< Luke 1 >

1 Forasmuch as many have undertaken to draw up a relation concerning the matters fully believed among us,
Kwa kuwa watu wengi wamekaa ili kuandika habari za mambo yaliyotukia katikati yetu,
2 as those who from the beginning were eye-witnesses of and attendants on the Word have delivered them to us,
kama vile yalivyokabidhiwa kwetu na wale waliokuwa mashahidi walioyaona na watumishi wa Bwana,
3 it has seemed good to me also, accurately acquainted from the origin with all things, to write to thee with method, most excellent Theophilus,
mimi nami baada ya kuchunguza kila kitu kwa uangalifu kuanzia mwanzo, niliamua kukuandikia habari za mambo hayo, ewe mtukufu Theofilo,
4 that thou mightest know the certainty of those things in which thou hast been instructed.
ili upate kujua ukweli kuhusu yale uliyofundishwa.
5 There was in the days of Herod, the king of Judaea, a certain priest, by name Zacharias, of the course of Abia, and his wife of the daughters of Aaron, and her name Elizabeth.
Wakati wa Herode mfalme wa Uyahudi, palikuwa na kuhani mmoja jina lake Zekaria, ambaye alikuwa wa ukoo wa kikuhani wa Abiya. Elizabeti mkewe alikuwa pia mzao wa Aroni.
6 And they were both just before God, walking in all the commandments and ordinances of the Lord blameless.
Zekaria na Elizabeti mkewe wote walikuwa watu wanyofu mbele za Mungu, wakizishika amri zote za Bwana na maagizo yote bila lawama.
7 And they had no child, because Elizabeth was barren, and they were both advanced in years.
Lakini walikuwa hawana watoto, kwa sababu Elizabeti alikuwa tasa; nao wote wawili walikuwa wazee sana.
8 And it came to pass, as he fulfilled his priestly service before God in the order of his course,
Siku moja ilipokuwa zamu ya kikundi cha Zekaria, yeye akifanya kazi ya ukuhani Hekaluni mbele za Mungu,
9 it fell to him by lot, according to the custom of the priesthood, to enter into the temple of the Lord to burn incense.
alichaguliwa kwa kura kwa kufuata desturi za ukuhani, kuingia Hekaluni mwa Bwana ili kufukiza uvumba.
10 And all the multitude of the people were praying without at the hour of incense.
Nao wakati wa kufukiza uvumba ulipowadia, wale wote waliokuwa wamekusanyika ili kuabudu walikuwa nje wakiomba.
11 And an angel of [the] Lord appeared to him, standing on the right of the altar of incense.
Ndipo malaika wa Bwana, akiwa amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya kufukizia uvumba, akamtokea Zekaria.
12 And Zacharias was troubled, seeing [him], and fear fell upon him.
Zekaria alipomwona huyo malaika, akafadhaika sana, akajawa na hofu.
13 But the angel said to him, Fear not, Zacharias, because thy supplication has been heard, and thy wife Elizabeth shall bear thee a son, and thou shalt call his name John.
Lakini malaika akamwambia, “Usiogope, Zekaria, kwa maana Mungu amesikia maombi yako. Mkeo Elizabeti atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utamwita jina lake Yohana.
14 And he shall be to thee joy and rejoicing, and many shall rejoice at his birth.
Yeye atakuwa furaha na shangwe kwako, nao watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
15 For he shall be great before [the] Lord, and he shall drink no wine nor strong drink; and he shall be filled with [the] Holy Spirit, even from his mother's womb.
Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele za Bwana, kamwe hataonja mvinyo wala kinywaji chochote cha kulevya, naye atajazwa Roho Mtakatifu hata kabla ya kuzaliwa kwake.
16 And many of the sons of Israel shall he turn to [the] Lord their God.
Naye atawageuza wengi wa wana wa Israeli warudi kwa Bwana Mungu wao.
17 And he shall go before him in [the] spirit and power of Elias, to turn hearts of fathers to children, and disobedient ones to [the] thoughts of just [men], to make ready for [the] Lord a prepared people.
Naye atatangulia mbele za Bwana katika roho na nguvu ya Eliya, ili kuigeuza mioyo ya baba kuwaelekea watoto wao, na wasiotii warejee katika hekima ya wenye haki, ili kuliweka tayari taifa lililoandaliwa kwa ajili ya Bwana.”
