< Job 12 >

1 Then Job answered and said:
Ndipo Ayubu akajibu na kusema,
2 No doubt ye are the whole people! And wisdom will die with you!
“Hakuna shaka ninyi wanadamu; Hekima mtakufa nayo.
3 But I have understanding as well as you; I am not inferior to you: Yea, who knoweth not such things as these?
Lakini nina ufahamu kama vile ninyi; Mimi siyo duni kwenu. Ni dhhiri, ni nani asiyefahamu vitu hivyo kama hivi?
4 I am become a laughing-stock to my friend, —I who call upon God, that he would answer me! The innocent and upright man is held in derision.
Mimi ni kitu cha kuchekwa na jirani-Mimi, ni mmoja aliyemwita Mungu na ambaye alijibiwa na yeye! Mimi, ni mwenye haki na mtu asiyekuwa na hatia-Mimi sasa nimekuwa kitu cha kuchekwa.
5 To calamity belongeth contempt in the mind of one at ease; It is ready for them that slip with the feet.
Katika mawazo yake mtu fulani aliye katika kufurahi, kuna kudharau kwa mashaka; hufikiri katika njia ambayo huleta mambo mabaya zaidi kwa wale ambao miguu yao inateleza.
6 The tents of robbers are in prosperity, And they who provoke God are secure, Who carry their God in their hand.
Hema za wezi hufanikiwa, na wale ambao humkasirisha Mungu huhisi salama; mikono yao wenyewe ni miungu wao.
7 For ask now the beasts, and they will teach thee; Or the fowls of the air, and they will tell thee;
Lakini sasa waulize hao wanyama wa mwituni, na watakufundisha wewe; waulize ndege wa angani, na watakuambia wewe.
8 Or speak to the earth, and it will instruct thee; And the fishes of the sea will declare unto thee.
Au iambie ardhi, na itakufundisha wewe; samaki wa baharini watakutangazia wewe.
9 Who among all these doth not know That the hand of Jehovah doeth these things?
Ni myama yupi miongoni mwa hawa asiyefahamu kuwa mkono wa Yahwe umetenda haya?
10 In whose hand is the soul of every living thing, And the breath of all mankind.
Katika mkono wake mna uzima wa kila kiumbe hai na pumzi ya wanadamu wote.
11 Doth not the ear prove words, As the mouth tasteth meat?
Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile kaakaa lionjavyo chakula chake?
12 With the aged is wisdom, And with length of days is understanding.
Kwa wazee mna hekima; katika wingi wa siku mna ufahamu.
13 With Him are wisdom and strength; With Him counsel and understanding.
Pamoja na Mungu mna hekima na ukuu; yeye anayo mashauri na ufahamu.
14 Lo! he pulleth down, and it shall not be rebuilt; He bindeth a man, and he shall not be set loose.
Tazama, yeye huangusha chini, na haiwezekani kujengwa tena; kama yeye akimtia gerezani mtu yeyote, hakutakuwa tena kufunguliwa.
15 Lo! he withholdeth the waters, and they are dried up; He sendeth them forth, and they lay waste the earth.
Tazama, kama yeye akiyazuia maji, yanakauka; na kama akiyaachilia nje yanaitaabisha ardhi.
16 With him are strength and wisdom; The deceived and the deceiver are his.
Pamoja na yeye mna nguvu na hekima; watu ambao wamedanganywa na mdanganyi wote pamoja wako katika nguvu zake.
17 He leadeth counsellors away captive, And judges he maketh fools.
Yeye huwaongoza washauri mbali bila kuvaa viatu katika huzuni; huwarudisha hakimu katika upumbavu.
18 He looseth the authority of kings, And bindeth their loins with a cord.
Yeye Huondoa minyororo ya mamlaka kutoka kwa wafalme; yeye hufunika viuno vyao kwa nguo.
19 He leadeth priests away captive, And overthroweth the mighty.
Yeye huwaongoza makuhani mbali bila kuvaa viatu na kuwapindua watu wakuu.
20 He removeth speech from the trusty, And taketh away judgment from the elders.
Yeye huondoa hotuba ya wale waliokuwa wameaminiwa na huondoa mbali ufahamu wa wazee.
21 He poureth contempt upon princes, And looseth the girdle of the mighty.
Yeye humwaga aibu juu ya binti za wafalme na hufungua mishipi ya watu wenye nguvu.
22 He revealeth deep things out of darkness, And bringeth the shadow of death to light.
Yeye huweka wazi vitu vya kina kutoka katika giza na kuvileta nje kumuika vivuli mahali ambapa watu waliokufa wapo.
23 He exalteth nations, and destroyeth them; He enlargeth nations, and leadeth them captive.
Yeye huyafanya mataifa kuwa na nguvu, na pia huyaharibu; Yeye pia huyakuza mataifa, na pia yeye huyaongoza mbali kama wafungwa.
24 He taketh away the understanding of the great men of the land, And causeth them to wander in a wilderness, where is no path;
Yeye huondoa mbali ufahamu kutoka kwa viongozi wa watu wa nchi; huwafanya wao kutangatanga msituni mahali pasipo na njia.
25 They grope in the dark without light; He maketh them stagger like a drunken man.
Wao wanapapasa katika giza bila kuwa na mwanga; yeye huwafanya wao kuweweseka kama mtu mlevi.

< Job 12 >