< Mark 10 >

1 And rising up thence he comes into the coasts of Judaea, and the other side of the Jordan. And again crowds come together to him, and, as he was accustomed, again he taught them.
Yesu akaondoka huko, akavuka Mto Yordani, akaenda sehemu za Uyahudi. Umati mkubwa wa watu ukaenda kwake tena, naye kama ilivyokuwa desturi yake, akawafundisha.
2 And Pharisees coming to [him] asked him, Is it lawful for a man to put away [his] wife? (tempting him).
Baadhi ya Mafarisayo wakaja ili kumjaribu kwa kumuuliza, “Je, ni halali mtu kumwacha mke wake?”
3 But he answering said to them, What did Moses command you?
Yesu akawajibu, “Je, Mose aliwaamuru nini?”
4 And they said, Moses allowed to write a bill of divorce, and to put away.
Wakajibu, “Mose aliruhusu kwamba mume anaweza kumwandikia mkewe hati ya talaka na kumwacha.”
5 And Jesus answering said to them, In view of your hard-heartedness he wrote this commandment for you;
Yesu akawaambia, “Mose aliwaandikia sheria hiyo kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu.
6 but from [the] beginning of [the] creation God made them male and female.
Lakini tangu mwanzo wa uumbaji, ‘Mungu aliwaumba mwanaume na mwanamke.
7 For this cause a man shall leave his father and mother and shall be united to his wife,
Kwa sababu hii mwanaume atamwacha baba yake na mama yake na kuambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja.’
8 and the two shall be one flesh: so that they are no longer two but one flesh.
Kwa hiyo hawatakuwa wawili tena, bali mwili mmoja.
9 What therefore God has joined together, let not man separate.
Basi, alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.”
10 And again in the house the disciples asked him concerning this.
Walipokuwa tena ndani ya nyumba, wanafunzi wake wakamuuliza kuhusu jambo hili.
11 And he says to them, Whosoever shall put away his wife and shall marry another, commits adultery against her.
Akawajibu, “Mtu yeyote amwachaye mkewe na kuoa mke mwingine, anazini naye.
12 And if a woman put away her husband and shall marry another, she commits adultery.
Naye mwanamke amwachaye mumewe na kuolewa na mume mwingine, anazini.”
13 And they brought little children to him that he might touch them. But the disciples rebuked those that brought [them].
Watu walikuwa wakimletea Yesu watoto wadogo ili awaguse, lakini wanafunzi wake wakawakemea.
14 But Jesus seeing [it], was indignant, and said to them, Suffer the little children to come to me; forbid them not; for of such is the kingdom of God.
Yesu alipoona yaliyokuwa yakitukia, akachukizwa. Akawaambia wanafunzi wake, “Waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wa wale walio kama hawa.
15 Verily I say to you, Whosoever shall not receive the kingdom of God as a little child, shall in no wise enter into it.
Amin, nawaambia, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hatauingia kamwe.”
16 And having taken them in his arms, having laid his hands on them, he blessed them.
Akawachukua watoto mikononi mwake, akawakumbatia, akaweka mikono yake juu yao, akawabariki.
17 And as he went forth into the way, a person ran up to [him], and kneeling to him asked him, Good Teacher, what shall I do that I may inherit eternal life? (aiōnios g166)
Yesu alipokuwa anaondoka, mtu mmoja akamkimbilia, akapiga magoti mbele yake, akamuuliza, “Mwalimu mwema, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?” (aiōnios g166)
18 But Jesus said to him, Why callest thou me good? no one is good but one, [that is] God.
Yesu akamwambia, “Mbona unaniita mwema? Hakuna yeyote aliye mwema ila Mungu peke yake.
19 Thou knowest the commandments: Do not commit adultery, Do not kill, Do not steal, Do not bear false witness, Do not defraud, Honour thy father and mother.
Unazijua amri: ‘Usiue, usizini, usiibe, usishuhudie uongo, usidanganye, waheshimu baba yako na mama yako.’”
20 And he answering said to him, Teacher, all these things have I kept from my youth.
Akamjibu, “Mwalimu, amri hizi zote nimezishika tangu nikiwa mtoto.”
21 And Jesus looking upon him loved him, and said to him, One thing lackest thou: go, sell whatever thou hast and give to the poor, and thou shalt have treasure in heaven; and come, follow me, [taking up the cross].
