< Genesis 10 >

1 Now these are the generations of the sons of Noah: Shem, Ham, and Japheth; and unto them were sons born after the flood.
Hawa ndio wazao wa Noa: Shemu, Hamu na Yafethi, ambao walizaa wana baada ya gharika.
2 The sons of Japheth: Gomer, and Magog, and Madai, and Javan, and Tubal, and Meshech, and Tiras.
Wana wa Yafethi walikuwa: Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Mesheki na Tirasi.
3 And the sons of Gomer: Ashkenaz, and Riphath, and Togarmah.
Wana wa Gomeri walikuwa: Ashkenazi, Rifathi na Togarma.
4 And the sons of Javan: Elishah, and Tarshish, Kittim, and Dodanim.
Wana wa Yavani walikuwa: Elisha, Tarshishi, Kitimu na Rodanimu.
5 Of these were the isles of the nations divided in their lands, every one after his tongue, after their families, in their nations.
(Kutokana na hawa mataifa ya Pwani yalienea katika nchi zao, kwa koo zao katika mataifa yao, kila moja kwa lugha yake.)
6 And the sons of Ham: Cush, and Mizraim, and Put, and Canaan.
Wana wa Hamu walikuwa: Kushi, Misraimu, Putu na Kanaani.
7 And the sons of Cush: Seba, and Havilah, and Sabtah, and Raamah, and Sabteca; and the sons of Raamah: Sheba, and Dedan.
Wana wa Kushi walikuwa: Seba, Havila, Sabta, Raama na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa: Sheba na Dedani.
8 And Cush begot Nimrod; he began to be a mighty one in the earth.
Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikua akawa mtu shujaa duniani.
9 He was a mighty hunter before the LORD; wherefore it is said: 'Like Nimrod a mighty hunter before the LORD.'
Alikuwa mwindaji hodari mbele za Bwana. Ndiyo sababu watu husema, “Kama Nimrodi, hodari wa kuwinda mbele za Bwana.”
10 And the beginning of his kingdom was Babel, and Erech, and Accad, and Calneh, in the land of Shinar.
Vituo vyake vya kwanza katika ufalme wake vilikuwa Babeli, Ereki, Akadi na Kalne katika Shinari.
11 Out of that land went forth Asshur, and builded Nineveh, and Rehoboth-ir, and Calah,
Kutoka nchi ile alikwenda Ashuru, ambako alijenga Ninawi, Rehoboth-iri, Kala,
12 and Resen between Nineveh and Calah — the same is the great city.
na Reseni, iliyo kati ya Ninawi na Kala; huo ndio mji mkubwa.
13 And Mizraim begot Ludim, and Anamim, and Lehabim, and Naphtuhim,
Misraimu alikuwa baba wa: Waludi, Waanami, Walehabi, Wanaftuhi,
14 and Pathrusim, and Casluhim — whence went forth the Philistines — and Caphtorim.
Wapathrusi, Wakasluhi (hao ndio asili ya Wafilisti), na Wakaftori.
15 And Canaan begot Zidon his firstborn, and Heth;
Kanaani alikuwa baba wa: Sidoni mzaliwa wake wa kwanza, Hethi,
16 and the Jebusite, and the Amorite, and the Girgashite;
Wayebusi, Waamori, Wagirgashi,
17 and the Hivite, and the Arkite, and the Sinite;
Wahivi, Waariki, Wasini,
18 and the Arvadite, and the Zemarite, and the Hamathite; and afterward were the families of the Canaanite spread abroad.
Waarvadi, Wasemari na Wahamathi. Baadaye koo za Wakanaani zilitawanyika,
19 And the border of the Canaanite was from Zidon, as thou goest toward Gerar, unto Gaza; as thou goest toward Sodom and Gomorrah and Admah and Zeboiim, unto Lasha.
na mipaka ya Kanaani ilienea kutoka Sidoni kuelekea Gerari hadi Gaza, kisha kuelekea Sodoma, Gomora, Adma na Seboimu, hadi kufikia Lasha.
20 These are the sons of Ham, after their families, after their tongues, in their lands, in their nations.
Hawa ni wana wa Hamu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
21 And unto Shem, the father of all the children of Eber, the elder brother of Japheth, to him also were children born.
Shemu ambaye ni ndugu mkubwa wa Yafethi, kwake kulizaliwa wana pia. Shemu alikuwa baba wa wana wote wa Eberi.
22 The sons of Shem: Elam, and Asshur, and Arpachshad, and Lud, and Aram.
Wana wa Shemu walikuwa: Elamu, Ashuru, Arfaksadi, Ludi na Aramu.
23 And the sons of Aram: Uz, and Hul, and Gether, and Mash.
Wana wa Aramu walikuwa: Usi, Huli, Getheri na Mesheki.
24 And Arpachshad begot Shelah; and Shelah begot Eber.
Arfaksadi alikuwa baba wa Shela, naye Shela akamzaa Eberi.
25 And unto Eber were born two sons; the name of the one was Peleg; for in his days was the earth divided; and his brother's name was Joktan.
Eberi akapata wana wawili: Mmoja wao aliitwa Pelegi, kwa kuwa wakati wake ndipo dunia iligawanyika; nduguye aliitwa Yoktani.
26 And Joktan begot Almodad, and Sheleph, and Hazarmaveth, and Jerah;
Yoktani alikuwa baba wa: Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
27 and Hadoram, and Uzal, and Diklah;
Hadoramu, Uzali, Dikla,
28 and Obal, and Abimael, and Sheba;
Obali, Abimaeli, Sheba,
29 and Ophir, and Havilah, and Jobab; all these were the sons of Joktan.
Ofiri, Havila na Yobabu. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
30 And their dwelling was from Mesha, as thou goest toward Sephar, unto the mountain of the east.
Nchi waliyoishi ilienea toka Mesha kuelekea Sefari kwenye nchi ya vilima iliyoko mashariki.
31 These are the sons of Shem, after their families, after their tongues, in their lands, after their nations.
Hao ndio wana wa Shemu kwa koo zao na lugha zao, katika nchi zao na mataifa yao.
32 These are the families of the sons of Noah, after their generations, in their nations; and of these were the nations divided in the earth after the flood.
Hizi ndizo koo za wana wa Noa, kufuatana na vizazi vyao, katika mataifa yao. Kutokana na hawa mataifa yalienea duniani kote baada ya gharika.

< Genesis 10 >