< Romans 2 >
1 Therefore, you are inexcusable, O man—everyone who is judging—for in that in which you judge the other, yourself you condemn, for the same things you practice who are judging,
Kwa hiyo hauna udhuru, wewe uhukumuye, kwa maana katika yale uhukumuyo mwingine wajitia hatiani mwenyewe. Kwa maana wewe uhukumuye unafanya mambo yale yale.
2 and we have known that the judgment of God is according to truth, on those practicing such things.
Lakini twajua kwamba hukumu ya Mungu ni ya kweli juu yao wafanyao mambo kama hayo.
3 And do you think this, O man, who are judging those who such things are practicing, and are doing them, that you will escape the judgment of God?
Lakini wewe tafakari hili, wewe ambaye unahukumu wale wanaotenda mambo hayo ingawa nawe unafanya mambo yayo hayo. Je utaepuka hukumu ya Mungu?
4 Or the riches of His goodness, and forbearance, and long-suffering, do you despise, not knowing that the goodness of God leads you to conversion?
Au unafikiri kidogo sana juu ya wingi wa wema wake, kuchelewa kwa adhabu yake, na uvumilivu wake? Je, hujui kwamba wema wake unapaswa kukuelekeza katika toba?
5 But according to your hardness and impenitent heart, you treasure up wrath to yourself in [the] day of wrath and of the revelation of the righteous judgment of God,
Bali kwa kadiri ya ugumu wako na kwa moyo wako usio na toba wajiwekea mwenyewe akiba ya ghadhabu kwa siku ile ya ghadhabu, yaani, siku ile ya ufunuo wa hukumu ya haki ya Mungu.
6 who will render to each according to his works;
Yeye atamlipa kila mtu kipimo sawa na matendo yake:
7 to those, indeed, who in continuance of a good work, seek glory, and honor, and incorruptibility—continuous life; (aiōnios )
kwa wale ambao kwa uthabiti wa matendo mema wametafuta sifa, heshima na kutokuharibika, atawapa uzima wa milele. (aiōnios )
8 and to those contentious, and disobedient, indeed, to the truth, and obeying the unrighteousness—indignation and wrath,
Lakini kwa wale ambao ni wabinafsi, wasioitii kweli bali hutii dhuluma, ghadhabu na hasira kali itakuja.
9 tribulation and distress, on every soul of man that is working the evil, both of Jew first, and of Greek;
Mungu ataleta dhiki na shida juu ya kila nafsi ya binadamu aliyefanya uovu, kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia.
10 and glory, and honor, and peace, to everyone who is working the good, both to Jew first, and to Greek.
Lakini sifa, heshima na amani itakuja kwa kila mtu atendaye mema, kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia.
11 For there is no favor by appearance with God,
Kwa maana hakuna upendeleo kwa Mungu.
12 for as many as sinned without law, will also perish without law, and as many as sinned in law, through law will be judged,
Kwa maana kama vile wengi waliokosa pasipo sheria watapotea pasipo sheria, na kama vile wengi waliokosa kulingana na sheria watahukumiwa kwa sheria.
13 for not the hearers of the Law [are] righteous before God, but the doers of the Law will be declared righteous.
Maana si wasikiaji wa sheria walio wenye haki mbele za Mungu, bali ni wale waitendao sheria watakaohesabiwa haki.
14 For when nations that have no law, by nature may do the things of the Law, these not having a law—to themselves are a law,
Kwa maana watu wa Mataifa, ambao hawana sheria, wanafanya kwa asili mambo ya sheria, wao, wamekuwa sheria kwa nafsi zao, ingawa wao hawana sheria.
15 who show the work of the Law written in their hearts, their conscience also witnessing with them, and between one another the thoughts accusing or else defending,
Kwa hili wanaonesha kwamba matendo yanayohitajika kwa mujibu wa sheria yameandikwa ndani ya mioyo yao. Dhamiri zao pia zinawashuhudia wao, na mawazo yao wenyewe ama huwashitaki au huwalinda wao wenyewe
16 in the day when God will judge the secrets of men, according to my good news, through Jesus Christ.
na pia kwa Mungu. Haya yatatokea katika siku ambayo Mungu atazihukumu siri za watu wote, sawasawa na injili yangu, kwa njia ya Yesu Kristo.
17 Behold, you are named a Jew, and rest on the Law, and boast in God,
Tuseme kwamba unajiita mwenyewe Myahudi, aliyekaa katika sheria, shangilia kwa kujisifu katika Mungu,
18 and know the will, and approve the distinctions, being instructed out of the Law,
yajue mapenzi yake, na kupima mambo ambayo yanatofautiana nayo, baada ya kuagizwa na sheria.
19 and have confidence that you yourself are a leader of blind ones, a light of those in darkness,
Na tuseme kwamba una ujasiri kwamba wewe mwenyewe ni kiongozi wa kipofu, mwanga kwa wale walio gizani,
20 a corrector of foolish ones, a teacher of babies, having the form of the knowledge and of the truth in the Law.
msahihishaji wa wajinga, mwalimu wa watoto, na kwamba unayo katika sheria jinsi ya elimu na kweli.
21 You, then, who are teaching another, do you not teach yourself?
Wewe basi, uhubiriye mwingine, je, hujifundishi mwenyewe? Wewe uhubiriye kutokuiba, je wewe huiba?
22 You who are preaching not to steal, do you steal? You who are saying not to commit adultery, do you commit adultery? You who are abhorring the idols, do you rob temples?
Wewe usemae usizini, je unazini? Wewe uchukiaye sanamu, je unaiba hekaluni?
23 You who boast in the Law, through the transgression of the Law do you dishonor God?
Wewe ujisifuye katika sheria, je haumfedheheshi Mungu katika kuvunja sheria?
24 For evil is spoken of the Name of God among the nations because of you, according as it has been written.
Kwa maana “jina la Mungu linafedheheshwa kati ya watu wa mataifa kwa sababu yenu,” kama ilivyoandikwa.
25 For circumcision, indeed, profits, if you may practice law, but if you may be a transgressor of law, your circumcision has become uncircumcision.
Kwa maana Kutahiriwa kweli kwafaa kama ukitii sheria, lakini kama wewe ni mkiukaji wa sheria, kutahiriwa kwako kunakuwa kutokutahiriwa.
26 If, therefore, the uncircumcision may keep the righteousness of the Law, will not his uncircumcision be reckoned for circumcision?
Basi, ikiwa, mtu asiyetahiriwa anaendelea kushika matakwa ya sheria, je kutokutahiriwa kwake hakutachukuliwa kana kwamba ametahiriwa?
27 And the uncircumcision, by nature, fulfilling the Law, will judge you who, through letter and circumcision, [are] a transgressor of law.
Na yeye asiyetahiriwa kwa asili hatakuhukumu kama akitimiza sheria? Hii ni kwa sababu una maandiko yaliyoandikwa na tohara pia lakini bado u mkiukaji wa sheria!
28 For he is not a Jew who is [so] outwardly, neither [is] circumcision that which is outward in flesh;
Kwa maana yeye si Myahudi aliye kwa hali ya nje; wala kutahiriwa si kule ambako ni kwa nje tu katika mwili.
29 but a Jew [is] he who is [so] inwardly, and circumcision [is] of the heart, in spirit, not in letter, of which the praise is not of men, but of God.
Lakini yeye ni Myahudi aliye kwa ndani, na tohara ni ya moyo, katika roho, si katika andiko. Sifa ya mtu wa namna hiyo haitokani na watu bali yatoka kwa Mungu.