< Acts 3 >

1 And Peter and John were going up together to the temple, at the hour of prayer, which is the ninth hour.
Siku moja Petro na Yohana walikuwa wanapanda kwenda Hekaluni kusali yapata saa tisa alasiri.
2 And a certain man lame from his birth was carried along, whom they laid daily at the gate of the temple which is called Beautiful, to ask alms of those who entered the temple;
Basi palikuwa na mtu mmoja aliyekuwa kiwete tangu kuzaliwa. Alichukuliwa na kuwekwa kwenye lango la Hekalu liitwalo Zuri, kila siku ili aombe msaada kwa watu wanaoingia Hekaluni.
3 who, seeing Peter and John about to go into the temple, asked alms.
Huyu mtu alipowaona Petro na Yohana wakikaribia kuingia Hekaluni, akawaomba wampe sadaka.
4 And Peter fixing his eyes upon him, with John, said, Look upon us.
Wakamkazia macho, kisha Petro akamwambia, “Tutazame sisi.”
5 And he gave heed to them, expecting to receive something from them.
Hivyo yule mtu akawatazama, akitazamia kupata kitu kutoka kwao.
6 Then Peter said, Silver and gold have I none; but what I have I give thee. In the name of Jesus Christ the Nazarene, rise up and walk.
Ndipo Petro akamwambia, “Sina fedha wala dhahabu, lakini nilicho nacho ndicho nikupacho. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, tembea!”
7 And grasping him by the right hand, he raised him up; and immediately his feet and ankles received strength.
Petro akamshika yule mtu kwa mkono wa kuume akamwinua, mara nyayo zake na vifundo vya miguu yake vikapata nguvu.
8 And leaping forth he stood, and walked, and entered with them into the temple, walking and leaping, praising God.
Akaruka juu na kusimama, akaanza kutembea. Kisha akaingia Hekaluni pamoja na Petro na Yohana, huku akitembea na kurukaruka na kumsifu Mungu.
9 And all the people saw him walking, and praising God;
Watu wote walipomwona akitembea na kumsifu Mungu,
10 and they recognized him as the man that sat for alms at the Beautiful Gate of the temple; and they were filled with wonder and amazement at that which had happened to him.
wakamtambua kuwa ni yule mtu aliyekuwa akiketi nje ya Hekalu penye lango liitwalo Zuri akiomba msaada, nao wakajawa na mshangao, wakastaajabu juu ya yale yaliyomtukia.
11 And as he held fast to Peter and John, all the people ran together to them in the porch that is called Solomon's greatly wondering.
Aliyeponywa alipokuwa akiambatana na Petro na Yohana, watu wote walishangaa mno, wakaja wakiwakimbilia pale ukumbi wa Solomoni.
12 But Peter seeing it, answered the people: Men of Israel, why wonder ye at this? Or why look ye earnestly on us, as though by our own power or godliness we had made this man to walk?
Petro alipoona watu wamekusanyika akawaambia, “Enyi Waisraeli, kwa nini mnastaajabu kuhusu jambo hili? Mbona mnatukazia macho kwa mshangao kana kwamba ni kwa uwezo wetu au utakatifu wetu tumemfanya mtu huyu kutembea?
13 The God of Abraham and Isaac and Jacob, the God of our fathers, hath glorified his servant Jesus, whom ye indeed delivered up, and denied him in the presence of Pilate, when he had decided to release him.
Mungu wa Abrahamu na Isaki na Yakobo, Mungu wa baba zetu amemtukuza Mwanawe Yesu, ambaye ninyi mlimtoa ahukumiwe kifo na mkamkana mbele ya Pilato, ingawa yeye alikuwa ameamua kumwachia aende zake.
14 But ye denied the holy and righteous one, and asked that a murderer should be granted to you.
Ninyi mlimkataa huyo Mtakatifu na Mwenye Haki mkaomba mpewe yule muuaji.
15 But the author of life ye killed; whom God raised from the dead, whereof we are witnesses.
Hivyo mkamuua aliye chanzo cha uzima, lakini Mungu akamfufua kutoka kwa wafu. Sisi tu mashahidi wa mambo haya.
16 And his name, through faith in his name, made this man strong, whom ye see and know; yea, the faith which is through him gave him this perfect soundness in the presence of you all.
Kwa imani katika jina la Yesu, huyu mtu mnayemwona na kumfahamu ametiwa nguvu. Ni kwa jina la Yesu na imani itokayo kwake ambayo imemponya kabisa huyu mtu, kama ninyi wote mnavyoona.
17 And now, brethren, I know that ye acted in ignorance, as did also your rulers.
“Sasa ndugu zangu, najua ya kuwa ninyi mlitenda bila kujua, kama walivyofanya viongozi wenu.
18 But God thus fulfilled what he had before announced by the mouth of all the prophets, that his Christ should suffer.
Lakini kwa njia hii Mungu alitimiza kile ambacho alikuwa ametabiri kwa vinywa vya manabii wake wote, kwamba Kristo atateswa.
19 Repent therefore and turn from your ways, that your sins may be blotted out, in order that the times of refreshing may come from the presence of the Lord,
Tubuni basi mkamgeukie Mungu, dhambi zenu zifutwe, ili zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwepo kwake Bwana,
20 and that he may send forth Christ Jesus, who was before appointed for you;
naye apate kumtuma Kristo, ambaye ameteuliwa kwa ajili yenu, yaani Yesu.
21 whom heaven indeed must receive until the times of a restoration of all things; of which times God spoke by the mouth of his holy prophets from the days of old. (aiōn g165)
Ilimpasa mbingu zimpokee mpaka wakati wa kufanywa upya kila kitu, kama Mungu alivyoahidi zamani kupitia kwa vinywa vya manabii wake watakatifu. (aiōn g165)
22 Moses indeed said, “A prophet will the Lord your God raise up to you from among your brethren, as be raised up me; him shall ye hear in all things, whatever he shall speak to you.
Kwa maana Mose alisema, ‘Bwana Mungu wenu atawainulia nabii kama mimi kutoka miongoni mwa ndugu zenu. Itawapasa kumtii huyo kwa kila jambo atakalowaambia.
23 And it shall come to pass, that every soul which doth not hear that prophet shall be utterly destroyed from among the people.”
Mtu yeyote ambaye hatamsikiliza huyo nabii, atatupiliwa mbali kabisa na watu wake.’
24 And all the prophets also, Samuel and those who followed, as many as spoke, announced these days.
“Naam, manabii wote tangu Samweli na waliokuja baada yake, wote walitabiri kuhusu siku hizi.
25 Ye are the sons of the prophets, and of the covenant which God made with our fathers, saying to Abraham, “And in thy posterity shall all the families of the earth be blessed.”
Ninyi ndio wana wa manabii na wa Agano ambalo Mungu alifanya na baba zenu, akimwambia Abrahamu, ‘Kupitia kwa uzao wako, watu wote wa ulimwengu watabarikiwa.’
26 To you first, God, having raised up his servant, sent him to bless you in turning away every one of you from your iniquities.
Mungu alipomfufua Yesu Mwanawe, alimtuma kwenu kwanza, ili awabariki kwa kumgeuza kila mmoja wenu kutoka njia yake mbaya.”

< Acts 3 >