< Job 32 >
1 So these three men ceased to answer Job, because he was righteous in his own eyes.
Hivyo hawa watu watatu walikoma kumjibu Ayubu kwasababu alikuwa ni mwenye haki katika macho yake mwenyewe.
2 Then was kindled the wrath of Elihu, the son of Barachel, the Buzite, of the family of Ram; against Job was his wrath kindled, because he accounted himself righteous rather than God.
Ndipo iliwaka hasira ya Elihu mwana wa Barakeli Mbuzi, wa familia ya Ramu, iliwaka dhidi ya Ayubu kwa kuwa alijihesabia haki mwenyewe kuliko Mungu.
3 Against his three friends also was his wrath kindled, because they had not found an answer, and yet had condemned Job.
Hasira ya Elihu iliwaka pia kinyume cha marafiki zake watatu kwasababu hawakupata jibu kwa ajili ya Ayubu, na bado walimhukumu Ayubu.
4 Now Elihu had delayed to reply to Job, because they were older than himself.
Sasa Elihu alikuwa amemsubiri Ayubu ili aweze kuzungumza naye kwa kuwa watu wengine walikuwa wakubwa kuliko yeye.
5 But when Elihu saw that there was no answer in the mouth of these three men, his wrath was kindled.
Hata hivyo, wakati Elihu alipoona ya kuwa hapakuwa na jibu katika midomo ya watu hawa watatu, hasira yake iliwaka.
6 Then spake Elihu, the son of Barachel, the Buzite, and said: I am young, and ye are very old; Therefore I was afraid, And durst not make known to you my opinion.
Ndipo Elihu mwana wa Barakeli Mbuzi alinena na kusema, “Mimi ni mdogo, na ninyi ni wazee. Hii ndio sababu nilijizuia na sikuthubutu kuzungumza mawazo yangu mwenyewe.
7 I said, “Days should speak, And the multitude of years should teach wisdom.”
Nilisema, “Urefu wa siku utazungumza; na wingi wa miaka utatufundisha hekima.
8 But it is the spirit in man, Even the inspiration of the Almighty, that giveth him understanding.
Lakini kuna roho ndani ya mtu; pumzi ya Mwenye nguvu humpa yeye ufahamu.
9 Great men are not always wise, Nor do the aged always understand what is right.
Si tu watu wakubwa ndio wenye hekima, wala watu wazee pekee ambao hufahamu haki.
10 Therefore, I pray, listen to me: I also will declare my opinion.
Hivyo basi nakwambia wewe, “Nisikilizeni mimi; Nitakwambia pia uelewa wangu.'
11 Behold, I have waited for your words, I have listened to your arguments, Whilst ye searched out what to say;
Tazama, niliyasubiria maneno yenu; nilisikiliza hoja zenu wakati mlipokuwa mnafikiri juu ya kile cha kusema.
12 Yea, I have attended to you; And behold, none of you hath refuted Job, Nor answered his words.
Hakika, niliwajali sana ninyi, lakini, tazama, hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kumshawishi Ayubu wala ambaye aliweza kumjibu maneno yake.
13 Say not, then, “We have found out wisdom; God must conquer him, not man.”
Iweni waangalifu msije mkasema, 'Tumepata hekima!' Mungu atakuwa amemshinda Ayubu; mtu wa kawaida hawezi akafanya hivyo.
14 He hath not directed his discourse against me, And with speeches like yours will I not answer him.
Kwa kuwa Ayubu hajasema mojamoja maneno yake juu yangu, basi sitamjibu kwa maneno yenu.
15 They were confounded! they answered no more! They could say nothing!
Hawa watu watatu wamep igwa bumbuwazi; hawawezi kuendelea kumjibu Ayubu; hawana neno zaidi la kusema.
16 I waited, but they spake not; They stood still; they answered no more!
Je ninapaswa kusubiria kwasababu hawazungumzi, kwa kuwa wamesimama pale kimya na wala hawajibu zaidi?
17 Therefore will I answer, on my part; I also will show my opinion.
La, nitajibu pia upande wangu; Nitawaambia pia ufahamu wangu.
18 For I am full of matter; The spirit within me constraineth me.
Kwa kuwa nimejawa na maneno mengi, roho ndani yangu inanisukuma.
19 Behold, my bosom is as wine that hath no vent; Like bottles of new wine, which are bursting.
Tazama, kifua changu ni kama divai yenye chachu ambayo haina tundu; kama viriba vipya, kiko tayari kupasuka.
20 I will speak, that I may be relieved; I will open my lips and answer.
Nitazungumza ili kwamba niweze kuburudishwa; nitafungua kimya changu na kusema.
21 I will not be partial to any man's person, Nor will I flatter any man.
Sitaonesha upendeleo; wala sitatoa sifa za majina kwa mtu yeyote.
22 For I know not how to flatter; Soon would my Maker take me away.
Kwa kuwa sijui namna ya kutoa sifa; kama nitafanya hivyo, Muumba wangu atanikatilia mimi mbali.