Yesu akamtazama na kumpenda, akamwambia, “Umepungukiwa na kitu kimoja. Nenda ukauze kila kitu ulicho nacho uwape maskini hizo fedha, nawe utakuwa na hazina mbinguni. Kisha njoo, unifuate.”
22 But he, sad at the word, went away grieved, for he had large possessions.
Yule mtu aliposikia hayo, akasikitika sana. Akaondoka kwa huzuni kwa sababu alikuwa na mali nyingi.
23 And Jesus looking around says to his disciples, How difficultly shall they that have riches enter into the kingdom of God!
Yesu akatazama pande zote, akawaambia wanafunzi wake, “Itakuwa vigumu sana kwa wenye mali kuingia katika Ufalme wa Mungu!”
24 And the disciples were amazed at his words. And Jesus again answering says to them, Children, how difficult it is that those who trust in riches should enter into the kingdom of God!
Wanafunzi wake wakashangazwa sana na maneno hayo. Lakini Yesu akawaambia tena, “Wanangu, tazama jinsi ilivyo vigumu kwa wale wanaotumainia mali kuingia katika Ufalme wa Mungu.
25 It is easier for a camel to go through the eye of a needle than for a rich man to enter into the kingdom of God.
Ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita kwenye tundu la sindano kuliko mtu tajirikuingia katika Ufalme wa Mungu.”
26 And they were exceedingly astonished, saying to one another, And who can be saved?
Wanafunzi wake wakashangaa sana. Wakaulizana wao kwa wao, “Ni nani basi awezaye kuokoka?”
27 But Jesus looking on them says, With men it is impossible, but not with God; for all things are possible with God.
Yesu akawatazama, akawaambia, “Kwa mwanadamu jambo hili haliwezekani, lakini kwa Mungu sivyo. Mambo yote yanawezekana kwa Mungu.”
28 Peter began to say to him, Behold, we have left all things and have followed thee.
Ndipo Petro akamjibu, “Tazama, tumeacha kila kitu na kukufuata wewe!”
29 Jesus answering said, Verily I say to you, There is no one who has left house, or brethren, or sisters, or father, or mother, [or wife], or children, or lands, for my sake and for the sake of the gospel,
Yesu akasema, “Amin, nawaambia, hakuna mtu yeyote aliyeacha nyumba, ndugu wa kiume au wa kike, au mama au baba, au watoto au mashamba kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili,
30 that shall not receive a hundredfold now in this time: houses, and brethren, and sisters, and mothers, and children, and lands, with persecutions, and in the coming age life eternal. (aiōn g165, aiōnios g166)
ambaye hatalipwa mara mia katika ulimwengu huu: nyumba, ndugu wa kiume na wa kike, mama na baba na watoto, mashamba pamoja na mateso, kisha uzima wa milele katika ulimwengu ujao. (aiōn g165, aiōnios g166)
31 But many first shall be last, and the last first.
Lakini wengi walio wa kwanza watakuwa wa mwisho, na wa mwisho watakuwa wa kwanza.”
32 And they were in the way going up to Jerusalem, and Jesus was going on before them; and they were amazed, and were afraid as they followed. And taking the twelve again to [him], he began to tell them what was going to happen to him:
Walikuwa njiani wakipanda kwenda Yerusalemu, na Yesu alikuwa ametangulia. Wanafunzi wake walishangaa, nao watu waliowafuata walijawa na hofu. Yesu akawachukua tena wale wanafunzi wake kumi na wawili kando na kuwaambia yatakayompata.
33 Behold, we go up to Jerusalem, and the Son of man shall be delivered up to the chief priests and to the scribes, and they shall condemn him to death, and shall deliver him up to the nations:
Akasema, “Tunapanda kwenda Yerusalemu, na Mwana wa Adamu atasalitiwa kwa viongozi wa makuhani na walimu wa sheria. Wao watamhukumu kifo na kumtia mikononi mwa watu wa Mataifa,
34 and they shall mock him, and shall scourge him, and shall spit upon him, and shall kill him; and after three days he shall rise again.
ambao watamdhihaki na kumtemea mate, watampiga na kumuua. Siku tatu baadaye atafufuka.”
35 And there come to him James and John, the sons of Zebedee, saying [to him], Teacher, we would that whatsoever we may ask thee, thou wouldst do it for us.
Kisha Yakobo na Yohana, wana wa Zebedayo, wakaja kwake na kumwambia, “Mwalimu, tunataka utufanyie lolote tutakalokuomba.”
