< John 8 >
1 But Jesus went to the mount of Olives.
Lakini Yesu akaenda katika Mlima wa Mizeituni.
2 And early in the morning he came again into the temple, and all the people came to him; and he sat down and taught them.
Alfajiri na mapema Yesu akaja tena Hekaluni, watu wote wakakusanyika, akakaa akaanza kuwafundisha.
3 And the scribes and the Pharisees bring [to him] a woman taken in adultery, and having set her in the midst,
Walimu wa sheria na Mafarisayo wakamleta mwanamke mmoja aliyefumaniwa akizini. Wakamsimamisha katikati ya umati wa watu wote.
4 they say to him, Teacher, this woman has been taken in the very act, committing adultery.
Wakamwambia Yesu, “Mwalimu, huyu mwanamke amekutwa akizini.
5 Now in the law Moses has commanded us to stone such; thou therefore, what sayest thou?
Katika sheria, Mose alituamuru kuwapiga kwa mawe wanawake wa namna hii, mpaka wafe. Sasa wewe wasemaje?”
6 But this they said proving him, that they might have [something] to accuse him [of]. But Jesus, having stooped down, wrote with his finger on the ground.
Walimuuliza swali hili kama mtego ili wapate sababu ya kumshtaki. Lakini Yesu akainama akaanza kuandika ardhini kwa kidole chake.
7 But when they continued asking him, he lifted himself up and said to them, Let him that is without sin among you first cast the stone at her.
Walipoendelea kumuulizauliza akainuka, akawaambia, “Kama kuna mtu yeyote miongoni mwenu ambaye hana dhambi na awe wa kwanza kumtupia jiwe.”
8 And again stooping down he wrote on the ground.
Akainama tena na kuandika ardhini.
9 But they, having heard [that], went out one by one beginning from the elder ones until the last; and Jesus was left alone and the woman standing there.
Waliposikia haya, wakaanza kuondoka mmoja mmoja, wakianzia wazee, hadi Yesu akabaki peke yake na yule mwanamke akiwa amesimama mbele yake.
10 And Jesus, lifting himself up and seeing no one but the woman, said to her, Woman, where are those thine accusers? Has no one condemned thee?
Yesu akainuka na kumwambia, “Wako wapi wale waliokuwa wanakuhukumu kuwa mwenye hatia?”
11 And she said, No one, sir. And Jesus said to her, Neither do I condemn thee: go, and sin no more.
Yule mwanamke akajibu, “Hakuna hata mmoja Bwana.” Yesu akamwambia, “Hata mimi sikuhukumu. Nenda zako, kuanzia sasa usitende dhambi tena.”]
12 Again therefore Jesus spoke to them, saying, I am the light of the world; he that follows me shall not walk in darkness, but shall have the light of life.
Kisha Yesu akasema nao tena akawaambia, “Mimi ni nuru ya ulimwengu. Mtu yeyote akinifuata hatatembea gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.”
13 The Pharisees therefore said to him, Thou bearest witness concerning thyself; thy witness is not true.
Mafarisayo wakamwambia, “Ushuhuda wako haukubaliki kwa kuwa unajishuhudia mwenyewe.”
14 Jesus answered and said to them, Even if I bear witness concerning myself, my witness is true, because I know whence I came and whither I go: but ye know not whence I come and whither I go.
Yesu akawajibu, “Hata kama najishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu ni kweli kwa sababu najua nilikotoka na ninakokwenda. Lakini ninyi hamjui nilikotoka wala ninakokwenda.
15 Ye judge according to the flesh, I judge no one.
Ninyi mnahukumu kwa kufuata vipimo vya kibinadamu, mimi simhukumu mtu yeyote.
16 And if also I judge, my judgment is true, because I am not alone, but I and the Father who has sent me.
Lakini hata kama nikihukumu, uamuzi wangu ni sahihi kwa sababu sitoi hukumu yangu peke yangu, bali niko pamoja na Baba, aliyenituma.
17 And in your law too it is written that the testimony of two men is true:
Imeandikwa katika Sheria yenu kwamba, ushahidi wa watu wawili ni thabiti.
18 I am [one] who bear witness concerning myself, and the Father who has sent me bears witness concerning me.
Mimi najishuhudia mwenyewe, naye Baba aliyenituma hunishuhudia.”
19 They said to him therefore, Where is thy Father? Jesus answered, Ye know neither me nor my Father. If ye had known me, ye would have known also my Father.
Ndipo wakamuuliza, “Huyo Baba yako yuko wapi?” Yesu akawajibu, “Ninyi hamnifahamu mimi ni nani, wala hammfahamu Baba yangu. Kama mngenifahamu mimi, mngemfahamu na Baba yangu.”
20 These words spoke he in the treasury, teaching in the temple; and no one took him, for his hour was not yet come.
Yesu alisema maneno haya alipokuwa akifundisha katika chumba cha hazina Hekaluni. Lakini hakuna mtu aliyemkamata kwa kuwa saa yake ilikuwa haijawadia.
21 He said therefore again to them, I go away, and ye shall seek me, and shall die in your sin; where I go ye cannot come.