18 And Zacharias said to the angel, How shall I know this, for I am an old man, and my wife advanced in years?
Zekaria akamuuliza malaika, “Jambo hilo linawezekanaje? Mimi ni mzee na mke wangu pia ana umri mkubwa.”
19 And the angel answering, said to him, I am Gabriel, who stand before God, and I have been sent to speak to thee, and to bring these glad tidings to thee;
Malaika akamjibu, akamwambia, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele za Mungu, nami nimetumwa kwako ili nikuambie habari hizi njema.
20 and behold, thou shalt be silent and not able to speak, till the day in which these things shall take place, because thou hast not believed my words, the which shall be fulfilled in their time.
Basi sasa kwa kuwa hujaamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati wake, utakuwa bubu hadi siku ile mambo haya yatakapotukia.”
21 And the people were awaiting Zacharias, and they wondered at his delaying in the temple.
Wakati huo watu walikuwa wanamngojea Zekaria nje huku wakishangaa kukawia kwake mle Hekaluni.
22 But when he came out he could not speak to them, and they recognised that he had seen a vision in the temple. And he was making signs to them, and continued dumb.
Alipotoka akawa hawezi kusema nao, wao wakatambua kuwa ameona maono ndani ya Hekalu. Lakini kwa kuwa alikuwa bubu, akawa anawaashiria kwa mikono.
23 And it came to pass, when the days of his service were completed, he departed to his house.
Muda wake wa kuhudumu Hekaluni ulipomalizika, akarudi nyumbani kwake.
24 Now after these days, Elizabeth his wife conceived, and hid herself five months, saying,
Baada ya muda usio mrefu, Elizabeti mkewe akapata mimba, naye akajitenga kwa miezi mitano.
25 Thus has [the] Lord done to me in [these] days in which he looked upon [me] to take away my reproach among men.
Akasema, “Hili ndilo Bwana alilonitendea aliponiangalia kwa upendeleo na kuniondolea aibu yangu mbele ya watu.”
26 But in the sixth month, the angel Gabriel was sent of God to a city of Galilee, of which [the] name [was] Nazareth,
Mwezi wa sita baada ya Elizabeti kupata mimba, Mungu alimtuma malaika Gabrieli aende Galilaya katika mji wa Nazareti,
27 to a virgin betrothed to a man whose name [was] Joseph, of the house of David; and the virgin's name [was] Mary.
kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu mmoja jina lake Yosefu wa nyumba ya Daudi. Jina la huyu mwanamwali bikira ni Maria.
28 And the angel came in to her, and said, Hail, [thou] favoured one! the Lord [is] with thee: [blessed art thou amongst women].
Naye malaika akaja kwake akamwambia: “Salamu, wewe uliyebarikiwa, Bwana yu pamoja nawe!”
29 But she, [seeing] [the angel], was troubled at his word, and reasoned in her mind what this salutation might be.
Maria akafadhaishwa sana na maneno haya, akajiuliza moyoni, “Salamu hii ni ya namna gani?”
30 And the angel said to her, Fear not, Mary, for thou hast found favour with God;
Ndipo malaika akamwambia, “Usiogope, Maria, umepata kibali kwa Mungu.
31 and behold, thou shalt conceive in the womb and bear a son, and thou shalt call his name Jesus.
Tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanaume na utamwita jina lake Yesu.
32 He shall be great, and shall be called Son of [the] Highest; and [the] Lord God shall give him the throne of David his father;
Yeye atakuwa mkuu, naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
33 and he shall reign over the house of Jacob for the ages, and of his kingdom there shall not be an end. (aiōn g165)
Ataimiliki nyumba ya Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn g165)
34 But Mary said to the angel, How shall this be, since I know not a man?
Maria akamuuliza huyo malaika, “Maadamu mimi ni bikira, jambo hili litawezekanaje?”
35 And the angel answering said to her, [The] Holy Spirit shall come upon thee, and power of [the] Highest overshadow thee, wherefore the holy thing also which shall be born shall be called Son of God.
Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, nazo nguvu zake Yeye Aliye Juu Sana zitakufunika kama kivuli. Kwa hiyo mtoto atakayezaliwa atakuwa mtakatifu, naye ataitwa Mwana wa Mungu.
