< Luke 2 >

1 It came to pass then in the days those went out a decree from Caesar Augustus to register all the world.
Siku zile Kaisari Augusto alitoa amri kwamba watu wote waandikishwe katika ulimwengu wa Kirumi.
2 This (*k*) registration first took place when is governing Syria Quirinius.
(Orodha hii ndiyo ya kwanza iliyofanyika wakati Krenio alikuwa mtawala wa Shamu).
3 And were going all to be registered, each to the (their own *N(k)O*) city.
Kila mtu alikwenda kuandikishwa katika mji wake alikozaliwa.
4 Went up then also Joseph from Galilee out of [the] town of Nazareth to Judea to [the] City of David which is called Bethlehem, because of being him from [the] house and family of David,
Hivyo Yosefu akapanda kutoka mji wa Nazareti ulioko Galilaya kwenda Uyahudi, mpaka Bethlehemu, mji wa Daudi, kwa sababu yeye alikuwa wa ukoo na wa nyumba ya Daudi.
5 to register with Mary who [was] betrothed to him (wife *k*) she being with child.
Alikwenda huko kujiandikisha pamoja na Maria, ambaye alikuwa amemposa naye alikuwa mjamzito.
6 It came to pass then in their being them there were fulfilled the days of the giving birth of her,
Wakiwa Bethlehemu, wakati wa Maria wa kujifungua ukawa umetimia,
7 And she brought forth the son of her the firstborn and wrapped in swaddling cloths him and she laid Him in (*k*) a manger, because not there was for them a place in the inn.
naye akamzaa mwanawe, kifungua mimba. Akamfunika nguo za kitoto na kumlaza katika hori ya kulia ngʼombe, kwa sababu hapakuwa na nafasi katika nyumba ya wageni.
8 And shepherds were in the region same lodging in the fields and keeping watch by night over the flock of them.
Katika eneo lile walikuwako wachungaji waliokuwa wakikaa mashambani, wakilinda makundi yao ya kondoo usiku.
9 And (behold *KO*) an angel of [the] Lord stood by them, and [the] glory of [the] Lord shone around them, and they feared [with] fear great.
Ghafula tazama, malaika wa Bwana akawatokea, nao utukufu wa Bwana ukawangʼaria kotekote, wakaingiwa na hofu.
10 And said to them the angel; Not do fear; behold for I bring good news to you [of] joy great which will be to all the people
Lakini malaika akawaambia: “Msiogope. Kwa maana tazama nawaletea habari njema za furaha itakayokuwa kwa watu wote.
11 For has been born to you today a Savior who is Christ [the] Lord in [the] City of David.
Leo katika mji wa Daudi kwa ajili yenu amezaliwa Mwokozi, ndiye Kristo Bwana.
12 And this [is] to you the sign: You will find a baby swaddled (and *no*) lying in (*k*) a manger.
Hii ndiyo itakayokuwa ishara kwenu: Mtamkuta mtoto mchanga amefunikwa nguo za kitoto na kulazwa katika hori ya kulia ngʼombe.”
13 And suddenly there came with the angel a multitude of [the] host (heavenly *NK(o)*) praising God and saying:
Ghafula pakawa na jeshi kubwa la mbinguni pamoja na huyo malaika wakimsifu Mungu wakisema,
14 Glory in [the] highest to God, and on earth peace among men (of good-will. *N(k)O*)
“Atukuzwe Mungu juu mbinguni, na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia.”
15 And it came to pass as they were departing from them into the heaven the angels, (and *ko*) the (men *ko*) shepherds (were speaking *N(k)O*) to one another; Let us go through indeed until Bethlehem and let us see declaration this that having happened which the Lord has made known to us.
Hao malaika walipokwisha kuondoka na kwenda zao mbinguni, wale wachungaji wakasemezana wao kwa wao, “Twendeni Bethlehemu tukaone mambo haya ya ajabu yaliyotukia, ambayo Bwana ametuambia habari zake.”
16 And they came having hurried and they found both Mary and Joseph and the baby lying in the manger.
Hivyo wakaenda haraka Bethlehemu, wakawakuta Maria na Yosefu na yule mtoto mchanga akiwa amelala katika hori la kulia ngʼombe.
17 Having seen now (they made known *N(k)O*) concerning the declaration which having been told to them concerning Child this.
Walipomwona yule mtoto, wakawaeleza yale waliyokuwa wameambiwa kuhusu huyo mtoto.
18 And all those having heard they marveled concerning the [things] having been spoken by the shepherds to them.
Nao wote waliosikia habari hizi wakastaajabia yale waliyoambiwa na wale wachungaji wa kondoo.
