< Acts 1 >

1 Truly, I made the first history, O Theophilus, concerning all things which Jesus began both to do and to teach,
Ndugu Theofilo, Katika kitabu cha kwanza niliandika juu ya mambo yote Yesu aliyotenda na kufundisha tangu mwanzo wa kazi yake
2 from the day on which, having given commandment through the Holy Ghost to the apostles whom He had chosen, He was received up.
mpaka siku ile alipochukuliwa mbinguni. Kabla ya kuchukuliwa mbinguni aliwapa maagizo kwa njia ya Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua.
3 To whom He also, after He suffered, manifested Himself alive in many testimonials, being seen by them forty days, and speaking the things concerning the kingdom of God:
Kwa muda wa siku arobaini baada ya kifo chake aliwatokea mara nyingi kwa namna ambazo zilithibitisha kabisa kwamba alikuwa hai. Walimwona, naye aliongea nao juu ya ufalme wa Mungu.
4 and being assembled together with them, He commanded them, Not to depart from Jerusalem, but to await the promise of the Father which ye heard from me;
Wakati walipokutana pamoja aliwaamuru hivi: “Msiondoke Yerusalemu, bali ngojeeni ile zawadi aliyoahidi Baba, zawadi ambayo mlikwisha nisikia nikiongea juu yake.
5 that John indeed baptized with water, but you shall be baptized with the Holy Ghost not many days hence.
Kwani Yohane alibatiza kwa maji, lakini baada ya siku chache, ninyi mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu.”
6 Therefore indeed having assembled, they asked Him saying, Lord, do you at this time restore the kingdom to Israel?
Basi, mitume walipokutana pamoja na Yesu, walimwuliza, “Je Bwana, wakati huu ndipo utakaporudisha ule ufalme kwa Israeli?”
7 He said to them; It is not your province, to know the times or seasons, which the Father placed in His own authority.
Lakini Yesu akawaambia, “Nyakati na majira ya mambo hayo viko chini ya mamlaka ya Baba yangu, wala si shauri lenu kujua yatakuwa lini.
8 But you shall receive the power of the Holy Ghost having come upon you, and shall be my witnesses both in Jerusalem, and all Judea, and in Samaria, and into the extremity of the earth.
Lakini wakati Roho Mtakatifu atakapowashukieni ninyi, mtajazwa nguvu na mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, katika nchi yote ya Yudea na Samaria, na hata miisho ya dunia.”
9 And having spoken these words, they looking, He was taken up, and a cloud received Him from their eyes.
Baada ya kusema hayo, wote wakiwa wanamtazama, alichukuliwa mbinguni; wingu likamficha wasimwone tena.
10 And while they were gazing up into the heaven, He going, and behold, two men stood by them in white garments, who also said,
Walipokuwa bado wanatazama juu angani, akiwa anakwenda zake, mara watu wawili waliokuwa wamevaa nguo nyeupe walisimama karibu nao,
11 Ye Galilean men, why stand you looking up into the heaven? this same Jesus, the One having been received up into the heaven, will so come in the manner in which you saw Him going up into the heaven.
wakasema, “Enyi wananchi wa Galilaya! Mbona mnasimama mkitazama angani? Yesu huyu ambaye amechukuliwa kutoka kwenu kwenda mbinguni atakuja tena namna hiyohiyo mliivyomwona akienda mbinguni.”
12 Then they returned into Jerusalem from the mount called Olivet, which is near Jerusalem, being a journey of a Sabbath day.
Kisha mitume wakarudi Yerusalemu kutoka mlima wa Mizeituni ulioko karibu kilomita moja kutoka mjini.
13 And when they came in, they went up into the upper room, where Peter and John and James and Andrew, Philip and Thomas, Bartholomew and Matthew, James the son of Alpheus, and Simon Zelotes, and Judas the brother of James, were abiding.