36 And behold, Elizabeth, thy kinswoman, she also has conceived a son in her old age, and this is the sixth month to her that was called barren:
Tazama, jamaa yako Elizabeti amechukua mimba katika uzee wake, na huu ni mwezi wake wa sita, yeye aliyeitwa tasa.
37 for nothing shall be impossible with God.
Kwa maana kwa Mungu hakuna lisilowezekana.”
38 And Mary said, Behold the bondmaid of [the] Lord; be it to me according to thy word. And the angel departed from her.
Maria akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa Bwana. Na iwe kwangu kama ulivyosema.” Kisha malaika akaondoka, akamwacha.
39 And Mary, rising up in those days, went into the hill country with haste, to a city of Judah,
Wakati huo Maria akajiandaa, akaharakisha kwenda katika mji mmoja kwenye vilima vya Uyahudi.
40 and entered into the house of Zacharias, and saluted Elizabeth.
Akaingia nyumbani kwa Zekaria na kumsalimu Elizabeti.
41 And it came to pass, as Elizabeth heard the salutation of Mary, the babe leaped in her womb; and Elizabeth was filled with [the] Holy Spirit,
Naye Elizabeti aliposikia salamu ya Maria, mtoto aliyekuwa tumboni mwake akaruka. Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu,
42 and cried out with a loud voice and said, Blessed [art] thou amongst women, and blessed the fruit of thy womb.
akapaza sauti kwa nguvu akasema, “Umebarikiwa wewe miongoni mwa wanawake, naye mtoto utakayemzaa amebarikiwa.
43 And whence [is] this to me, that the mother of my Lord should come to me?
Lakini ni kwa nini mimi nimepata upendeleo kiasi hiki, hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
44 For behold, as the voice of thy salutation sounded in my ears, the babe leaped with joy in my womb.
Mara tu niliposikia sauti ya salamu yako, mtoto aliyeko tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
45 And blessed [is] she that has believed, for there shall be a fulfilment of the things spoken to her from [the] Lord.
Amebarikiwa yeye aliyeamini kwamba lile Bwana alilomwambia litatimizwa.”
46 And Mary said, My soul magnifies the Lord,
Naye Maria akasema: “Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,
47 and my spirit has rejoiced in God my Saviour.
nayo roho yangu inamfurahia Mungu Mwokozi wangu,
48 For he has looked upon the low estate of his bondmaid; for behold, from henceforth all generations shall call me blessed.
kwa kuwa ameangalia kwa fadhili unyonge wa mtumishi wake. Hakika tangu sasa vizazi vyote vitaniita aliyebarikiwa,
49 For the Mighty One has done to me great things, and holy [is] his name;
kwa maana yeye Mwenye Nguvu amenitendea mambo ya ajabu: jina lake ni takatifu.
50 and his mercy [is] to generations and generations to them that fear him.
Rehema zake huwaendea wale wamchao, kutoka kizazi hadi kizazi.
51 He has wrought strength with his arm; he has scattered haughty [ones] in the thought of their heart.
Kwa kuwa ametenda mambo ya ajabu kwa mkono wake; amewatawanya wale wenye kiburi ndani ya mioyo yao.
52 He has put down rulers from thrones, and exalted the lowly.
Amewashusha watawala toka kwenye viti vyao vya enzi, lakini amewainua wanyenyekevu.
53 He has filled the hungry with good things, and sent away the rich empty.
Amewashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
54 He has helped Israel his servant, in order to remember mercy,
Amemsaidia mtumishi wake Israeli, kwa kukumbuka ahadi yake ya kumrehemu
55 (as he spoke to our fathers, ) to Abraham and to his seed for ever. (aiōn g165)
Abrahamu na uzao wake milele, kama alivyowaahidi baba zetu.” (aiōn g165)
56 And Mary abode with her about three months, and returned to her house.
Maria akakaa na Elizabeti karibu miezi mitatu, kisha akarudi nyumbani kwake.
57 But the time was fulfilled for Elizabeth that she should bring forth, and she gave birth to a son.
Ulipowadia wakati wa Elizabeti kujifungua, alizaa mtoto mwanaume.
58 And her neighbours and kinsfolk heard that [the] Lord had magnified his mercy with her, and they rejoiced with her.
Majirani zake na jamii zake wakasikia jinsi Bwana alivyomfanyia rehema kuu, nao wakafurahi pamoja naye.