Yesu akawaambia tena, “Ninaenda zangu, nanyi mtanitafuta, lakini mtakufa katika dhambi zenu. Niendako mimi ninyi hamwezi kuja.”
22 The Jews therefore said, Will he kill himself, that he says, Where I go ye cannot come?
Ndipo wale Wayahudi wakasema, “Je, atajiua? Je, hii ndiyo sababu amesema, ‘Niendako mimi ninyi hamwezi kuja’?”
23 And he said to them, Ye are from beneath; I am from above. Ye are of this world; I am not of this world.
Akawaambia, “Ninyi mmetoka chini, mimi nimetoka juu. Ninyi ni wa ulimwengu huu, mimi si wa ulimwengu huu.
24 I said therefore to you, that ye shall die in your sins; for unless ye shall believe that I am [he], ye shall die in your sins.
Niliwaambia kuwa mtakufa katika dhambi zenu, kwa maana msipoamini ya kwamba ‘Mimi Ndiye,’ mtakufa katika dhambi zenu.”
25 They said therefore to him, Who art thou? [And] Jesus said to them, Altogether that which I also say to you.
Wakamuuliza, “Wewe ni nani?” Naye Yesu akawajibu, “Mimi ndiye yule ambaye nimekuwa nikiwaambia tangu mwanzo.
26 I have many things to say and to judge concerning you, but he that has sent me is true, and I, what I have heard from him, these things I say to the world.
Nina mambo mengi ya kusema juu yenu na mengi ya kuwahukumu. Lakini yeye aliyenituma ni wa kweli, nami nanena na ulimwengu niliyoyasikia kutoka kwake.”
27 They knew not that he spoke to them of the Father.
Hawakuelewa kuwa alikuwa akiwaambia juu ya Baba yake wa Mbinguni.
28 Jesus therefore said to them, When ye shall have lifted up the Son of man, then ye shall know that I am [he], and [that] I do nothing of myself, but as the Father has taught me I speak these things.
Kisha Yesu akawaambia, “Mtakapokwisha kumwinua juu Mwana wa Adamu, ndipo mtakapojua kuwa, ‘Mimi ndiye yule niliyesema na kwamba mimi sitendi jambo lolote peke yangu bali ninasema yale tu ambayo Baba yangu amenifundisha.
29 And he that has sent me is with me; he has not left me alone, because I do always the things that are pleasing to him.
Yeye aliyenituma yu pamoja nami, hajaniacha, kwa kuwa siku zote nafanya mapenzi yake.’”
30 As he spoke these things many believed on him.
Wengi waliomsikia Yesu akisema maneno haya wakamwamini.
31 Jesus therefore said to the Jews who believed him, If ye abide in my word, ye are truly my disciples;
Kisha Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, “Kama mkidumu katika maneno yangu, mtakuwa wanafunzi wangu kweli kweli.
32 and ye shall know the truth, and the truth shall set you free.
Ndipo mtaijua kweli nayo kweli itawaweka huru.”
33 They answered him, We are Abraham's seed, and have never been under bondage to any one; how sayest thou, Ye shall become free?
Wao wakamjibu, “Sisi tu wazao wa Abrahamu, nasi hatujawa watumwa wa mtu yeyote. Wawezaje kusema kwamba tutawekwa huru?”
34 Jesus answered them, Verily, verily, I say to you, Every one that practises sin is the bondman of sin.
Yesu akajibu, “Amin, amin nawaambia, kila atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi.
35 Now the bondman abides not in the house for ever: the son abides for ever. (aiōn )
Mtumwa hakai nyumbani anakotumika siku zote, lakini mwana hukaa nyumbani daima. (aiōn )
36 If therefore the Son shall set you free, ye shall be really free.
Hivyo Mwana akiwaweka huru mtakuwa huru kweli kweli.
37 I know that ye are Abraham's seed; but ye seek to kill me, because my word has no entrance in you.
Ninajua ya kuwa ninyi ni wazao wa Abrahamu, lakini mnatafuta wasaa wa kuniua kwa sababu ndani yenu hamna nafasi ya neno langu.
38 I speak what I have seen with my Father, and ye then do what ye have seen with your father.
Ninasema yale niliyoyaona mbele za Baba yangu, nanyi inawapa kufanya yale mliyosikia kutoka kwa baba yenu.”
39 They answered and said to him, Abraham is our father. Jesus says to them, If ye were Abraham's children, ye would do the works of Abraham;
Wakajibu, “Baba yetu ni Abrahamu.” Yesu akawaambia, “Kama mngekuwa wazao wa Abrahamu mngefanya mambo yale aliyofanya Abrahamu.
40 but now ye seek to kill me, a man who has spoken the truth to you, which I have heard from God: this did not Abraham.
Lakini sasa ninyi mnatafuta kuniua, mtu ambaye nimewaambia kweli ile niliyosikia kutoka kwa Mungu, Abrahamu hakufanya jambo la namna hii.
41 Ye do the works of your father. They said [therefore] to him, We are not born of fornication; we have one father, God.
