< Luke 1 >

1 Inasmuch as many undertook to draw up a narration concerning the accomplished among us things,
Kwa kuwa watu wengi wamekaa ili kuandika habari za mambo yaliyotukia katikati yetu,
2 even as delivered [them] to us those from [the] beginning eyewitnesses and servants having been of the word,
kama vile yalivyokabidhiwa kwetu na wale waliokuwa mashahidi walioyaona na watumishi wa Bwana,
3 it seemed good also to me also to me having been acquainted from the first with all things carefully with method to you to write, most excellent Theophilus,
mimi nami baada ya kuchunguza kila kitu kwa uangalifu kuanzia mwanzo, niliamua kukuandikia habari za mambo hayo, ewe mtukufu Theofilo,
4 so that you may know concerning which you were instructed [of the] things the certainty.
ili upate kujua ukweli kuhusu yale uliyofundishwa.
5 There was in the days of Herod (*k*) king of Judea a priest certain named Zechariah of [the] division of Abijah, and (the *k*) wife (of him *N(k)O*) of the daughters of Aaron and the name of her Elizabeth.
Wakati wa Herode mfalme wa Uyahudi, palikuwa na kuhani mmoja jina lake Zekaria, ambaye alikuwa wa ukoo wa kikuhani wa Abiya. Elizabeti mkewe alikuwa pia mzao wa Aroni.
6 They were now righteous both (in front of *N(k)O*) God walking in all the commandments and ordinances of the Lord blameless.
Zekaria na Elizabeti mkewe wote walikuwa watu wanyofu mbele za Mungu, wakizishika amri zote za Bwana na maagizo yote bila lawama.
7 And no there was to them child, inasmuch as was Elizabeth barren and both having advanced in the years of them were.
Lakini walikuwa hawana watoto, kwa sababu Elizabeti alikuwa tasa; nao wote wawili walikuwa wazee sana.
8 It came to pass now in the priestly serving of him in the order of the division of him before God,
Siku moja ilipokuwa zamu ya kikundi cha Zekaria, yeye akifanya kazi ya ukuhani Hekaluni mbele za Mungu,
9 according to the custom of the priesthood the lot picked [him as] the [one] to burn incense entering into the temple of the Lord;
alichaguliwa kwa kura kwa kufuata desturi za ukuhani, kuingia Hekaluni mwa Bwana ili kufukiza uvumba.
10 And all the multitude were of the people praying outside at the hour of the incense.
Nao wakati wa kufukiza uvumba ulipowadia, wale wote waliokuwa wamekusanyika ili kuabudu walikuwa nje wakiomba.
11 Appeared then to him an angel of [the] Lord already standing at [the] right of the altar of the incense;
Ndipo malaika wa Bwana, akiwa amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya kufukizia uvumba, akamtokea Zekaria.
12 And was troubled Zechariah having seen [him], and fear fell upon him.
Zekaria alipomwona huyo malaika, akafadhaika sana, akajawa na hofu.
13 Said then to him the angel; Not do fear Zechariah; because has been heard the prayer of you, and the wife of You Elizabeth will bear a son to you, and you will call the name of him John.
Lakini malaika akamwambia, “Usiogope, Zekaria, kwa maana Mungu amesikia maombi yako. Mkeo Elizabeti atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utamwita jina lake Yohana.
14 And he will be joy to you and gladness, and many at the (birth *N(k)O*) of him will rejoice.
Yeye atakuwa furaha na shangwe kwako, nao watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
15 He will be for great before the Lord, and wine and strong drink certainly not shall he drink, and [of the] Spirit Holy he will be filled even from [the] womb of [the] mother of him.
Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele za Bwana, kamwe hataonja mvinyo wala kinywaji chochote cha kulevya, naye atajazwa Roho Mtakatifu hata kabla ya kuzaliwa kwake.
16 And many of the sons of Israel he will turn to [the] Lord the God of them,
Naye atawageuza wengi wa wana wa Israeli warudi kwa Bwana Mungu wao.
17 And he himself will go forth before Him in [the] spirit and power of Elijah to turn [the] hearts of [the] fathers to [the] children and [the] disobedient to [the] wisdom of [the] righteous, to make ready for [the] Lord a people prepared.
Naye atatangulia mbele za Bwana katika roho na nguvu ya Eliya, ili kuigeuza mioyo ya baba kuwaelekea watoto wao, na wasiotii warejee katika hekima ya wenye haki, ili kuliweka tayari taifa lililoandaliwa kwa ajili ya Bwana.”