36 And he said to them, What would ye that I should do for you?
Naye akawaambia, “Je, mwataka niwafanyie jambo gani?”
37 And they said to him, Give to us that we may sit, one on thy right hand, and one on thy left hand, in thy glory.
Wakamwambia, “Tupe kukaa mmoja upande wako wa kuume na mwingine upande wako wa kushoto katika utukufu wako.”
38 And Jesus said to them, Ye do not know what ye ask. Are ye able to drink the cup which I drink, or be baptised with the baptism that I am baptised with?
Lakini Yesu akawaambia, “Ninyi hamjui mnaloliomba. Je, mnaweza kukinywea kikombe ninyweacho mimi, au kubatizwa ubatizo nibatizwao mimi?”
39 And they said to him, We are able. And Jesus said to them, The cup that I drink ye will drink and with the baptism that I am baptised with ye will be baptised,
Wakajibu, “Tunaweza.” Kisha Yesu akawaambia, “Kikombe nikinyweacho mtakinywea na ubatizo nibatizwao mtabatizwa,
40 but to sit on my right hand or on my left is not mine to give, but for those for whom it is prepared.
lakini kuketi mkono wangu wa kuume au wa kushoto si juu yangu mimi kuwapa. Nafasi hizi ni kwa ajili ya wale walioandaliwa.”
41 And the ten having heard [of it], began to be indignant about James and John.
Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia hayo, wakaanza kuwakasirikia Yakobo na Yohana.
42 But Jesus having called them to [him], says to them, Ye know that those who are esteemed to rule over the nations exercise lordship over them; and their great men exercise authority over them;
Lakini Yesu akawaita wote pamoja na kuwaambia, “Mnafahamu kuwa wale wanaodhaniwa kuwa watawala wa watu wa Mataifa huwatawala watu kwa nguvu, nao wenye vyeo huonyesha mamlaka yao.
43 but it is not thus among you; but whosoever would be great among you, shall be your minister;
Lakini isiwe hivyo kwenu. Badala yake, yeyote anayetaka kuwa mkuu miongoni mwenu hana budi kuwa mtumishi wenu,
44 and whosoever would be first of you shall be bondman of all.
na yeyote anayetaka kuwa wa kwanza, hana budi kuwa mtumwa wa wote.
45 For also the Son of man did not come to be ministered to, but to minister, and give his life a ransom for many.
Kwa kuwa hata Mwana wa Adamu hakuja ili kutumikiwa, bali kutumika na kuutoa uhai wake uwe fidia kwa ajili ya wengi.”
46 And they come to Jericho, and as he was going out from Jericho, and his disciples and a large crowd, the son of Timaeus, Bartimaeus, the blind [man], sat by the wayside begging.
Kisha wakafika Yeriko. Yesu alipokuwa akiondoka mjini na wanafunzi wake pamoja na umati mkubwa wa watu, kipofu mmoja, jina lake Bartimayo, mwana wa Timayo, alikuwa ameketi kando ya njia akiomba msaada.
47 And having heard that it was Jesus the Nazaraean, he began to cry out and to say, O Son of David, Jesus, have mercy on me.
Aliposikia kuwa ni Yesu wa Nazareti aliyekuwa anapita, akaanza kupaza sauti akisema, “Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!”
48 And many rebuked him, that he might be silent; but he cried so much the more, Son of David, have mercy on me.
Watu wengi wakamkemea, wakamwambia akae kimya, lakini yeye akazidi kupaza sauti, akisema, “Mwana wa Daudi, nihurumie!”
49 And Jesus, standing still, desired him to be called. And they call the blind [man], saying to him, Be of good courage, rise up, he calls thee.
Yesu akasimama na kusema, “Mwiteni.” Hivyo wakamwita yule mtu kipofu, wakamwambia, “Jipe moyo! Inuka, anakuita.”
50 And, throwing away his garment, he started up and came to Jesus.
Akiwa analivua lile joho lake, alisimama na kumwendea Yesu.
51 And Jesus answering says to him, What wilt thou that I shall do to thee? And the blind [man] said to him, Rabboni, that I may see.
Yesu akamuuliza, “Unataka nikufanyie nini?” Yule kipofu akajibu, “Mwalimu, nataka kuona.”
52 And Jesus said to him, Go, thy faith has healed thee. And he saw immediately, and followed him in the way.
Yesu akamwambia, “Nenda zako, imani yako imekuponya.” Mara akapata kuona, akamfuata Yesu njiani.

< Mark 10 >