Ninyi mnafanya mambo afanyayo baba yenu.” Wakamjibu, “Sisi hatukuzaliwa kwa uzinzi. Tunaye Baba mmoja, Mungu pekee.”
42 Jesus said to them, If God were your father ye would have loved me, for I came forth from God and am come [from him]; for neither am I come of myself, but he has sent me.
Yesu akawaambia, “Kama Mungu angekuwa Baba yenu, mngenipenda, kwa maana nilitoka kwa Mungu na sasa niko hapa. Sikuja kwa ajili yangu mwenyewe, ila yeye alinituma.
43 Why do ye not know my speech? Because ye cannot hear my word.
Kwa nini hamwelewi ninayowaambia? Ni kwa sababu hamwezi kusikia nisemacho.
44 Ye are of the devil, as [your] father, and ye desire to do the lusts of your father. He was a murderer from the beginning, and has not stood in the truth, because there is no truth in him. When he speaks falsehood, he speaks of what is his own; for he is a liar and its father:
Ninyi ni watoto wa baba yenu ibilisi, nanyi mnataka kutimiza matakwa ya baba yenu. Yeye alikuwa muuaji tangu mwanzo, wala hakushikana na kweli maana hamna kweli ndani yake. Asemapo uongo husema yaliyo yake mwenyewe kwa maana yeye ni mwongo na baba wa huo uongo.
45 and because I speak the truth, ye do not believe me.
Lakini kwa sababu nimewaambia kweli hamkuniamini!
46 Which of you convinces me of sin? If I speak truth, why do ye not believe me?
Je, kuna yeyote miongoni mwenu awezaye kunithibitisha kuwa mwenye dhambi? Kama nawaambia yaliyo kweli, mbona hamniamini?
47 He that is of God hears the words of God: therefore ye hear [them] not, because ye are not of God.
Yeye atokaye kwa Mungu husikia kile Mungu asemacho. Sababu ya ninyi kutosikia ni kwa kuwa hamtokani na Mungu.”
48 The Jews answered and said to him, Say we not well that thou art a Samaritan and hast a demon?
Wayahudi wakamjibu Yesu, “Je, hatuko sahihi tunaposema ya kwamba wewe ni Msamaria na ya kwamba una pepo mchafu?”
49 Jesus answered, I have not a demon; but I honour my Father, and ye dishonour me.
Yesu akawajibu, “Mimi sina pepo mchafu, bali ninamheshimu Baba yangu, nanyi mnanidharau.
50 But I do not seek my own glory: there is he that seeks and judges.
Lakini mimi sitafuti utukufu wangu mwenyewe, bali yuko anayetaka kunitukuza, naye ndiye mwamuzi.
51 Verily, verily, I say unto you, If any one shall keep my word, he shall never see death. (aiōn )
Amin, amin nawaambia, mtu yeyote akilitii neno langu hataona mauti milele.” (aiōn )
52 The Jews therefore said to him, Now we know that thou hast a demon. Abraham has died, and the prophets, and thou sayest, If any one keep my word, he shall never taste death. (aiōn )
Ndipo Wayahudi wakamwambia, “Sasa tumejua kwamba una pepo mchafu. Ikiwa Abrahamu alikufa na vivyo hivyo manabii, nawe unasema ‘Mtu akitii neno langu hatakufa milele.’ (aiōn )
53 Art thou greater than our father Abraham, who has died? and the prophets have died: whom makest thou thyself?
Je, wewe ni mkuu kuliko baba yetu Abrahamu ambaye alikufa na manabii ambao nao pia walikufa? Hivi wewe unajifanya kuwa nani?”
54 Jesus answered, If I glorify myself, my glory is nothing: it is my Father who glorifies me, [of] whom ye say, He is our God.
Yesu akawajibu, “Kama nikijitukuza utukufu wangu hauna maana. Baba yangu, huyo ambaye ninyi mnadai kuwa ni Mungu wenu, ndiye anitukuzaye mimi.
55 And ye know him not; but I know him; and if I said, I know him not, I should be like you, a liar. But I know him, and I keep his word.
Ingawa hamkumjua, mimi ninamjua. Kama ningesema simjui, ningekuwa mwongo kama ninyi, lakini mimi ninamjua na ninalitii neno lake.
56 Your father Abraham exulted in that he should see my day, and he saw and rejoiced.
Baba yenu Abrahamu alishangilia kwamba angaliiona siku yangu, naye akaiona na akafurahi.”
57 The Jews therefore said to him, Thou hast not yet fifty years, and hast thou seen Abraham?
Wayahudi wakamwambia, “Wewe hujatimiza hata miaka hamsini, wewe wasema umemwona Abrahamu?”
58 Jesus said to them, Verily, verily, I say unto you, Before Abraham was, I am.
Yesu akawaambia, “Amin, amin nawaambia, kabla Abrahamu hajakuwako, ‘Mimi niko.’”
59 They took up therefore stones that they might cast [them] at him; but Jesus hid himself and went out of the temple, [going through the midst of them, and thus passed on.]
Ndipo wakaokota mawe ili kumpiga, lakini Yesu akajificha, naye akatoka Hekaluni.