< Psalms 2 >

1 Why are the nations in an uproar? And why do the peoples mutter in vain?
Kwa nini mataifa wanafanya dhoruba, kwa nini watu wanafanya njama ambazo zitafeli?
2 The kings of the earth stand up, and the rulers take counsel together, against the LORD, and against His anointed:
Wafalme wa nchi kwa pamoja hushikilia misimamo yao na watawala kwa pamoja hufanya njama kinyume na Yahwe na kinyume na Masihi, wakisema,
3 'Let us break their bands asunder, and cast away their cords from us.'
“Ngoja tuzikate pingu walizo tufingia sisi na kuzitupa pingu zao.”
4 He that sitteth in heaven laugheth, the Lord hath them in derision.
Yeye aketie katika mbingu atacheka kwa dharau mbele yao; Bwana atawadhihaki wao.
5 Then will He speak unto them in His wrath, and affright them in His sore displeasure:
Kisha ataongea nao katika hasira yake na kuwaogofya kwa gadhabu yake, akisema,
6 'Truly it is I that have established My king upon Zion, My holy mountain.'
“Mimi mwenyewe nilimpaka mafuta mfalme wa Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
7 I will tell of the decree: the LORD said unto me: 'Thou art My son, this day have I begotten thee.
Nami nitatangaza amri ya Yahwe. Yeye aliniambia, “wewe ni mwanangu! Leo hii nimekuwa baba yako.
8 Ask of Me, and I will give the nations for thine inheritance, and the ends of the earth for thy possession.
Uniombe, nami nitakupa wewe taifa kwa ajili ya urithi na mikoa ya nchi iliyo bora kwa ajili ya umiliki wako.
9 Thou shalt break them with a rod of iron; thou shalt dash them in pieces like a potter's vessel.'
Wewe utawavunja wao kwa fimbo ya chuma; kama vile mtungi wa mfinyanzi, wewe utawavunja wao vipande vipande.”
10 Now therefore, O ye kings, be wise; be admonished, ye judges of the earth.
Hivyo sasa, ninyi wafalme; mchukue tahadhari; mjirekebishe.
11 Serve the LORD with fear, and rejoice with trembling.
Mwabuduni Yahwe kwa hofu na mfurahi mkitetemeka.
12 Do homage in purity, lest He be angry, and ye perish in the way, when suddenly His wrath is kindled. Happy are all they that take refuge in Him.
Mumbusu mwana vinginevyo atawakasirikia, na mtakufa pale pale hasira yake ikiwaka. Ni jinsi gani wamebarikiwa wale wote watafutao usalama ndani yake.

< Psalms 2 >