< Psalms 28 >

1 “A psalm of David.” To thee do I cry, O LORD! O my rock! be not silent to me, Lest, if thou answer me not, I become like those who go down to the pit!
Zaburi ya Daudi. Ninakuita wewe, Ee Bwana, Mwamba wangu; usiwe kwangu kama kiziwi. Kwa sababu ukinyamaza nitafanana na walioshuka shimoni.
2 Hear the voice of my supplication, when I cry unto thee, When I lift up my hands to thy most holy sanctuary!
Sikia kilio changu unihurumie ninapokuita kwa ajili ya msaada, niinuapo mikono yangu kuelekea Patakatifu pa Patakatifu pako.
3 Draw me not away with the impious, and with evil-doers, Who speak peace to their neighbors, while mischief is in their hearts!
Usiniburute pamoja na waovu, pamoja na hao watendao mabaya, ambao huzungumza na jirani zao maneno mazuri, lakini mioyoni mwao wameficha chuki.
4 Give them according to their deeds, and the wickedness of their doings; Give them according to the work of their hands; Render to them their desert!
Walipe sawasawa na matendo yao, sawasawa na matendo yao maovu; walipe sawasawa na kazi za mikono yao, uwalipe wanavyostahili.
5 For they regard not the doings of the LORD, nor the work of his hands; Therefore will he destroy them, and not again build them up.
Kwa kuwa hawaheshimu kazi za Bwana, na yale ambayo mikono yake imetenda, atawabomoa na kamwe hatawajenga tena.
6 Praised be the LORD, for he hath heard the voice of my supplications!
Bwana asifiwe, kwa maana amesikia kilio changu nikimwomba anihurumie.
7 The LORD is my strength and my shield; My heart trusteth in him, and he helpeth me; Therefore doth my heart exult, And in my song I will praise him.
Bwana ni nguvu zangu na ngao yangu, moyo wangu umemtumaini yeye, nami nimesaidiwa. Moyo wangu unarukaruka kwa furaha nami nitamshukuru kwa wimbo.
8 Jehovah is the strength of his people; He is the protecting shield of his anointed.
Bwana ni nguvu ya watu wake, ngome ya wokovu kwa mpakwa mafuta wake.
9 Save thy people, and bless thine inheritance; Feed them also, and build them up for ever!
Waokoe watu wako na uubariki urithi wako; uwe mchungaji wao na uwabebe milele.

< Psalms 28 >