< Psalms 69 >

1 For the Leader; upon Shoshannim. A Psalm of David. Save me, O God; for the waters are come in even unto the soul.
Uniokoe, Mungu; maana maji yameweka uhai wangu hatarini.
2 I am sunk in deep mire, where there is no standing; I am come into deep waters, and the flood overwhelmeth me.
Ninazama kwenye kina cha matope, pasipo na hahari pa kusimama; nimekuja kwenye kina kirefu cha maji, ambako mafuriko yananifunika.
3 I am weary of my crying; my throat is dried; mine eyes fail while I wait for my God.
Nimechoka sana kwa kulia kwangu; koo langu ni kavu; macho yangu yanafifia wakati namngoja Mungu wangu.
4 They that hate me without a cause are more than the hairs of my head; they that would cut me off, being mine enemies wrongfully, are many; should I restore that which I took not away?
Wale wanichukiao bila sababu wako zaidi ya nywele za kichwa changu; wale ambao wangeweza kuniua, wakiwa adui zangu kwa sababu zisizo sahihi, ni wengi mno; wanalazimisha nirudishe kile ambacho sijaiba.
5 O God, Thou knowest my folly; and my trespasses are not hid from Thee.
Mungu, wewe unaujua ujinga wangu, na dhambi zangu hazifichiki kwako.
6 Let not them that wait for Thee be ashamed through me, O Lord GOD of hosts; let not those that seek Thee be brought to confusion through me, O God of Israel.
Usiwaache wale wanao kungoja wewe waaibishwe kwa sababu yangu, Bwana Yahwe wa majeshi; usiwaache wale wanaokutafuta wewe wadharauliwe kwa sababu yangu, Mungu wa Israeli.
7 Because for Thy sake I have borne reproach; confusion hath covered my face.
Kwa ajili yako nimestahimili lawama; aibu imeufunika uso wangu.
8 I am become a stranger unto my brethren, and an alien unto my mother's children.
Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, nisiye fahamika wala kuaminika kwa watoto wa mama yangu.
9 Because zeal for Thy house hath eaten me up, and the reproaches of them that reproach Thee are fallen upon me.
Kwa maana bidii ya nyumba yako imenila, na laumu zao wanao kulaumu wewe zimeniangukia mimi.
10 And I wept with my soul fasting, and that became unto me a reproach.
Wakati nilipolia na kutokula chakula, walinitukana.
11 I made sackcloth also my garment, and I became a byword unto them.
Nilipoteneneza mavazi ya gunia, nikawa kituko kwao.
12 They that sit in the gate talk of me; and I am the song of the drunkards.
Wale wakaao katika lango la mji huniseng'enya; mimi ni wimbo wa walevi.
13 But as for me, let my prayer be unto Thee, O LORD, in an acceptable time; O God, in the abundance of Thy mercy, answer me with the truth of Thy salvation.
Lakini kwangu mimi, maombi yangu ni kwako, Yahwe, wakati ambao wewe utayapokea; unijibu katika uaminifu wa wokovu wako.
14 Deliver me out of the mire, and let me not sink; let me be delivered from them that hate me, and out of the deep waters.
Unitoe matopeni, na usiniache nizame; uniondoe mbali na wale wanaonichukia na uniokoe katika kina cha maji.
15 Let not the waterflood overwhelm me, neither let the deep swallow me up; and let not the pit shut her mouth upon me.
Usiache mafuliko ya maji yanielemee, wala kina kisinimeze. Usiache mdomo wa shimo unimeze.
16 Answer me, O LORD, for Thy mercy is good; according to the multitude of Thy compassions turn Thou unto me.
Unijibu, Yahwe, maana uaminifu wa agano lako ni mwema; kwa maana rehema zako kwangu ni nyingi, unigeukie.
17 And hide not Thy face from Thy servant; for I am in distress; answer me speedily.
Usiufiche uso wako mbali na mtumishi wako, maana niko katika dhiki; unijibu haraka.
18 Draw nigh unto my soul, and redeem it; ransom me because of mine enemies.
Uje kwangu na unikomboe. Kwa sababu ya adui zangu, uwe fidia yangu.
19 Thou knowest my reproach, and my shame, and my confusion; mine adversaries are all before Thee.
Wewe wajua kulaumiwa kwangu, kuaibishwa kwangu, na kudharauliwa kwangu; wapinzani wangu wote wako mbele yako.
20 Reproach hath broken my heart; and I am sore sick; and I looked for some to show compassion, but there was none; and for comforters, but I found none.
Lawama imevunja moyo wangu; nimejawa na huzuni kubwa; nilitafuta mtu wa kunihurumia, lakini hakuwepo; nilitafuta wafariji, lakini sikupata.
21 Yea, they put poison into my food; and in my thirst they gave me vinegar to drink.
Walinipa sumu kwa ajili ya chakula changu; katika kiu yangu walinipa siki ninywe.
22 Let their table before them become a snare; and when they are in peace, let it become a trap.
Meza yao mbele yao na iwe mtego; wafikiripo wako kwenye usalama, iwe kitanzi.
23 Let their eyes be darkened, that they see not; and make their loins continually to totter.
Macho yao na yatiwe giza ili kwamba wasiweze kuona; uvifanye viuno vyao kutetemeka daima.
24 Pour out Thine indignation upon them, and let the fierceness of Thine anger overtake them.
Wamwagie gadhabu yako, ukali wa hasira yako uwafikie wao.
25 Let their encampment be desolate; let none dwell in their tents.
Sehemu yao na iwe ukiwa; mtu yeyote asiishi katika hema yao.
26 For they persecute him whom Thou hast smitten; and they tell of the pain of those whom Thou hast wounded.
Kwa kuwa walimtesa yule uliyempa adhabu. Mara kwa mara walihesabu maumivu ya wale walioumizwa.
27 Add iniquity unto their iniquity; and let them not come into Thy righteousness.
Wakiwashtaki kuwa wamefanya uovu juu ya uovu; usiwaache waje kwenye ushindi wa haki yako.
28 Let them be blotted out of the book of the living, and not be written with the righteous.
Uwafute kwenye Kitabu cha Uzima na wasiandikwe pamoja na wenyehaki.
29 But I am afflicted and in pain; let Thy salvation, O God, set me up on high.
Lakini mimi ni maskini na mwenye huzuni; uruhusu wokovu wako, Mungu, uniweke juu sana.
30 I will praise the name of God with a song, and will magnify Him with thanksgiving.
Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo na nitamtukuza yeye kwa shukrani.
31 And it shall please the LORD better than a bullock that hath horns and hoofs.
Nitamsifu Yahwe zaidi kuliko ng'ombe au ndama aliye na mapembe na kwato.
32 The humble shall see it, and be glad; ye that seek after God, let your heart revive.
Wanyenyekevu wameona na kufurahi; ninyi mnao matafuta Mungu, mioyo yenu itiwe nguvu.
33 For the LORD hearkeneth unto the needy, and despiseth not His prisoners.
Maana Yahwe husikia wenye uhitaji naye hawadharau wafungwa wake.
34 Let heaven and earth praise Him, the seas, and every thing that moveth therein.
Mbingu na nchi zimsifu yeye, bahari na vyote vitembeavyo majini.
35 For God will save Zion, and build the cities of Judah; and they shall abide there, and have it in possession.
Kwa maana Mungu ataiokoa Sayuni na ataujenga tena mji wa Yuda; watu wataishi huko na kupata umiliki wao.
36 The seed also of His servants shall inherit it; and they that love His name shall dwell therein.
Ukoo wa watumishi wake watairithi; nao walipendao jina lake wataishi humo.

< Psalms 69 >