18 And said Zechariah to the angel; By what will I know this? I myself for am an old man, and the wife of mine having advanced in the years of her.
Zekaria akamuuliza malaika, “Jambo hilo linawezekanaje? Mimi ni mzee na mke wangu pia ana umri mkubwa.”
19 And answering the angel said to him; I myself am Gabriel the [one] standing before God and I was sent to speak to you and to bring glad tidings to you these.
Malaika akamjibu, akamwambia, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele za Mungu, nami nimetumwa kwako ili nikuambie habari hizi njema.
20 And behold you will be silent and not able to speak until that day may happen these things, in return for that not you did believe in the words of mine which will be fulfilled in the season of them.
Basi sasa kwa kuwa hujaamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati wake, utakuwa bubu hadi siku ile mambo haya yatakapotukia.”
21 And were the people expecting Zechariah and they were wondering at the delaying in the temple of him.
Wakati huo watu walikuwa wanamngojea Zekaria nje huku wakishangaa kukawia kwake mle Hekaluni.
22 Having come out then not he was able to speak to them; and they recognized that a vision he has seen in the temple. And he himself was making signs to them and was remaining mute.
Alipotoka akawa hawezi kusema nao, wao wakatambua kuwa ameona maono ndani ya Hekalu. Lakini kwa kuwa alikuwa bubu, akawa anawaashiria kwa mikono.
23 And it came to pass when were fulfilled the days of the service of him, he departed to the home of him.
Muda wake wa kuhudumu Hekaluni ulipomalizika, akarudi nyumbani kwake.
24 After then these days conceived Elizabeth the wife of him and was hiding herself months five saying
Baada ya muda usio mrefu, Elizabeti mkewe akapata mimba, naye akajitenga kwa miezi mitano.
25 that Thus to me has done (the *k*) Lord in [the] days in which He looked upon [me] to take away (the *k*) disgrace of mine among men.
Akasema, “Hili ndilo Bwana alilonitendea aliponiangalia kwa upendeleo na kuniondolea aibu yangu mbele ya watu.”
26 In now the month sixth was sent the angel Gabriel (by *N(k)O*) God to a city of Galilee whose name [was] Nazareth
Mwezi wa sita baada ya Elizabeti kupata mimba, Mungu alimtuma malaika Gabrieli aende Galilaya katika mji wa Nazareti,
27 to a virgin betrothed to a man whose name [was] Joseph of [the] house of David, and the name of the virgin [was] Mary.
kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu mmoja jina lake Yosefu wa nyumba ya Daudi. Jina la huyu mwanamwali bikira ni Maria.
28 And having come (*ko*) (angel *KO*) to her he said; Greetings! you graciously favored; The Lord [is] with you. (blessed [are] you yourself among women. *KO*)
Naye malaika akaja kwake akamwambia: “Salamu, wewe uliyebarikiwa, Bwana yu pamoja nawe!”
29 And (having seen [him] *K*) at the statement she was troubled (of him *k*) and was pondering what kind would be salutation this.
Maria akafadhaishwa sana na maneno haya, akajiuliza moyoni, “Salamu hii ni ya namna gani?”
30 And said the angel to her; Not do fear Mary, you have found for favor with God.
Ndipo malaika akamwambia, “Usiogope, Maria, umepata kibali kwa Mungu.
31 and behold you will conceive in womb and will bring forth a son and you will call the name of Him Jesus.
Tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanaume na utamwita jina lake Yesu.
32 He will be great and Son of [the] Most High He will be called, and will give to Him [the] Lord God the throne of David of the father of Him,
Yeye atakuwa mkuu, naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
33 and He will reign over the house of Jacob to the ages, and of the kingdom of Him not there will be an end! (aiōn g165)
Ataimiliki nyumba ya Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn g165)
34 Said then Mary to the angel; How will be this since a man not I know?
Maria akamuuliza huyo malaika, “Maadamu mimi ni bikira, jambo hili litawezekanaje?”
35 And answering the angel said to her; [the] Spirit Holy will come upon you and power of [the] Most High will overshadow you; therefore also the [one] being born Holy [One] will be called [the] Son of God.
Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, nazo nguvu zake Yeye Aliye Juu Sana zitakufunika kama kivuli. Kwa hiyo mtoto atakayezaliwa atakuwa mtakatifu, naye ataitwa Mwana wa Mungu.
36 And behold Elizabeth the (relative *N(k)O*) of you also she (has conceived *N(k)O*) a son in old age of her, and this month [the] sixth is to her who [was] called barren
Tazama, jamaa yako Elizabeti amechukua mimba katika uzee wake, na huu ni mwezi wake wa sita, yeye aliyeitwa tasa.
