< Romans 10 >

1 Brothers, the pleasure indeed of my heart, and my supplication that [is] to God for Israel, is—for salvation;
Ndugu, nia ya moyo wangu na ombi langu kwa Mungu ni kwa ajili yao, kwa ajili ya wokovu wao.
2 for I bear them testimony that they have a zeal of God, but not according to knowledge,
Kwa kuwa nawashuhudia kwamba wanajuhudi kwa ajili ya Mungu, lakini si kwa ajili ya ufahamu.
3 for not knowing the righteousness of God, and seeking to establish their own righteousness, they did not submit to the righteousness of God.
Kwa kuwa hawajui haki ya Mungu, na wanatafuta kujenga haki yao wenyewe. Hawakuwa watiifu kwa haki ya Mungu.
4 For Christ is an end of law for righteousness to everyone who is believing,
Kwa kuwa Kristo ndiye utimilifu wa sheria kwa ajili ya haki ya kila mtu aaminiye.
5 for Moses describes the righteousness that [is] of the Law, that, “The man who did them will live in them,”
Kwa kuwa Musa anaandika kuhusu haki ambayo huja kutokana na sheria: “Mtu ambaye hutenda haki ya sheria ataishi kwa haki hii.”
6 and the righteousness of faith thus speaks: “You may not say in your heart, Who will go up to Heaven?” (that is, to bring Christ down)
Lakini haki ambayo inatokana na imani husema hivi, “Usiseme moyoni mwako, 'Nani atapaa kwenda mbinguni?' (Hii ni kumleta Kristo chini).
7 or, “Who will go down to the abyss?” (that is, to bring up Christ out of the dead). (Abyssos g12)
Na usiseme, 'Nani atashuka katika shimo?”' (Hii ni, kumleta Kristo juu kutoka kwa wafu). (Abyssos g12)
8 But what does it say? “The saying is near you—in your mouth, and in your heart”: that is, the saying of the faith that we preach;
Lakini inasema nini? “Neno liko karibu na wewe, katika kinywa chako na katika moyo wako.” Hilo ni neno la imani, ambalo tunatangaza.
9 that if you may confess with your mouth that Jesus [is] LORD, and may believe in your heart that God raised Him out of the dead, you will be saved,
Kwa kuwa kama kwa kinywa chako unamkiri Yesu ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako kwamba Mungu alimfufua kutoka kwa wafu, utaokoka.
10 for with the heart [one] believes to righteousness, and with the mouth is confession made to salvation;
Kwa kuwa kwa moyo mtu huamini na kupata haki, na kwa kinywa hukiri na kupata wokovu.
11 for the Writing says, “Everyone who is believing on Him will not be ashamed,”
Kwa kuwa andiko lasema, “Kila amwaminiye hata aibika.”
12 for there is no difference between Jew and Greek, for the same Lord of all [is] rich to all those calling on Him,
kwa kuwa hakuna tofauti kati ya Myahudi na Myunani. Kwa kuwa Bwana yule yule ni Bwana wa wote, na ni tajiri kwa wote wamwitao.
13 for “Everyone who, if he may have called on the Name of the LORD, will be saved.”
Kwa kuwa kila mtu ambaye huliitia jina la Bwana ataokoka.
14 How then will they call on [Him] in whom they did not believe? And how will they believe [on Him] of whom they did not hear? And how will they hear apart from one preaching?
Kwa jinsi gani wanaweza kumwita yeye ambaye hawajamwamini? Na jinsi gani wanaweza kuamini katika yeye ambaye hawajamsikia? Na watasikiaje pasipo muhubiri?
15 And how will they preach, if they may not be sent? According as it has been written: “How beautiful the feet of those proclaiming good tidings of peace, of those proclaiming good tidings of the good things!”
Na jinsi gani wanaweza kuhubiri, isipokuwa wametumwa? - Kama ilivyoandikwa, “Jinsi gani ni mizuri miguu ya wale ambao wanatangaza habari za furaha za mambo mema!”
16 But they were not all obedient to the good tidings, for Isaiah says, “LORD, who gave credence to our report?”
Lakini wote hawakusikiliza injili. Kwa kuwa Isaya hunena, “Bwana, ni nani aliyesikia ujumbe wetu?”
17 So then faith [is] by a report, and the report through a saying of God,
Hivyo imani huja kutokana na kusikia, na kusikia kwa neno la Kristo.
18 but I say, did they not hear? Yes, indeed, “their voice went forth to all the earth, and their sayings to the ends of the habitable world.”
Lakini nasema, “Je hawakusikia?” Ndiyo, kwa hakika sana. “Sauti yao imekwisha toka nje katika nchi yote, na maneno yao kwenda miisho ya dunia.”
19 But I say, did Israel not know? First Moses says, “I will provoke you to jealousy by [that which is] not a nation, By an unintelligent nation I will anger you,”
Zaidi ya yote, Ninasema, “Je Israel hakujua?” Kwanza Musa hunena, “Nitawachokoza kuwatia wivu kwa watu ambao si taifa. Kwa njia ya taifa lisilo na uelewa, nitawachochea hadi mkasirike.”
20 and Isaiah is very bold and says, “I was found by those not seeking Me; I became visible to those not inquiring after Me”;
Na Isaya ni jasiri sana na husema, “Nilipatikana na wale ambao hawakunitafuta. Nilionekana kwa wale ambao hawakunihitaji.”
21 and to Israel He says, “All the day I stretched out My hands to a people unbelieving and contradicting.”
Lakini kwa Israel husema, “Siku zote nilinyoosha mikono yangu kwa wasiotii na kwa watu wagumu.”

< Romans 10 >