< Psalms 2 >

1 Why do the heathen rage, And the nations meditate a vain thing?
Kwa nini mataifa wanafanya dhoruba, kwa nini watu wanafanya njama ambazo zitafeli?
2 Why do the kings of the earth rise up, And the princes combine together, Against Jehovah, and against his anointed king?
Wafalme wa nchi kwa pamoja hushikilia misimamo yao na watawala kwa pamoja hufanya njama kinyume na Yahwe na kinyume na Masihi, wakisema,
3 “Let us break their bonds asunder; Let us cast away from us their fetters!”
“Ngoja tuzikate pingu walizo tufingia sisi na kuzitupa pingu zao.”
4 He that sitteth in heaven will laugh; The Lord will have them in derision.
Yeye aketie katika mbingu atacheka kwa dharau mbele yao; Bwana atawadhihaki wao.
5 Then shall he speak to them in his wrath, And confound them in his hot displeasure.
Kisha ataongea nao katika hasira yake na kuwaogofya kwa gadhabu yake, akisema,
6 “I myself have anointed my king, Upon Zion, my holy hill!”
“Mimi mwenyewe nilimpaka mafuta mfalme wa Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
7 I will declare the decree of Jehovah: He hath said to me, “Thou art my son; This day I have begotten thee.
Nami nitatangaza amri ya Yahwe. Yeye aliniambia, “wewe ni mwanangu! Leo hii nimekuwa baba yako.
8 Ask of me, and I will give thee the nations for thine inheritance, And the ends of the earth for thy possession.
Uniombe, nami nitakupa wewe taifa kwa ajili ya urithi na mikoa ya nchi iliyo bora kwa ajili ya umiliki wako.
9 Thou shalt break them with a rod of iron; Thou shalt dash them in pieces like a potter's vessel.”
Wewe utawavunja wao kwa fimbo ya chuma; kama vile mtungi wa mfinyanzi, wewe utawavunja wao vipande vipande.”
10 Be wise, therefore, O ye kings! Be admonished, ye rulers of the earth!
Hivyo sasa, ninyi wafalme; mchukue tahadhari; mjirekebishe.
11 Be subject to Jehovah with awe, And fear with trembling!
Mwabuduni Yahwe kwa hofu na mfurahi mkitetemeka.
12 Kiss the son, lest He be angry, and ye perish in your way; For soon shall his wrath be kindled. Happy are all they who seek refuge in him.
Mumbusu mwana vinginevyo atawakasirikia, na mtakufa pale pale hasira yake ikiwaka. Ni jinsi gani wamebarikiwa wale wote watafutao usalama ndani yake.

< Psalms 2 >