59 And it came to pass on the eighth day they came to circumcise the child, and they called it after the name of his father, Zacharias.
Siku ya nane wakaja kumtahiri mtoto, wakataka yule mtoto aitwe Zekaria, ambalo ndilo jina la baba yake.
60 And his mother answering said, No; but he shall be called John.
Lakini mama yake akakataa na kusema, “Hapana! Jina lake ataitwa Yohana.”
61 And they said to her, There is no one among thy kinsfolk who is called by this name.
Wakamwambia, “Hakuna mtu yeyote katika jamaa yako mwenye jina kama hilo.”
62 And they made signs to his father as to what he might wish it to be called.
Basi wakamfanyia Zekaria baba yake ishara ili kujua kwamba yeye angependa kumpa mtoto jina gani.
63 And having asked for a writing-table, he wrote saying, John is his name. And they all wondered.
Akaomba wampe kibao cha kuandikia na kwa mshangao wa kila mtu akaandika: “Jina lake ni Yohana.”
64 And his mouth was opened immediately, and his tongue, and he spake, blessing God.
Papo hapo kinywa chake kikafunguliwa na ulimi wake ukaachiwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
65 And fear came upon all who dwelt round about them; and in the whole hill-country of Judaea all these things were the subject of conversation.
Majirani wote wakajawa na hofu ya Mungu, na katika nchi yote ya vilima vya Uyahudi watu walikuwa wakinena juu ya mambo haya yote.
66 And all who heard them laid them up in their heart, saying, What then will this child be? And [the] Lord's hand was with him.
Kila aliyesikia habari hizi alishangaa akauliza, “Je, mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
67 And Zacharias his father was filled with [the] Holy Spirit, and prophesied, saying,
Zekaria, baba yake, akajazwa na Roho Mtakatifu, naye akatoa unabii, akisema:
68 Blessed be [the] Lord the God of Israel, because he has visited and wrought redemption for his people,
“Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa kuwa amewajilia watu wake na kuwakomboa.
69 and raised up a horn of deliverance for us in the house of David his servant;
Naye ametusimamishia pembe ya wokovu katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,
70 as he spoke by [the] mouth of his holy prophets, who have been since the world began; (aiōn g165)
kama alivyonena kwa vinywa vya manabii wake watakatifu tangu zamani, (aiōn g165)
71 deliverance from our enemies and out of the hand of all who hate us;
kwamba atatuokoa kutoka kwa adui zetu, na kutoka mikononi mwao wote watuchukiao:
72 to fulfil mercy with our fathers and remember his holy covenant,
ili kuonyesha rehema kwa baba zetu na kukumbuka Agano lake takatifu,
73 [the] oath which he swore to Abraham our father,
kiapo alichomwapia baba yetu Abrahamu:
74 to give us, that, saved out of the hand of our enemies, we should serve him without fear
kutuokoa kutoka mikononi mwa adui zetu, tupate kumtumikia yeye pasipo hofu
75 in piety and righteousness before him all our days.
katika utakatifu na haki mbele zake, siku zetu zote.
76 And thou, child, shalt be called [the] prophet of [the] Highest; for thou shalt go before the face of [the] Lord to make ready his ways;
“Nawe mtoto wangu, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana; kwa kuwa utamtangulia Bwana na kuandaa njia kwa ajili yake,
77 to give knowledge of deliverance to his people by [the] remission of their sins
kuwajulisha watu wake juu ya wokovu utakaopatikana kwa kusamehewa dhambi zao,
78 on account of [the] bowels of mercy of our God; wherein [the] dayspring from on high has visited us,
kwa ajili ya wingi wa rehema za Mungu wetu, nuru itokayo juu itatuzukia
79 to shine upon them who were sitting in darkness and in [the] shadow of death, to guide our feet into [the] way of peace.
ili kuwaangazia wale waishio gizani na katika uvuli wa mauti, kuiongoza miguu yetu katika njia ya amani.”
80 — And the child grew and was strengthened in spirit; and he was in the deserts until the day of his shewing to Israel.
Yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu katika roho; akaishi nyikani hadi siku ile alipojionyesha hadharani kwa Waisraeli.

< Luke 1 >