< 1 Corinthians 1 >
1 Paul, a called apostle of Jesus Christ, through the will of God, and Sosthenes the brother,
Paulo, aliyeitwa na Kristo Yesu kuwa mtume kwa mapenzi ya Mungu, na Sosthene ndugu yetu,
2 to the Assembly of God that is in Corinth, to those sanctified in Christ Jesus, called holy ones, with all those calling on the Name of our Lord Jesus Christ in every place—both theirs and ours:
kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, kwa wale ambao wamewekwa wakfu katika Yesu Kristo, ambao wameitwa kuwa watu watakatifu. Tunawaandikia pia wale wote wanaoliitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo katika mahali pote, Bwana wao na wetu.
3 Grace to you and peace from God our Father and the Lord Jesus Christ!
Neema na amani iwe kwenu kutoka kwa Mungu baba yetu na Bwana wetu Yesu Kristo.
4 I give thanks to my God always concerning you for the grace of God that was given to you in Christ Jesus,
Siku zote namshukru Mungu wangu kwa ajili yenu, kwa sababu ya neema ya Mungu ambayo Kristo Yesu aliwapa.
5 that in everything you were enriched in Him, in all discourse and all knowledge,
Amewafanya kuwa matajiri katika kila njia, katika usemi na pamoja maarifa yote.
6 according as the testimony of the Christ was confirmed in you,
Amewafanya matajiri, kama ushuhuda kuhusu Kristo ya kwamba amethibitishwa kuwa kweli miongoni mwenu.
7 so that you are not behind in any gift, waiting for the revelation of our Lord Jesus Christ,
Kwa hiyo hampungukiwi karama za kiroho, kama mlivyo na hamu ya kusubiri ufunuo wa Bwana wetu Yesu Kristo.
8 who also will confirm you to the end—unblamable in the day of our Lord Jesus Christ;
Atawaimarisha ninyi pia hadi mwisho, ili msilaumiwe siku ya Bwana wetu Yesu Kristo.
9 faithful [is] God, through whom you were called into the fellowship of His Son Jesus Christ our Lord.
Mungu ni mwaminifu ambaye aliwaita ninyi katika ushirika wa mwana wake, Yesu Kristo Bwana wetu.
10 And I call on you, brothers, through the Name of our Lord Jesus Christ, that the same thing you may all say, and there may not be divisions among you, and you may be perfected in the same mind, and in the same judgment,
Sasa nawasihi kaka na dada zangu, kupitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba wote mkubali, na kwamba kusiwe na migawanyiko miongoni mwenu. Nawasihi kwamba muungane pamoja katika nia moja na katika kusudi moja.
11 for it was signified to me concerning you, my brothers, by those of Chloe, that contentions are among you;
Kwani watu wa nyumba ya Kloe wamenitaarifu kuwa kuna mgawanyiko unaoendelea miongoni mwenu.
12 and I say this, that each one of you says, “I, indeed, am of Paul,” and “I of Apollos,” and “I of Cephas,” and “I of Christ.”
Nina maana hii: Kila mmoja wenu husema, “Mimi ni wa Paulo,” au “Mimi ni wa Apolo”, au “Mimi ni wa Kefa” au “Mimi ni wa Kristo”.
13 Has the Christ been divided? Was Paul crucified for you? Or were you immersed into the name of Paul?
Je! Kristo amegawanyika? Je! Paulo alisulubiwa kwa ajili yenu? Je! Mlibatizwa kwa jina la Paulo?
14 I give thanks to God that I immersed no one of you, except Crispus and Gaius—
Namshukuru Mungu kuwa sikumbatiza yeyote, isipokuwa Krispo na Gayo.
15 that no one may say that to my own name I immersed;
Hii ilikuwa kwamba hakuna yeyote angesema mlibatizwa kwa jina langu.
16 and I also immersed Stephanas’ household—further, I have not known if I immersed any other.
(Pia niliwabatiza wa nyumba ya Stephania. Zaidi ya hapo, sijui kama nilimbatiza mtu mwingine yeyote).
