< Job 6 >

1 And he answered Job and he said.
Kisha Ayubu akajibu:
2 Certainly [if] it will be weighed grief my (and destruction my *Q(K)*) in [the] balances people will raise together.
“Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa, nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
3 For now more than [the] sand of [the] seas it will be heavy there-fore words my they have been rash.
Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote, kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
4 For [the] arrows of [the] Almighty [are] with me which poison their [is] drinking spirit my [the] terrors of God they are arranged against me.
Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
5 ¿ Does it bray a wild donkey on grass or? does it low an ox on fodder its.
Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani, au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula?
6 ¿ Is it eaten tasteless [food] because not salt or? [is] there taste in [the] slime of purslane.
Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi, au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
7 It refuses to touch [them] self my they [are] like [the] illness of food my.
Ninakataa kuvigusa; vyakula vya aina hii hunichukiza.
8 Who? will he give it will come petition my and hope my he will give God.
“Laiti ningepata haja yangu, kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
9 And may he be willing God and may he crush me may he loosen hand his and may he cut off me.
kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda, kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
10 And may it be still - comfort my and may I jump in anguish [which] not it relents that not I have hidden [the] words of [the] holy [one].
Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
11 What? [is] strength my that I will wait and what? [is] end my that I will prolong life my.
“Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini? Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
12 [the] strength of Stones [is] strength my or? [is] flesh my bronze.
Je, mimi nina nguvu za jiwe? Je, mwili wangu ni shaba?
13 ¿ If not [is] help my in myself and sound wisdom it has been banished from me.
Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe, wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
14 [belongs] to Despairing [person] from friend his loyalty and [the] fear of [the] Almighty he will forsake.
“Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.
15 Brothers my they have acted treacherously like a wadi like a stream-bed of wadis [which] they pass away.
Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika
16 That are dark from ice over them it hides itself snow.
wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo, ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
17 At [the] time [when] they flow they are silenced in heat its they are dried up from place their.
lakini hukauka majira ya ukame, na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
18 They twist [the] paths of way their they go up in the wasteland so they may perish.
Misafara hugeuka kutoka njia zake; hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
19 They look [the] caravans of Tema [the] travelers of Sheba they look eagerly for them.
Misafara ya Tema inatafuta maji, wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri hutazama kwa matarajio.
20 They are disappointed for he had been confident they come to it and they were disappointed.
Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini; wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
21 For now you have become (it *Q(K)*) you have seen a terror and you were afraid.
Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote; mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
22 ¿ For have I said give for me and from wealth your give a reward for me.
Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu, au mnilipie fidia kutoka mali zenu,
23 And rescue me from [the] hand of an opponent and from [the] hand of ruthless [people] you will ransom me.
au niokoeni mikononi mwa adui, au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
24 Teach me and I I will keep silent and what? have I erred explain to me.
“Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya; nionyesheni nilikokosea.
25 How! they are painful words of uprightness and what? does it prove completely from you.
Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli! Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
26 ¿ To reprove words do you plan and to wind [the] words of [one who] despairs.
Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema, na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
27 Even on a fatherless one you will make fall and you may bargain on friend your.
Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali.
28 And therefore be willing turn on me and on faces your if I will lie.
“Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi. Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
29 Turn back please may not it be injustice (and turn back *Q(K)*) still righteousness my [is] in it.
Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu; angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.
30 ¿ [is] there On tongue my injustice or? palate my not does it discern destruction.
Je, pana uovu wowote midomoni mwangu? Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?

< Job 6 >