< Psalms 1 >

1 BOOK I HAPPY IS the man that hath not walked in the counsel of the wicked, nor stood in the way of sinners, nor sat in the seat of the scornful.
Amebarikiwa mtu yule asiye enenda katika ushauri wa waovu, au kusimama katika njia ya wenye dhambi, au kukaa katika kusanyiko la wenye mizaha.
2 But his delight is in the law of the LORD; and in His law doth he meditate day and night.
Bali yeye huifurahia sheria ya Yahwe, na huitafakari sheria yake mchana na usiku.
3 And he shall be like a tree planted by streams of water, that bringeth forth its fruit in its season, and whose leaf doth not wither; and in whatsoever he doeth he shall prosper.
Atakuwa kama mti uliopandwa karibu na mkondo wa maji ambao huzaa matunda yake kwa majira yake, ambao majani yake hayakauki; lolote afanyalo litafanikiwa.
4 Not so the wicked; but they are like the chaff which the wind driveth away.
Waovu hawako hivyo, wao badala yake ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
5 Therefore the wicked shall not stand in the judgment, nor sinners in the congregation of the righteous.
Kwa hivyo waovu hawatasimama katika hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
6 For the LORD regardeth the way of the righteous; but the way of the wicked shall perish.
Kwa kuwa Yahweh huikubali njia ya wenye haki, njia ya waovu itaangamizwa.

< Psalms 1 >