19 But Mary all was treasuring up declarations these pondering [them] in the heart of her.
Lakini Maria akayaweka mambo haya yote moyoni mwake na kuyatafakari.
20 And (returned *N(k)O*) the shepherds glorifying and praising God for all things which they had heard and seen even as it was said to them.
Wale wachungaji wakarudi, huku wakimtukuza Mungu na kumsifu kwa ajili ya mambo yote waliyokuwa wameambiwa na kuyaona.
21 And when were fulfilled days eight to circumcise (Him *no*) (the child *K*) then was called the name of Him Jesus, which He had been called by the angel before conceiving He in the womb.
Hata zilipotimia siku nane, ulikuwa ndio wakati wa kumtahiri mtoto, akaitwa Yesu, jina alilokuwa amepewa na malaika kabla hajatungwa mimba.
22 And when were fulfilled the days of the purification of them according to the law of Moses, they brought Him to Jerusalem to present to the Lord
Ulipotimia wakati wa utakaso wake Maria kwa mujibu wa Sheria ya Mose, basi Yosefu na Maria walimpeleka mtoto Yerusalemu, ili kumweka wakfu kwa Bwana
23 even as it has been written in [the] law of [the] Lord that Every male opening a womb holy to the Lord will be called;
(kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Bwana, kwamba, “Kila mtoto wa kiume kifungua mimba atawekwa wakfu kwa Bwana”),
24 and to offer a sacrifice according to that said in (the *no*) law of [the] Lord; A pair of turtle doves or two young pigeons.
na pia kutoa dhabihu kulingana na yale yaliyonenwa katika Sheria ya Bwana: “Hua wawili au makinda mawili ya njiwa.”
25 And behold a man there was in Jerusalem whose name [was] Simeon and man this [was] righteous and devout waiting for [the] consolation of Israel; and [the] Spirit was Holy upon him.
Basi alikuwako huko Yerusalemu mtu mmoja jina lake Simeoni, ambaye alikuwa mwenye haki na mcha Mungu, akitarajia faraja ya Israeli, na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake.
26 And it was to him revealed by the Spirit Holy not to see death before than (when *no*) he may see the Christ of [the] Lord
Roho Mtakatifu alikuwa amemfunulia kuwa hatakufa kabla hajamwona Kristo wa Bwana.
27 And he came in the Spirit into the temple; and in the [time when] bringing in the parents the child Jesus for the [thing] [were] doing they according to that accustomed by the law for Him,
Simeoni, akiwa ameongozwa na Roho Mtakatifu, alikwenda Hekaluni. Wazazi walipomleta mtoto Yesu ili kumfanyia kama ilivyokuwa desturi ya Sheria,
28 then he himself received Him into the arms (of him *ko*) and blessed God and said:
ndipo Simeoni akampokea mtoto mikononi mwake na kumsifu Mungu, akisema:
29 Now You dismiss the servant of You, Lord, according to the declaration of You in peace
“Bwana Mwenyezi, kama ulivyoahidi, sasa wamruhusu mtumishi wako aende zake kwa amani.
30 for have seen the eyes of mine the salvation of You
Kwa maana macho yangu yameuona wokovu wako,
31 which You have prepared before [the] face of all the peoples,
ulioweka tayari machoni pa watu wote,
32 a light for revelation of [the] Gentiles and glory of [the] people of You of Israel.
nuru kwa ajili ya ufunuo kwa watu wa Mataifa na kwa ajili ya utukufu kwa watu wako Israeli.”
33 And were (the *no*) (father *N(K)O*) of Him and the mother marveling at the [things] being spoken concerning Him.
Naye Yosefu na mama yake mtoto wakastaajabu kwa yale yaliyokuwa yamesemwa kumhusu huyo mtoto.
34 And blessed them Simeon and said to Mary the mother of Him: Behold this [Child] is appointed for [the] falling and rising up of many in Israel and for a sign spoken against.
Kisha Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, “Mtoto huyu amewekwa kwa makusudi ya kuanguka na kuinuka kwa wengi katika Israeli. Atakuwa ishara ambayo watu watanena dhidi yake,
35 and of you also of her the soul will go through a sword — so that maybe may be revealed of many hearts [the] thoughts.
ili mawazo ya mioyo mingi yadhihirike. Nao upanga utauchoma moyo wako.”
