< Romans 8 >

1 There is therefore now no condemnation to those who are in Christ Jesus.
Kwa hiyo, sasa hakuna hukumu kwa wale ambao katika maisha yao wameungana na Kristo.
2 For the law of the Spirit of life has made thee free from the law of sin and of death.
Maana, sheria ya Roho iletayo uzima kwa kuungana na Kristo Yesu imenikomboa kutoka katika sheria ya dhambi na kifo.
3 For there was an impotency of the law, in which it was weak through depravity, God having sent his own Son in the likeness of the sin of depravity and for sin, condemned sin in depravity:
Mungu ametekeleza jambo lile ambalo Sheria haikuweza kutekeleza kwa sababu ya udhaifu w binadamu. Mungu alimtuma Mwanae akiwa mwenye mwili sawa na miili yetu sisi wenye dhambi, ili aikabili dhambi, na kwa mwili huo akaiangamiza dhambi.
4 in order that the righteousness of the law may be fulfilled in us, who walk not according to depravity, but according to the spirit.
Mungu alifanya hivyo kusudi matakwa ya haki ya Sheria yatekelezwe kikamilifu ndani yetu sisi ambao tunaishi, si kwa nguvu za kibinadamu, bali kwa nguvu ya Roho.
5 For those being in harmony with depravity, do mind the things of depravity, and those in harmony with the Spirit, the things of the Spirit:
Maana, wale wanaoishi kufuatana na matakwa ya mwili, hutawaliwa na fikira za mwili. Lakini wale wanaoishi kufuatana na matakwa ya Roho Mtakatifu, hutawaliwa na fikira za Roho.
6 for the mind of depravity is death: and the mind of the Spirit is life and peace.
Fikira za mwili huleta kifo; fikira za Roho huleta uzima na amani.
7 Therefore the mind of depravity is enmity toward God: for it is not subordinated to the law of God, for it is not able so to be.
Maana, mwenye kutawaliwa na fikira za mwili ni adui wa Mungu; haitii sheria ya Mungu, wala hawezi kuitii.
8 But those being in depravity are not able to please God.
Watu wanaotii matakwa ya mwili hawawezi kumpendeza Mungu.
9 But ye are not in depravity, but in the Spirit, if indeed the Spirit of God dwells in you. But if any one has not the Spirit of Christ, he is none of His.
Lakini ninyi hamuishi kufuatana na matakwa ya mwili, bali kufuatana na matakwa ya Roho, ikiwa Roho wa Mungu anaishi ndani yenu. Yeyote asiye na Roho wa Kristo, huyo si wake Kristo.
10 But if Christ is in you, the body is dead so far as sin is concerned; but the Spirit is life so far as righteousness is concerned.
Lakini kama Kristo yumo ndani yenu, ingawa miili yenu itakufa kwa sababu ya dhambi, kwenu Roho ndiye uhai kwa sababu mmekubaliwa kuwa waadilifu.
11 But if the Spirit of Him who raised up Jesus from the dead dwells in you, the one having raised Christ Jesus from the dead will also create life in your mortal bodies through His Spirit, who dwells in you.
Ikiwa Roho wa Mungu aliyemfufua Kristo kutoka wafu anaishi ndani yenu, basi huyo aliyemfufua Kristo kutoka wafu ataipa uzima miili yenu yenye hali ya kufa; atafanya hivyo kwa njia ya Roho wake akaaye ndani yenu.
12 Then therefore, brethren, we are debtors, not to depravity, to live according to depravity.
Hivyo basi, ndugu zangu, tunalo jukumu, lakini si la kuishi kufuatana na maumbile ya kibinadamu.
13 For if you live according to depravity, you are about to die: but if through the Spirit you kill the practices of the body, you shall live.
Kwa maana, kama mkiishi kufuatana na matakwa ya maumbile ya kibinadamu, hakika mtakufa. Lakini, kama kwa njia ya Roho mnayaua matendo yenu maovu, basi, mtaishi.
14 For so many as are led by the Spirit of God, these are the sons of God.
Wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu ni watoto wa Mungu.
15 For you did not receive the spirit of bondage again unto fear; but you received the Spirit of adoption, in which we cry; Father, Father.
Kwa maana, Roho mliyempokea si Roho mwenye kuwafanya ninyi watumwa na kuwatia tena hofu; sivyo, bali mmempokea Roho mwenye kuwafanya ninyi watoto wa Mungu, na kwa nguvu ya huyo Roho, sisi tunaweza kumwita Mungu, “Aba,” yaani “Baba!”
16 The Spirit Himself witnesses along with our spirit, that we are the children of God.
Naye Roho mwenyewe anajiunga na roho zetu na kuthibitisha kwamba sisi ni watoto wa Mungu.
17 And if children, indeed heirs; truly heirs of God, and joint heirs with Christ; if we suffer together, in order that we may also be glorified together.
Basi, kwa vile sisi ni watoto wa Mungu, tutapokea baraka zote Mungu alizowawekea watu wake, na tutashiriki urithi huo pamoja na Kristo; maana, tukiyashiriki mateso yake Kristo, tutaushiriki pia utukufu wake.
18 For I reckon that the sufferings of these present times are not worthy to be compared to the glory which is about to be revealed in us.
Naona kuwa mateso ya wakati huu wa sasa si kitu kamwe kama tukiyafananisha na ule utukufu utakaodhihirishwa kwetu.
19 For the earnest expectation of the creature awaits the revelation of the sons of God.
Viumbe vyote vinatazamia kwa hamu Mungu awadhihirishe watoto wake.
