< Job 38 >

1 And after Elius had ceased from speaking, the Lord spoke to Job through the whirlwind and clouds, [saying],
Ndipo Yahweh alimwita Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kumwambia,
2 Who is this that hides counsel from me, and confines words in [his] heart, and thinks to conceal [them] from me?
“Huyu ni nani aletaye giza katika mipango kwa njia ya maneno bila maarifa?
3 Gird your loins like a man; and I will ask you, and do you answer me.
Basi sasa jifunge kiunoni mwako kama mwanaume kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
4 Where was you when I founded the earth? tell me now, if you have knowledge,
Wewe ulikuwa wapi wakati nilipoitandaza misingi ya dunia? Niambie, kama unao ufahamu zaidi.
5 who set the measures of it, if you know? or who stretched a line upon it?
Je ni nani aliyeamuru vipimo vyake? Niambie, kama unajua, ni nani alivinyosha vipimo juu yake?
6 On what are its rings fastened? and who is he that laid the corner-stone upon it?
Misingi yake ilitandazwa juu ya nini? Ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni
7 When the stars were made, all my angels praised me with a loud voice.
wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?
8 And I shut up the sea with gates, when it rushed out, coming forth out its mother's womb.
Ni nani huifunga bahari kwa milango wakati inapofurika, kana kwamba inatoka katika tumbo,
9 And I made a cloud its clothing, and swathed it in mist.
wakati nilipoyafanya mawingu kuwa ni mavazi yake, na giza nene kuwa mkanda wake wa kujifungia?
10 And I set bounds to it, surrounding it with bars and gates.
Hapo ilikuwa wakati nilipoweka bahari mpaka wangu, na nilipoweka makomeo yake na milango,
11 And I said to it, Hitherto shall you come, but you shall not go beyond, but your waves shall be confined within you.
na wakati nilipoiambia, 'Unaweza kuja hapa kutoka mbali, lakini si zaidi; na hapa ndipo nitauweka mpaka kwa fahari ya mawimbi yako.'
12 Or did I order the morning light in your time; and [did] the morning star [then first] see his appointed place;
Je tangu mwanzo wa siku zako, ulishawahi kuigiza asubuhi ianze, na kuyafanya mapambazuko yajue sehemu yake katika mpangilio wa vitu,
13 to lay hold of the extremities of the earth, to cast out the ungodly out of it?
ili kwamba ishikilie sehemu za dunia ili watu waovu watikiswe mbali nayo.
14 Or did you take clay of the ground, and form a living creature, and set it with the power of speech upon the earth?
Dunia imebadilishwa katika mwonekano kama udongo unavyobadilika chini ya muhuri; vitu vyote husimama juu yake dhahiri kama cha kibindo cha nguo.
15 And have you removed light from the ungodly, and crushed the arm of the proud?
'Mwanga' wao umeondolewa kutoka kwa watu waovu; na mkono wao ulioinuliwa umevunjwa.
16 Or have you gone to the source of the sea, and walked in the tracks of the deep?
Je umeshaenda kwenye vyanzo vya maji ya bahari? Je umeshatembea sehemu za chini kabisa za kilindi?
17 And do the gates of death open to you for fear; and did the porters of hell quake when they saw you? (questioned)
Je malango ya mauti yamefunuliwa kwako? Je umeshaona malango ya uvuli wa mauti?
18 And have you been instructed in the breadth of the [whole earth] under heaven? tell me now, what is the extent of it?
Je umeifahamu dunia katika upana wake? Niambie kama unayajua yote hayo.
19 And in what kind of a land does the light dwell? and of what kind is the place of darkness?
Je iko wapi njia ya sehemu ya kupumzikia kwa mwanga, na kama ilivyo kwa giza, iko wapi sehemu yake?
20 If you could bring me to their [utmost] boundaries, and if also you know their paths;
Je unaweza kuuongoza mwanga na giza katika sehemu zake za kazi? Waweza kuitambua njia ya kurudi katika nyumba zao?
21 I know then that you were born at that time, and the number of your years is great.
Bila shaka unajua, kwa kuwa ulizaliwa wakati huo; hesabu ya siku zako ni kubwa sana!