17 For Christ did not send me to immerse, but to proclaim good news, not in wisdom of discourse, that the Cross of the Christ may not be made of no effect;
Kwa kuwa, Kristo hakunituma kubatiza bali kuhubiri injili. Hakunituma kuhubiri kwa maneno ya hekima ya kibinadamu, ili kwamba nguvu ya msalaba wa Kristo isiondolewe.
18 for the word of the Cross to those indeed perishing is foolishness, and to us—those being saved—it is the power of God,
Kwa kuwa ujumbe wa msalaba ni upuuzi kwa wale wanaokufa. Lakini kwa wale ambao Mungu anawaokoa, ni nguvu ya Mungu.
19 for it has been written: “I will destroy the wisdom of the wise, and the intelligence of the intelligent I will bring to nothing”;
Kwa kuwa imeandikwa, “Nitaiharibu hekima ya wenye busara. Nitauharibu ufahamu wa wenye akili.”
20 where [is] the wise? Where the scribe? Where a disputer of this age? Did God not make foolish the wisdom of this world? (aiōn )
Yuko wapi mtu mwenye busara? Yuko wapi mwenye elimu? Yuko wapi msemaji mshawishi wa dunia hii? Je, Mungu hakuigeuza hekima ya dunia hii kuwa ujinga? (aiōn )
21 For seeing in the wisdom of God the world through the wisdom did not know God, it pleased God through the foolishness of the preaching to save those believing.
Tangu dunia imekuwa katika hekima yake haikumjua Mungu, ilimpendeza Mungu katika ujinga wao wa kuhubiri ili kuokoa wale wanaoamini.
22 Since also Jews ask a sign, and Greeks seek wisdom,
Kwa Wayahudi huuliza ishara za miujiza na kwa Wayunani hutafuta hekima.
23 also we preach Christ crucified, to Jews, indeed, a stumbling-block, and to Greeks foolishness,
Lakini tunamhubiri Kristo aliyesulubiwa, aliye kikwazo kwa Wayahudi na ni ujinga kwa Wayunani.
24 and to those called—both Jews and Greeks—Christ the power of God, and the wisdom of God,
Lakini kwa wale ambao waliitwa na Mungu, Wayahudi na Wayunani, tunamhubiri Kristo kama nguvu na hekima ya Mungu.
25 because the foolishness of God is wiser than men, and the weakness of God is stronger than men;
Kwa kuwa ujinga wa Mungu una hekima kuliko ya wanadamu, na udhaifu wa Mungu una nguvu zaidi ya wanadamu.
26 for see your calling, brothers, that not many [are] wise according to the flesh, not many mighty, not many noble;
Angalia wito wa Mungu juu yenu, kaka na dada zangu. Si wengi wenu mlikuwa na hekima katika viwango vya kibinadamu. Si wengi wenu mlikuwa na nguvu. Si wengi wenu mlizaliwa katika ukuu.
27 but God chose the foolish things of the world that He may put the wise to shame; and God chose the weak things of the world that He may put the strong to shame;
Lakini Mungu alichagua vitu vijinga vya dunia ili kuviaibisha vyenye hekima. Mungu alichagua kilicho dhaifu katika dunia kukiaibisha chenye nguvu.
28 and God chose the base things of the world, and the things despised, and the things that are not, that He may make useless the things that are—
Mungu alichagua kile kilicho cha hali ya chini na kilichodharauliwa katika dunia. Alichagua hata vitu ambavyo havikuhesabiwa kuwa kitu, kwa kuvifanya si kitu vitu vilivyo na thamani.
29 that no flesh may glory before Him;
Alifanya hivi ili asiwepo yeyote aliye na sababu ya kujivuna mbele zake.
30 but out of Him you are in Christ Jesus, who became to us from God wisdom, righteousness also, and sanctification, and redemption,
Kwa sababu ya kile Mungu alichofanya, sasa mko ndani ya Kristo Yesu, ambaye amefanyika hekima kwa ajili yetu kutoka kwa Mungu. Alikuwa haki yetu, utakatifu na ukombozi.
31 that, according as it has been written: “He who is glorying—let him glory in the LORD.”
Kama matokeo, kama andiko lisemavyo, “Anayejisifu, ajisifu katika Bwana.”