< Genesis 11 >

1 And the whole earth was of one language and of one speech.
Wakati huo dunia yote ilikuwa na lugha moja na msemo mmoja.
2 And it came to pass, as they journeyed east, that they found a plain in the land of Shinar; and they dwelt there.
Watu walipoelekea upande wa mashariki, wakafika kwenye tambarare katika nchi ya Shinari nao wakaishi huko.
3 And they said one to another: 'Come, let us make brick, and burn them thoroughly.' And they had brick for stone, and slime had they for mortar.
Wakasemezana wao kwa wao, “Njooni, tufyatue matofali na tuyachome vizuri kwa moto.” Walitumia matofali badala ya mawe, na lami kwa ajili ya kushikamanishia hayo matofali.
4 And they said: 'Come, let us build us a city, and a tower, with its top in heaven, and let us make us a name; lest we be scattered abroad upon the face of the whole earth.'
Ndipo wakasema, “Njooni, tujijengee mji wenye mnara ambao utafika hadi mbinguni, ili tujipatie jina tusije tukatawanyika usoni pa dunia yote.”
5 And the LORD came down to see the city and the tower, which the children of men builded.
Lakini Bwana akashuka ili auone mji na mnara ambao wanadamu waliokuwa wanaujenga.
6 And the LORD said: 'Behold, they are one people, and they have all one language; and this is what they begin to do; and now nothing will be withholden from them, which they purpose to do.
Bwana akasema, “Ikiwa kama taifa moja wanaozungumza lugha moja wameanza kufanya hili, basi hakuna lolote watakalopanga kufanya ambalo halitawezekana kwao.
7 Come, let us go down, and there confound their language, that they may not understand one another's speech.'
Njooni, tushuke tuvuruge lugha yao ili wasielewane wao kwa wao.”
8 So the LORD scattered them abroad from thence upon the face of all the earth; and they left off to build the city.
Hivyo Bwana akawatawanya kutoka mahali pale kwenda katika dunia yote, nao wakaacha kuujenga huo mji.
9 Therefore was the name of it called Babel; because the LORD did there confound the language of all the earth; and from thence did the LORD scatter them abroad upon the face of all the earth.
Ndiyo maana pakaitwa Babeli, kwa sababu hapo ndipo Bwana alipoivuruga lugha ya dunia nzima. Kutoka hapo Bwana akawatawanya katika uso wa dunia yote.
10 These are the generations of Shem. Shem was a hundred years old, and begot Arpachshad two years after the flood.
Hivi ndivyo vizazi vya Shemu. Miaka miwili baada ya gharika, Shemu alipokuwa na miaka 100, akamzaa Arfaksadi.
11 And Shem lived after he begot Arpachshad five hundred years, and begot sons and daughters.
Baada ya kumzaa Arfaksadi, Shemu aliishi miaka 500, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
12 And Arpachshad lived five and thirty years, and begot Shelah.
Wakati Arfaksadi alipokuwa na miaka thelathini na mitano, akamzaa Shela.
13 And Arpachshad lived after he begot Shelah four hundred and three years, and begot sons and daughters.
Baada ya Arfaksadi kumzaa Shela, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
14 And Shelah lived thirty years, and begot Eber.
Shela alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Eberi.
15 And Shelah lived after he begot Eber four hundred and three years, and begot sons and daughters.
Shela baada ya kumzaa Eberi, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
16 And Eber lived four and thirty years, and begot Peleg.
Eberi alipokuwa na miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.
17 And Eber lived after he begot Peleg four hundred and thirty years, and begot sons and daughters.
Baada ya Eberi kumzaa Pelegi, aliishi miaka 430, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
18 And Peleg lived thirty years, and begot Reu.
Pelegi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Reu.
19 And Peleg lived after he begot Reu two hundred and nine years, and begot sons and daughters.
Baada ya Pelegi kumzaa Reu, aliishi miaka 209, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
20 And Reu lived two and thirty years, and begot Serug.
Reu alipokuwa na miaka thelathini na miwili, akamzaa Serugi.
21 And Reu lived after he begot Serug two hundred and seven years, and begot sons and daughters.
Baada ya Reu kumzaa Serugi, aliishi miaka 207, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
22 And Serug lived thirty years, and begot Nahor.
Serugi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Nahori.
23 And Serug lived after he begot Nahor two hundred years, and begot sons and daughters.
Baada ya Serugi kumzaa Nahori, aliishi miaka 200, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
24 And Nahor lived nine and twenty years, and begot Terah.
Nahori alipokuwa na miaka ishirini na tisa, akamzaa Tera.
25 And Nahor lived after he begot Terah a hundred and nineteen years, and begot sons and daughters.
Baada ya Nahori kumzaa Tera, aliishi miaka 119, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
26 And Terah lived seventy years, and begot Abram, Nahor, and Haran.
Tera alipokuwa na miaka sabini, akamzaa Abramu, Nahori na Harani.
27 Now these are the generations of Terah. Terah begot Abram, Nahor, and Haran; and Haran begot Lot.
Hawa ndio wazao wa Tera. Tera aliwazaa Abramu, Nahori na Harani. Harani akamzaa Loti.
28 And Haran died in the presence of his father Terah in the land of his nativity, in Ur of the Chaldees.
Tera alipokuwa bado hai, Harani akafa huko Uru ya Wakaldayo, nchi alimozaliwa.
29 And Abram and Nahor took them wives: the name of Abram's wife was Sarai; and the name of Nahor's wife, Milcah, the daughter of Haran, the father of Milcah, and the father of Iscah.
Abramu na Nahori walioa. Mke wa Abramu aliitwa Sarai, na mke wa Nahori aliitwa Milka; Milka na Iska walikuwa watoto wa Harani.
30 And Sarai was barren; she had no child.
Sarai alikuwa tasa, hakuwa na watoto.
31 And Terah took Abram his son, and Lot the son of Haran, his son's son, and Sarai his daughter-in-law, his son Abram's wife; and they went forth with them from Ur of the Chaldees, to go into the land of Canaan; and they came unto Haran, and dwelt there.
Tera akamchukua Abramu mwanawe, Loti mwana wa Harani mwanawe, na Sarai mkwewe, mke wa Abramu mwanawe, wakatoka kwa pamoja katika Uru ya Wakaldayo kwenda nchi ya Kanaani. Lakini walipofika Harani, wakaishi huko.
32 And the days of Terah were two hundred and five years; and Terah died in Haran.
Tera alikufa huko Harani akiwa na miaka 205.

< Genesis 11 >