36 And there was Anna a prophetess, daughter of Phanuel, of [the] tribe of Asher; she having advanced in years great, having lived with a husband years seven from the marriage of herself;
Tena alikuwako Hekaluni nabii mmoja mwanamke, jina lake Ana binti Fanueli, wa kabila la Asheri. Alikuwa mzee sana; naye alikuwa ameolewa na kuishi na mume kwa miaka saba tu, kisha mumewe akafa.
37 and she [was] a widow (until *N(k)O*) years eighty [and] four who not was departing (from *k*) the temple with fastings and prayers serving night and day;
Hivyo alikuwa mjane na umri wake ulikuwa miaka themanini na minne. Yeye hakuondoka humo Hekaluni usiku wala mchana, bali alikuwa akimwabudu Mungu, akifunga na kuomba.
38 And (this *k*) she at that hour having come up she was giving praise (to God *N(K)O*) and was speaking concerning Him to all those waiting for [the] redemption (in *k*) of Jerusalem.
Wakati huo huo, Ana alikuja akaanza kusifu, akimshukuru Mungu na kusema habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wakitarajia ukombozi wa Yerusalemu.
39 And when they had performed (everything *N(k)O*) according to the law of [the] Lord, (they returned *N(k)O*) to Galilee to (the *k*) town (of themselves *N(k)O*) Nazareth.
Yosefu na Maria walipokuwa wamekamilisha mambo yote yaliyotakiwa na Sheria ya Bwana, walirudi mjini kwao Nazareti huko Galilaya.
40 And the Child was continuing to grow and He was being strengthened (in spirit *K*) being filled (with wisdom, *N(k)O*) and [the] grace of God was upon Him.
Naye yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu, akiwa amejaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa juu yake.
41 And were going the parents of Him every year to Jerusalem at the feast of the Passover.
Kila mwaka Yosefu na Maria mama yake Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kwa ajili ya Sikukuu ya Pasaka.
42 And when He was years [old] twelve (when were going up *N(k)O*) they (into Jerusalem *KO*) according to the custom of the Feast
Yesu alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, walipanda kwenda kwenye Sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi.
43 and when having completed the days in the returning of them remained behind Jesus the boy in Jerusalem, But not (knew *N(k)O*) (the parents *NO*) (Joseph and the mother *K*) of Him.
Baada ya Sikukuu kumalizika, wakati Yosefu na Maria mama yake walipokuwa wakirudi nyumbani, Yesu alibaki Yerusalemu lakini hawakutambua.
44 Having supposed now Him to be in their company they went a day’s journey and were seeking Him among the relatives and (in *k*) the acquaintances.
Wao wakidhani kuwa yuko miongoni mwa wasafiri, walienda mwendo wa kutwa nzima. Ndipo wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa zao na marafiki.
45 and not having found (Him *k*) they returned to Jerusalem (searching *N(k)O*) Him.
Walipomkosa walirudi Yerusalemu ili kumtafuta.
46 And it came to pass after days three they found Him in the temple sitting in [the] midst of the teachers both hearing them and questioning them.
Baada ya siku tatu wakamkuta ndani ya Hekalu, akiwa ameketi katikati ya walimu wa sheria, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
47 Were amazed then all those hearing Him at the understanding and at the answers of Him.
Wote waliomsikia walistaajabishwa na uwezo wake mkubwa wa kuelewa, na majibu aliyoyatoa.
48 And having seen Him they were astonished, and said to Him the mother of Him: Child why You did to us thus? Behold the father of You and I myself and I myself distressing (were seeking *NK(o)*) You.
Yosefu na Maria mama yake walipomwona walishangaa. Mama yake akamuuliza, “Mwanangu, mbona umetufanyia hivi? Tazama, mimi na baba yako tumekuwa tukikutafuta kwa wasiwasi mkubwa kila mahali.”
49 And He said to them; Why [is it] for you were seeking Me? Surely you knew that in the [house] of the Father of Mine it behooves to be Me?
Yesu akawaambia, “Kwa nini kunitafuta? Hamkujua kwamba imenipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?”
50 And they themselves not understood the declaration that He spoke to them.
Lakini wao hawakuelewa maana ya lile alilowaambia.
51 And He went down with them and He came to Nazareth and He was subject to them. And the mother of Him was treasuring up all declaration (these *ko*) in the heart of her.
Ndipo akashuka pamoja nao hadi Nazareti, naye alikuwa mtiifu kwao. Lakini mama yake akayaweka moyoni mwake mambo haya yote.
52 And Jesus was continuing to advance (in *n*) (*no*) wisdom and stature and in favor with God and men.
Naye Yesu akakua katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu.

< Luke 2 >