< Psalms 49 >

1 For the Leader; a Psalm of the sons of Korah. Hear this, all ye peoples; give ear, all ye inhabitants of the world,
Sikieni hili, ninyi watu wote; tegeni masikio, ninyi wenyeji wa dunia,
2 Both low and high, rich and poor together.
wote walio chini na walio juu, tajiri na masikini wote pamoja.
3 My mouth shall speak wisdom, and the meditation of my heart shall be understanding.
Mdomo wangu utazungumza hekima na tafakari ya moyo wangu itakuwa ya uelewa.
4 I will incline mine ear to a parable; I will open my dark saying upon the harp.
Nitaelekeza sikio langu kwenye mfano; nitaanza mfano wangu kwa kinubi.
5 Wherefore should I fear in the days of evil, when the iniquity of my supplanters compasseth me about,
Kwa nini nilazimike kuziogopa siku za uovu, wakati uovu umenizunguka kwenye visigino vyangu?
6 Of them that trust in their wealth, and boast themselves in the multitude of their riches?
Kwa nini niwaogope wale wanao amini katika mali zao na kujivuna kuhusu utajiri wao?
7 No man can by any means redeem his brother, nor give to God a ransom for him —
Ni hakika kuwa hakuna yeyote atakaye muokoa ndugu yake au kumpa Mungu pesa kwa ajili yake,
8 For too costly is the redemption of their soul, and must be let alone for ever —
Kwa maana ukombozi wa uhai wa mtu ni gharama kubwa, na hakuna awezaye kulipa kile tunacho daiwa.
9 That he should still live alway, that he should not see the pit.
Hakuna yeyote atakaye ishi milele ili mwili wake usioze.
10 For he seeth that wise men die, the fool and the brutish together perish, and leave their wealth to others.
Maana yeye ataona uozo. Watu wenye hekima hufa; wajinga pia huangamia na kuacha mali zao kwa wengine.
11 Their inward thought is, that their houses shall continue for ever, and their dwelling-places to all generations; they call their lands after their own names.
Mawazo yao ya ndani ni kuwa familia zao zitaishi milele, na mahali waishipo, kwa vizazi vyote; wanaita ardhi zao kwa majina yao wenyewe.
12 But man abideth not in honour; he is like the beasts that perish.
Lakini mtu, kuwa na mali, haimaanishi atabaki hai; kama wanyama walioangamia.
13 This is the way of them that are foolish, and of those who after them approve their sayings. (Selah)
Hii ni hatma ya wafanyao ujinga baada ya kufa, .................
14 Like sheep they are appointed for the nether-world; death shall be their shepherd; and the upright shall have dominion over them in the morning; and their form shall be for the nether-world to wear away, that there be no habitation for it. (Sheol h7585)
Kama kondoo wamechaguliwa kwa ajili ya kuzimu na kifo kitakuwa mchungaji wao. Nao watatawaliwa na wenye haki ifikapo asubuhi, na miili yao italiwa kuzimuni, wakiwa hawana afasi ya kuishi kwa ajili yao. (Sheol h7585)
15 But God will redeem my soul from the power of the nether-world; for He shall receive me. (Selah) (Sheol h7585)
Bali Mungu ataufufua uhai wangu kutoka katika nguvu ya kuzimu; naye atanipokea. (Selah) (Sheol h7585)
16 Be not thou afraid when one waxeth rich, when the wealth of his house is increased;
Msifadhaike mtu awapo tajiri, utukufu wa nyumba yake uongezekapo.
17 For when he dieth he shall carry nothing away; his wealth shall not descend after him.
Maana atakapo kufa hataondoka na chochote; utukufu wake hautamfuata yeye.
18 Though while he lived he blessed his soul: 'Men will praise thee, when thou shalt do well to thyself';
Yeye huifurahisha nafsi yake awapo hai na watu hukusifu wewe uishipo maisha yako mwenyewe-
19 It shall go to the generation of his fathers; they shall never see the light.
naye atakwenda kwenye ukoo wa baba zake naye kamwe hataiona nuru tena.
20 Man that is in honour understandeth not; he is like the beasts that perish.
Yule ambaye ana mali lakini hana ufahamu ni kama wanyama, ambao wataangamia.

< Psalms 49 >