [one who] understands more than striking a fool a hundred [times].
Karipio humwingia sana mtu mwenye kutambua kuliko mapigo mia kwa mpumbavu.
11 Only rebellion he seeks an evil [person] and a messenger cruel he will be sent in him.
Mtu mbaya hupenda kuasi tu; mjumbe asiye na huruma atatumwa dhidi yake.
12 May he meet a bear robbed of cubs a person and may not [he meet] a fool in foolishness his.
Ni afadhali ukutane na dubu aliyenyangʼanywa watoto wake, kuliko mpumbavu katika upumbavu wake.
13 [one who] returns Evil for good not (it will depart *Q(k)*) evil from house his.
Ikiwa mtu atalipa baya kwa jema, kamwe ubaya hautaondoka katika nyumba yake.
14 [is one who] lets out Water [the] beginning of strife and before it has broken out the dispute abandon.
Kuanzisha ugomvi ni kama kutoboa bwawa la maji; kwa hiyo acha jambo hilo kabla mabishano hayajaanza.
15 [one who] justifies [the] wicked And [one who] condemns as guilty [the] righteous [are] [the] abomination of Yahweh also both of them.
Yeye asemaye kuwa asiye na haki ana haki, naye asemaye kuwa mwenye haki hana haki: Bwana huwachukia sana wote wawili.
16 Why? this [is] a price in [the] hand of a fool to acquire wisdom and [is] heart there not.
Fedha ina faida gani mikononi mwa mpumbavu, wakati yeye hana haja ya kupata hekima?
17 At every time [is] loving the friend and a brother for adversity he is born.
Rafiki hupenda wakati wote naye ndugu amezaliwa kwa ajili ya wakati wa shida.
18 A person lacking of heart [is] striking a palm [is] pledging a pledge before neighbor his.
Mtu mjinga hupana mkono ili kuweka rehani, naye huweka dhamana kwa jirani yake.
19 [one who] loves Transgression [is] loving contention [one who] makes high entrance his [is] seeking ruin.
Yeye apendaye ugomvi apenda dhambi; naye ainuaye sana lango lake hutafuta uharibifu.
20 [a person] twisted of Heart not he finds good and [one who] is perverted in tongue his he falls in trouble.
Mtu mwenye moyo mpotovu hawezi kufanikiwa; naye ambaye ulimi wake ni mdanganyifu huanguka kwenye taabu.
21 [one who] begets A fool to grief of him and not he rejoices [the] father of a fool.
Kuwa na mwana mpumbavu huleta huzuni; hakuna furaha kwa baba wa mpumbavu.
22 A heart joyful it makes good healing and a spirit stricken it dries up bone[s].
Moyo wenye furaha ni dawa nzuri, bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.
23 A bribe from [the] bosom a wicked [person] he accepts to turn aside [the] paths of justice.
Mtu mwovu hukubali rushwa kwa siri ili kupotosha njia ya haki.
24 [is] with [the] face of [one who] has understanding Wisdom and [the] eyes of a fool [are] at [the] end of [the] earth.
Mtu wa ufahamu huitazama hekima, lakini macho ya mpumbavu huhangaika hadi kwenye miisho ya dunia.
25 [is] grief To father his a son a fool and bitterness to [the] [one who] bore him.
Mwana mpumbavu huleta huzuni kwa baba yake na uchungu kwa yeye aliyemzaa.
26 Also to impose a fine to righteous [person] not [is] good to strike noble [people] [is] on uprightness.
Si vizuri kumwadhibu mtu asiye na hatia, au kuwapiga sana maafisa kwa ajili ya uadilifu wao.
27 [one who] restrains Words his [is] knowing knowledge ([a person] noble of *Q(K)*) spirit [is] a person of understanding.
Mtu mwenye maarifa hutumia maneno kwa kujizuia, naye mtu mwenye ufahamu ana moyo wa utulivu.
28 Also a fool [who] keeps silent wise he is considered [who] shuts lips his discerning.
Hata mtu mpumbavu hudhaniwa kuwa na hekima kama akinyamaza, na mwenye ufahamu kama akiuzuia ulimi wake.

< Proverbs 17 >