< Psalms 64 >

1 “For the leader of the music. A psalm of David.” Hear my voice, O God! when I pray! Preserve my life from the terrors of the enemy!
Sikia sauti yangu, Mungu, usikilize malalamiko yangu; unilinde dhidi ya hofu ya adui zangu.
2 Hide me from the assembly of the wicked, From the brawling crowd of evil-doers!
Unifiche dhidi ya mipango ya siri ya wafanyao maovu, unifiche dhidi ya watendao vurugu ya udhalimu.
3 For like a sword they sharpen their tongues, Like arrows they aim their poisoned words,
Wao wamenoa ndimi zao kama panga; wamelenga mishale yao, maneno machungu,
4 To shoot in secret at the upright; Suddenly do they shoot at him without fear.
ili kwamba waweze kupiga kutoka mahali pa siri kwenda kwa mtu asiye na hatia; wampige yeye kwa ghafla nao wasihofu lolote.
5 They prepare themselves for an evil deed; They commune of laying secret snares: “Who,” say they, “will see them?”
Wao wanahamasishana wenyewe katika kupanga uovu; wanashauriana pamoja wao binafsi ili kuweka mitego; nao husema, “Ni nani atakayetuona?”
6 They meditate crimes: “We have finished,” say they, “our plans!” The heart and bosom of every one of them are deep.
Wanabuni mipango ya dhambi; “Tumemaliza,” wanasema, “ni mpango makini.” Mawazo ya ndani na mioyo ya watu ni ya kina.
7 But God will shoot an arrow at them; Suddenly shall they be wounded.
Lakini Mungu atawapiga wao; ghafla watajeruhiwa kwa mishale yake.
8 Thus their own tongues shall bring them down; All who see them will flee away.
Watafanywa kuwa mashakani, kwa kuwa ndimi zao wenyewe ziko kinyume nao; wote wawaonao watatikisa vichwa vyao.
9 Then will all men stand in awe, And declare what God hath done, And attentively consider his work.
Watu wote wataogopa na kutangaza matendo ya Mungu. Kwa hekima watafikiria kuhusu kile yeye ametenda.
10 The righteous shall rejoice, and trust in the LORD; All the upright in heart shall glory.
Wenye haki watakuwa na furaha kuhusu Yahwe nao watakimbilia kwake; wote wenye haki moyoni watajivuna katika yeye.

< Psalms 64 >