37 For not will be impossible with (God *N(k)O*) every declaration.
Kwa maana kwa Mungu hakuna lisilowezekana.”
38 Said then Mary; Behold the handmaid of [the] Lord; Would [that] it happen to me according to the declaration of you. And departed from her the angel.
Maria akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa Bwana. Na iwe kwangu kama ulivyosema.” Kisha malaika akaondoka, akamwacha.
39 Having risen up then Mary in days these she went into the hill country with haste to a town of Judah
Wakati huo Maria akajiandaa, akaharakisha kwenda katika mji mmoja kwenye vilima vya Uyahudi.
40 and she entered into the house of Zechariah and greeted Elizabeth.
Akaingia nyumbani kwa Zekaria na kumsalimu Elizabeti.
41 And it came to pass as heard the greeting of Mary Elizabeth, leaped the baby in the womb of her, and was filled with [the] Spirit Holy Elizabeth
Naye Elizabeti aliposikia salamu ya Maria, mtoto aliyekuwa tumboni mwake akaruka. Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu,
42 and she cried out (in a shout *N(k)O*) loud and said; Blessed [are] you yourself among women, and blessed [is] the fruit of the womb of you.
akapaza sauti kwa nguvu akasema, “Umebarikiwa wewe miongoni mwa wanawake, naye mtoto utakayemzaa amebarikiwa.
43 And from where to me this that may come the mother of the Lord of mine to me myself?
Lakini ni kwa nini mimi nimepata upendeleo kiasi hiki, hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
44 Behold for as came the voice of the greeting of you into the ears of mine, leaped in exultation the baby in the womb of mine.
Mara tu niliposikia sauti ya salamu yako, mtoto aliyeko tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
45 And blessed [is] the [one] having believed that there will be a fulfillment to the [things] spoken to her from [the] Lord.
Amebarikiwa yeye aliyeamini kwamba lile Bwana alilomwambia litatimizwa.”
46 And said Mary: Magnifies the soul of Mine the Lord,
Naye Maria akasema: “Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,
47 and rejoices the spirit of mine in God the Savior of mine,
nayo roho yangu inamfurahia Mungu Mwokozi wangu,
48 For He has looked upon the humiliation of the handmaiden of Him. Behold for from henceforth will count blessed me all the generations
kwa kuwa ameangalia kwa fadhili unyonge wa mtumishi wake. Hakika tangu sasa vizazi vyote vitaniita aliyebarikiwa,
49 For has done to me (great [things] *N(k)O*) the Mighty One; And holy [is] the name of Him;
kwa maana yeye Mwenye Nguvu amenitendea mambo ya ajabu: jina lake ni takatifu.
50 And the mercy of Him [is] to generations (and *no*) (generations *N(k)O*) to those fearing Him;
Rehema zake huwaendea wale wamchao, kutoka kizazi hadi kizazi.
51 He has shown strength with [the] arm of Him; He has scattered [the] proud in [the] thought of heart of them;
Kwa kuwa ametenda mambo ya ajabu kwa mkono wake; amewatawanya wale wenye kiburi ndani ya mioyo yao.
52 He has brought down rulers from thrones and exalted [the] humble;
Amewashusha watawala toka kwenye viti vyao vya enzi, lakini amewainua wanyenyekevu.
53 [Those] hungering He has filled with good things and [those] being rich He has sent away empty;
Amewashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
54 He has helped Israel [the] servant of Him remembering mercy,
Amemsaidia mtumishi wake Israeli, kwa kukumbuka ahadi yake ya kumrehemu
55 even as He spoke to the fathers of us, to Abraham and to the descendants of him to the age. (aiōn g165)
Abrahamu na uzao wake milele, kama alivyowaahidi baba zetu.” (aiōn g165)
56 Dwelt then Mary with her (about *N(k)O*) months three and returned to the home of her.
Maria akakaa na Elizabeti karibu miezi mitatu, kisha akarudi nyumbani kwake.
57 Now Elizabeth was fulfilled the time to give birth for her and she bore a son.
Ulipowadia wakati wa Elizabeti kujifungua, alizaa mtoto mwanaume.
58 And heard the neighbours and the relatives of her that magnified [the] Lord the mercy of Him with her, and they were rejoicing with her.
Majirani zake na jamii zake wakasikia jinsi Bwana alivyomfanyia rehema kuu, nao wakafurahi pamoja naye.
