< Psalms 29 >
1 “A psalm of David.” Give to Jehovah, O ye sons of God! Give to Jehovah glory and praise!
Zaburi ya Daudi. Mpeni Bwana, enyi mashujaa, mpeni Bwana utukufu na nguvu.
2 Give to Jehovah the glory due to his name; Worship Jehovah in holy attire!
Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake; mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.
3 The voice of Jehovah is heard above the waters; The God of glory thundereth, -Jehovah above the great waters.
Sauti ya Bwana iko juu ya maji; Mungu wa utukufu hupiga radi, Bwana hupiga radi juu ya maji makuu.
4 The voice of Jehovah is powerful; The voice of Jehovah is full of majesty;
Sauti ya Bwana ina nguvu; sauti ya Bwana ni tukufu.
5 The voice of Jehovah breaketh the cedars; Yea, Jehovah breaketh the cedars of Lebanon;
Sauti ya Bwana huvunja mierezi; Bwana huvunja vipande vipande mierezi ya Lebanoni.
6 Yea, he maketh them to leap like a calf, —Lebanon and Sirion like a young buffalo.
Hufanya Lebanoni irukaruke kama ndama, Sirioni urukaruke kama mwana nyati.
7 The voice of Jehovah divideth the flames of fire.
Sauti ya Bwana hupiga kwa miali ya umeme wa radi.
8 The voice of Jehovah maketh the wilderness tremble; Yea, Jehovah maketh the wilderness of Kadesh tremble.
Sauti ya Bwana hutikisa jangwa; Bwana hutikisa Jangwa la Kadeshi.
9 The voice of Jehovah maketh the hinds bring forth, And layeth bare the forests; While, in his palace, every one declareth his glory.
Sauti ya Bwana huzalisha ayala, na huuacha msitu wazi. Hekaluni mwake wote wasema, “Utukufu!”
10 Jehovah sitteth above the flood; Yea, Jehovah sitteth king for ever.
Bwana huketi akiwa ametawazwa juu ya gharika; Bwana ametawazwa kuwa Mfalme milele.
11 Jehovah will give strength to his people; Jehovah will bless his people with peace.
Bwana huwapa watu wake nguvu; Bwana huwabariki watu wake kwa kuwapa amani.