< Psalms 125 >
1 They that trust in the Lord shall be as mount Sion: he shall not be moved for ever that dwelleth
Wimbo wa kwenda juu. Wale wamtumainio Bwana ni kama mlima Sayuni, ambao hauwezi kutikisika, bali wadumu milele.
2 In Jerusalem. Mountains are round about it: so the Lord is round about his people from henceforth now and for ever.
Kama milima inavyozunguka Yerusalemu, ndivyo Bwana anavyowazunguka watu wake sasa na hata milele.
3 For the Lord will not leave the rod of sinners upon the lot of the just: that the just may not stretch forth their hands to iniquity.
Fimbo ya waovu haitadumu juu ya nchi waliopewa wenye haki, ili wenye haki wasije wakatumia mikono yao kutenda ubaya.
4 Do good, O Lord, to those that are good, and to the upright of heart.
Ee Bwana, watendee mema walio wema, wale walio wanyofu wa moyo.
5 But such as turn aside into bonds, the Lord shall lead out with the workers of iniquity: peace upon Israel.
Bali wale wanaogeukia njia zilizopotoka, Bwana atawafukuza pamoja na watenda mabaya. Amani iwe juu ya Israeli.