22 But have you gone to the treasures of snow? and have you seen the treasures of hail?
Je ulishaingia katika ghala ya barafu, au umeshaiona ghala ya mawe ya mvua,
23 And is there a store [of them], for you against the time of [your] enemies, for the day of wars and battle?
vitu hivi nimeviweka kwa ajili ya siku za mateso, kwa siku za mapigano na vita?
24 And whence proceeds the frost? or [whence] is the south wind dispersed over the [whole world] under heaven?
Je iko wapi njia ya mshindo wa mwanga hutokea au je upepo husambazwa kutoka mashariki juu ya dunia?
25 And who prepared a course for the violent rain, and a way for the thunders;
Ni nani aliyezitengeneza mifereji ya gharika ya mvua, au ni nani aliyezifanya njia za milipuko ya radi,
26 to rain upon the land where [there is] no man, the wilderness, where there is not a man in it; so as to feed the untrodden and uninhabited [land],
na kuifanya mvua inyeshe juu ya nchi ambazo hakuna mtu aishiye ndani yake, na juu ya jangwa, ambayo ndani yake hakuna mtu yeyote,
27 and cause it to send forth a crop of green herbs?
kwa kusudi la kutimiza mahitaji ya mikoa iliyo kame na yenye ukiwa, na kuyastawisha majani mororo?
28 Who is the rain's father? and who has generated the drops of dew?
Je kuna baba wa mvua? Ni nani aliyeyafanya matone ya umande?
29 And out of whose womb comes the ice? and who has produced the frost in the sky,
Je barafu ilitoka katika tumbo la nani? Na ni nani aliyeizaa theluji nyeupe katika anga?
30 which descends like flowing water? who has terrified the face of the ungodly?
Maji hujificha menyewe na kuwa kama jiwe; sehemu za juu za vilindi huwa kama barafu.
31 And do you understand the band of Pleias, and have you opened the barrier of Orion?
Je unaweza kuzifunga minyororo ya Kilimia, au kuvifungua vifundo vya Orioni?
32 Or will you reveal Mazuroth in his season, and the evening star with his rays? Will you guide them?
Je unaweza kuziongoza nyota kutokea katika nyakati zake? Je waweza kuongoza dubu pamoja na watoto wake?
33 And know you the changes of heaven, or the events which take place together under heaven?
Je unazijua sheria za anga? Wewe uliweza kuanzisha sheria za anga juu ya dunia?
34 And will you call a cloud with your voice, and will it obey you with a violent shower of much rain?
Je waweza kupaza sauti yako hadi mawinguni, ili kwamba maji mengi ya mvua yakufunike?
35 And will you send lightnings, and they shall go? and shall they say to you, What is [your pleasure]?
Je waweza kuagiza miali ya mwanga ili itokee, na kukwambia, 'Sisi tupo hapa'?
36 And who has given to women skill in weaving, or knowledge of embroidery?
Ni nani ameweka hekima katika mawingu au ni nani ameweka ufahamu kwa ukungu?
37 And who is he that numbers the clouds in wisdom, and has bowed the heaven [down] to the earth?
Nani anaweza kuyahesabu mawingu kwa maarifa yake? Na ni nani awezaye kuvimwaga viriba vya anga
38 For it is spread out as dusty earth, and I have cemented it as one hewn stone to another.
wakati mavumbi yanapoungana kuwa kitu kigumu na mabonge ya dunia yanaposhikama kwa pamoja?
39 And will you hunt a prey for the lions? and satisfy the desires of the serpents?
Je waweza kuwinda mawindo kwa ajili ya simba jike au kutosheleza hamu ya watoto wadogo wa simba
40 For they fear in their lairs, and lying in wait couch in the woods.
wakati wanapokwaruza kwaruza katika pango lao na kukaa katika kificho ili kulala katika hali ya kuvizia?
41 And who has prepared food for the raven? for its young ones wander and cry to the Lord, in search of food.
Ni nani aletaye mawindo kwa ajili ya kunguru wakati ambapo watoto wao wanapomlilia Mungu na kutangatanga kwa kukosa chakula?

< Job 38 >