Walipofika mjini waliingia katika chumba ghorofani ambamo walikuwa wanakaa; nao walikuwa Petro, Yohane, Yakobo, Andrea, Filipo na Thoma, Bartholomayo na Mathayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni Zelote na Yuda mwana wa Yakobo.
14 They were all persevering of one accord in prayer along with the women, and Mary, the mother of Jesus, and His brothers.
Hawa wote walikusanyika pamoja kusali, pamoja na wanawake kadha wa kadha, na Maria mama yake Yesu, na ndugu zake.
15 And during those days, Peter standing up in the midst of the brethren, said (and the number of names were about one hundred and twenty),
Siku chache baadaye, kulikuwa na mkutano wa waumini, karibu watu mia moja na ishirini. Petro alisimama mbele yao,
16 Men, brethren, it behooved the scripture which the Holy Ghost predicted through the mouth of David concerning Judas, the one becoming leader to those arresting Jesus, to be fulfilled;
akasema, “Ndugu zangu, ilikuwa lazima ile sehemu ya Maandiko Matakatifu itimie, sehemu ambayo Roho Mtakatifu, kwa maneno ya Daudi, alibashiri habari za Yuda ambaye aliwaongoza wale waliomtia Yesu nguvuni.
17 because he was numbered among us and received the lot of this ministry.
Yuda alikuwa mmoja wa kikundi chetu maana alichaguliwa ashiriki huduma yetu.
18 Then indeed he purchased a field by the reward of iniquity, and falling headlong, burst asunder in the middle, and all his bowels burst out;
(“Mnajua kwamba yeye alinunua shamba kwa zile fedha alizopata kutokana na kitendo chake kiovu. Akaanguka chini, akapasuka na matumbo yake yakamwagika nje.
19 which indeed was known to all those dwelling at Jerusalem, so that field, in their own dialect, is called Acheldamach; that is, field of blood.
Kila mtu katika Yerusalemu alisikia habari za tukio hilo na hivyo, kwa lugha yao, wakaliita lile shamba Hekeli Dama, maana yake, Shamba la Damu.)
20 For it has been written in the book of Psalms, Let his habitation be desolate, and let there be no one dwelling in it, and let another take his pastorate.
Basi, imeandikwa katika kitabu cha Zaburi: Nyumba yake ibaki mahame; mtu yeyote asiishi ndani yake. Tena imeandikwa: Mtu mwingine achukue nafasi yake katika huduma hiyo.
21 Therefore the men having come together with us all the time in which the Lord Jesus came in unto us and went out,
Kwa hiyo, ni lazima mtu mwingine ajiunge nasi kama shahidi wa ufufuo wake Bwana Yesu.
22 beginning from the baptism of John, until the day on which He was taken up from us, it behooveth one of these to be witness of His resurrection along with us.
Anapaswa kuwa mmoja wa wale waliokuwa katika kundi letu wakati wote Bwana alipokuwa anasafiri pamoja nasi, tangu wakati Yohane alipokuwa anabatiza mpaka siku ile Yesu alipochukuliwa kutoka kwetu kwenda mbinguni.”
23 And they nominated two, Joseph, called Barsabas who was called Justus, and Matthias.
Basi, wakataja majina ya watu wawili; wa kwanza Yosefu aliyeitwa Barsaba (au pia Yusto), na wa pili Mathia.
24 And praying they said, Thou, O Lord, Heart-searcher of all, show up the one of these two, whom thou hast chosen
Kisha wakasali: “Bwana, wewe unajua mioyo ya watu wote. Hivyo, utuonyeshe ni yupi kati ya hawa wawili uliyemchagua
25 to receive the place of this ministry and apostleship from which Judas departed to go into his own place.
ili achukue nafasi hii ya huduma ya kitume aliyoacha Yuda akaenda mahali pake mwenyewe.”
26 And they gave lots for them, and the lot fell upon Matthias; and he was numbered with the eleven apostles.
Hapo, wakapiga kura; kura ikampata Mathia, naye akaongezwa katika idadi ya wale mitume wengine kumi na mmoja.

< Acts 1 >