20 For the creature has been subordinated to mortality, not willingly, but through Him who subordinated it;
Kwa maana, viumbe viliwekwa katika hali ya kutojiweza kabisa, si kwa hiari yao, ila vilifanywa hivyo kwa mapenzi ya Mungu. Hata hivyo yapo matumaini,
21 therefore indeed pursuant to hope, the creature itself shall be delivered from the bondage of corruption into the liberty of the glory of the children of God.
maana hivyo viumbe navyo vitaokolewa kutoka katika utumwa wa uharibifu, vishiriki uhuru mtukufu wa watoto wa Mungu.
22 For we know that all creation groans together and travails together until now;
Kwa maana tunajua kwamba mpaka hivi sasa, viumbe vyote vinalia kwa maumivu kama ya kujifungua mtoto.
23 and not only so, but we ourselves, having the earnest of the Spirit, and we ourselves groan within ourselves, waiting for the adoption of sons, the redemption of our body.
Wala si hivyo viumbe peke yake, bali hata sisi tulio na huyo Roho, aliye wa kwanza wa zawadi za Mungu; sisi pia tunalalamika ndani yetu, tukitazamia kufanywa watoto wa Mungu, nazo nafsi zenu zikombolewe.
24 For we are saved by hope: but hope which is seen is not hope: for why does any one indeed hope for that which he sees?
Maana kwa matumaini hayo sisi tumekombolewa; lakini tumaini halina maana ikiwa tunakiona kile tunachotumainia. Maana ni nani anayetumaini kile ambacho tayari anakiona?
25 But if we hope for that which we do not see, we wait for it with patience.
Kama tunakitumaini kile ambacho hatujakiona bado, basi, tunakingojea kwa uvumilivu.
26 And likewise the Spirit also helps our infirmity. For we know not what we should pray for as it behooves us: but the Spirit himself makes intercession with unutterable groanings:
Hali kadhalika, naye Roho anatusaidia katika udhaifu wetu. Maana hatujui inavyotupasa kuomba; lakini Roho mwenyewe anatuombea kwa Mungu kwa mlio wa huzuni usioelezeka.
27 but he that searches the hearts knows what is the mind of the Spirit, because he makes intercession towards God in behalf of the saints.
Naye Mungu aonaye mpaka ndani ya mioyo ya watu, anajua fikira ya huyo Roho; kwani huyo Roho huwaombea watu wa Mungu kufuatana na mapenzi ya Mungu.
28 But we know that all things work together for good to them that love God, to them that are called according to his purpose.
Tunajua kwamba, katika mambo yote, Mungu hufanya kazi na kuifanikisha pamoja na wote wampendao, yaani wale aliowaita kufuatana na kusudi lake.
29 Because whom he did foreknow, he did also predestinate to be conformed to the image of his Son, in order that he might be the firstborn among many brethren:
Maana hao aliowachagua tangu mwanzo, ndio aliowateua wapate kufanana na Mwanae, ili Mwana awe wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi.
30 and whom He did foreknow, them he also called: and whom he called, them he also justified: and whom he justified, them He also glorified.
Basi, Mungu aliwaita wale aliokuwa amewateua; na hao aliowaita aliwakubali kuwa waadilifu; na hao aliowakubali kuwa waadilifu aliwashirikisha pia utukufu wake.
31 Then what shall we say to these things? If God is for us, who can be against us?
Kutokana na hayo, tuseme nini zaidi? Ikiwa Mungu yuko upande wetu, nani awezaye kutupinga?
32 Indeed he who spared not his own Son, but delivered Him up for us all, how will He not with him, freely give us all things?
Mungu hakumhurumia hata mwanae wa pekee, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote. Ikiwa amefanya hivyo, je, hatatujalia pia mema yote?
33 Who will lay anything to the charge of God's elect?
Ni nani atakayewashtaki wateule wa Mungu? Mungu mwenyewe huwaondolea hatia!
34 It is God who justifies: who is he that condemns? It is Christ who died, and rather who is risen, who is on the right hand of God, who indeed is interceding in our behalf.
Ni nani atakayewahukumu? Hakuna! Maana Kristo ndiye aliyekufa, tena alifufuka kutoka wafu na anakaa upande wa kulia wa Mungu. Yeye anatuombea!
35 Who shall separate us from the love of Christ? shall tribulation, or anguish, or persecution, or famine, or nakedness, or peril, or sword?
Ni nani awezaye kututenga na mapendo ya Kristo? Je, ni taabu, au dhiki, au mateso, au njaa, au ukosefu wa nguo, au hatari, au kuuawa?
36 As has been written, that We are killed all day for thy sake; we are counted as sheep of the slaughter.
Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: “Kwa ajili yako, twakikabili kifo kutwa kucha: tunatendewa kama kondoo wa kuchinjwa.”
37 But in all these we are more than conquerors through him that loved us.
Lakini, katika mambo haya yote, tumepata ushindi mkubwa kwa msaada wake yeye aliyetupenda.
38 For I am persuaded that, neither death, nor life, nor angels, nor principalities, nor things present, nor things to come,
Maana ninajua hakika kwamba hakuna kitu kiwezacho kututenganisha na upendo wake: wala kifo, wala uhai; wala malaika, au nguvu nyingine za mbinguni; wala yanayotokea sasa, wala yatakayotokea baadaye; wala mamlaka;
39 nor powers, nor height, nor depth, nor any other creature, shall be able to separate us from the love of God, which is in Christ Jesus our Lord.
Wala ulimwengu wa juu, wala wa chini kabisa. Hakuna kiumbe chochote kitakachoweza kututenga na upendo wa Mungu kwetu kwa njia ya Kristo Yesu Bwana wetu.

< Romans 8 >