< Hosea 11 >

1 Just as the morning passes, so has the king of Israel passed by. For Israel was a child and I loved him; and out of Egypt I called my son.
“Wakati Israeli alipokuwa mtoto, nilimpenda, nilimwita mwanangu kutoka Misri.
2 They called them, and so they departed before their face. They offered victims to the Baals, and they sacrificed to graven images.
Lakini kadiri nilivyomwita Israeli, ndivyo walivyokwenda mbali nami. Walitoa dhabihu kwa Mabaali na kufukiza uvumba kwa vinyago.
3 And I was like a foster father to Ephraim. I carried them in my arms. And they did not know that I healed them.
Mimi ndiye niliyemfundisha Efraimu kutembea, nikiwashika mikono; lakini hawakutambua kuwa ni mimi niliyewaponya.
4 I will draw them with the cords of Adam, with the bands of love. And I will be to them like one who raises the yoke over their jaws. And I will reach down to him so that he may eat.
Niliwaongoza kwa kamba za huruma ya kibinadamu, kwa vifungo vya upendo; niliondoa nira shingoni mwao nami nikainama kuwalisha.
5 He will not return to the land of Egypt, but Assur himself will be the king over him, because they were not willing to be converted.
“Je, hawatarudi Misri, nayo Ashuru haitawatawala kwa sababu wamekataa kutubu?
6 The sword has begun in his cities, and it will consume his elect and devour their heads.
Panga zitametameta katika miji yao, zitaharibu makomeo ya malango yao na kukomesha mipango yao.
7 And my people will long for my return. But a yoke will be imposed on them together, which will not be taken away.
Watu wangu wamedhamiria kuniacha. Hata kama wakimwita Yeye Aliye Juu Sana, kwa vyovyote hatawainua.
8 How will I provide for you, Ephraim; how will I protect you, Israel? How will I provide for you as for Adam; will I set you like Zeboiim? My heart has changed within me; together with my regret, it has been stirred up.
“Efraimu, ninawezaje kukuacha? Ee Israeli, ninawezaje kukutoa? Nitawezaje kukutendea kama Adma? Nitawezaje kukufanya kama Seboimu? Moyo wangu umegeuka ndani yangu, huruma zangu zote zimeamshwa.
9 I will not act on the fury of my wrath. I will not turn back to utterly destroy Ephraim. For I am God, and not man, the Divine in your midst, and I will not advance upon the city.
Sitatimiza hasira yangu kali, wala sitageuka na kumharibu Efraimu. Kwa kuwa mimi ndimi Mungu, wala si mwanadamu, Aliye Mtakatifu miongoni mwenu. Sitakuja kwa ghadhabu.
10 They will walk after the Lord; he will roar like a lion. For he himself will roar, and the sons of the sea will dread.
Watamfuata Bwana; atanguruma kama simba. Wakati angurumapo, watoto wake watakuja wakitetemeka kutoka magharibi.
11 And they will fly like a bird out of Egypt, and like a dove from the land of the Assyrians. And I will arrange them in their own houses, says the Lord.
Watakuja wakitetemeka kama ndege wakitoka Misri, kama hua wakitoka Ashuru. Nitawakalisha katika nyumba zao,” asema Bwana.
12 Ephraim has besieged me with denials, and the house of Israel with deceit. But Judah went down as a witness before God and the holy ones of faith.
Efraimu amenizunguka kwa uongo, nyumba ya Israeli kwa udanganyifu. Naye Yuda ni mkaidi dhidi ya Mungu, hata kinyume cha yule mwaminifu Aliye Mtakatifu.

< Hosea 11 >