59 And it came to pass on day the eighth they came to circumcise the child and were calling it after the name of the father of him Zechariah.
Siku ya nane wakaja kumtahiri mtoto, wakataka yule mtoto aitwe Zekaria, ambalo ndilo jina la baba yake.
60 And answering the mother of him said; No, but he will be called John.
Lakini mama yake akakataa na kusema, “Hapana! Jina lake ataitwa Yohana.”
61 And they said to her that No [one] is (among the relatives *N(k)O*) of you who is called the name by this.
Wakamwambia, “Hakuna mtu yeyote katika jamaa yako mwenye jina kama hilo.”
62 They were making signs then to the father of him the what maybe he would wish to be called (him. *N(k)O*)
Basi wakamfanyia Zekaria baba yake ishara ili kujua kwamba yeye angependa kumpa mtoto jina gani.
63 And having asked for a writing tablet he wrote saying; John is (the *ko*) name of him. And they marveled all.
Akaomba wampe kibao cha kuandikia na kwa mshangao wa kila mtu akaandika: “Jina lake ni Yohana.”
64 Was opened then the mouth of him immediately and the tongue of him and he was speaking blessing God.
Papo hapo kinywa chake kikafunguliwa na ulimi wake ukaachiwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
65 And came upon all fear those dwelling around them; and in all the hill country of Judea were being talked about all declarations these,
Majirani wote wakajawa na hofu ya Mungu, na katika nchi yote ya vilima vya Uyahudi watu walikuwa wakinena juu ya mambo haya yote.
66 And laid [them] up all those having heard in the heart of them saying; What then child this will be? And (for *no*) [the] hand of [the] Lord was with him.
Kila aliyesikia habari hizi alishangaa akauliza, “Je, mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
67 And Zechariah the father of him was filled with [the] Spirit Holy and prophesied saying;
Zekaria, baba yake, akajazwa na Roho Mtakatifu, naye akatoa unabii, akisema:
68 Blessed [be] [the] Lord the God of Israel, because He has visited and He has performed redemption [on] the people of Him,
“Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa kuwa amewajilia watu wake na kuwakomboa.
69 and has raised up a horn of salvation for us in (the *k*) house of David (the *k*) servant of Him,
Naye ametusimamishia pembe ya wokovu katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,
70 even as He spoke through [the] mouth of the holy (of the *k*) of [old] age prophets of Him; (aiōn g165)
kama alivyonena kwa vinywa vya manabii wake watakatifu tangu zamani, (aiōn g165)
71 salvation from [the] enemies of us and from [the] hand of all those hating us,
kwamba atatuokoa kutoka kwa adui zetu, na kutoka mikononi mwao wote watuchukiao:
72 to fulfill mercy toward the fathers of us, and to remember [the] covenant holy of Him,
ili kuonyesha rehema kwa baba zetu na kukumbuka Agano lake takatifu,
73 [the] oath that He swore to Abraham the father of us,
kiapo alichomwapia baba yetu Abrahamu:
74 to grant us without fear from [the] hand (of the *k*) enemies (of us *k*) having been saved to serve Him
kutuokoa kutoka mikononi mwa adui zetu, tupate kumtumikia yeye pasipo hofu
75 in holiness and righteousness before Him (all the days *N(k)O*) (of the life *k*) of us.
katika utakatifu na haki mbele zake, siku zetu zote.
76 And you yourself (now, *no*) child, prophet of [the] Most High will be called; you will go for (in front of *N(k)O*) ([the] face of *ko*) [the] Lord to prepare ways of Him,
“Nawe mtoto wangu, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana; kwa kuwa utamtangulia Bwana na kuandaa njia kwa ajili yake,
77 to give knowledge of salvation to the people of Him in forgiveness of [the] sins of them
kuwajulisha watu wake juu ya wokovu utakaopatikana kwa kusamehewa dhambi zao,
78 through [the] affections of compassion of God of us in which (will visit *N(k)O*) us [the] Sunrise from on high,
kwa ajili ya wingi wa rehema za Mungu wetu, nuru itokayo juu itatuzukia
79 to shine upon those in darkness and in [the] shadow of death sitting, to direct the feet of us into [the] way of peace.
ili kuwaangazia wale waishio gizani na katika uvuli wa mauti, kuiongoza miguu yetu katika njia ya amani.”
80 And the child was continuing to grow and he was strengthened in spirit and he was in the deserted places until [the] day of appearance of him to Israel.
Yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu katika roho; akaishi nyikani hadi siku ile alipojionyesha hadharani kwa Waisraeli.

< Luke 1 >