< Daniel 1 >
1 In the third year of the reign of Jehoiakim king of Judah, Nebuchadnezzar king of Babylon came to Jerusalem and besieged it.
Katika mwaka wa tatu wa utawala wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda, Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuja akazingira Yerusalemu kwa jeshi.
2 And the Lord delivered into his hand Jehoiakim the king of Judah and a portion of the vessels of the house of God. And he carried them away into the land of Shinar, to the house of his god, and he brought the vessels into the treasure chamber of his god.
Bwana akamtia Yehoyakimu mfalme wa Yuda mkononi mwa Nebukadneza, pamoja na baadhi ya vyombo kutoka Hekalu la Mungu. Hivi akavichukua hadi kwenye hekalu la mungu wake huko Shinari, naye akaviweka nyumbani ya hazina ya mungu wake.
3 And the king told Ashpenaz, the chief of the eunuchs, that he should bring in some of the sons of Israel, and some of the offspring of the king and of the sovereigns:
Kisha mfalme akamwagiza Ashpenazi, mkuu wa maafisa wa mfalme, kumletea baadhi ya Waisraeli kutoka jamaa ya mfalme na kutoka jamaa kuu,
4 young men, in whom there was no blemish, noble in appearance, and accomplished in all wisdom, cautious in knowledge, and well-educated, and who could stand in the palace of the king, so that he might teach them the letters and the language of the Chaldeans.
vijana wanaume wasio na dosari mwilini, wenye sura nzuri, wanaoonyesha kipaji katika kila aina ya elimu, wenye ufahamu mzuri, wepesi kuelewa, na waliofuzu kuhudumu katika jumba la kifalme. Alikuwa awafundishe lugha na maandiko ya Wakaldayo.
5 And the king appointed for them provisions for each day, from his own food and from the wine which he himself drank, so that, after being nourished for three years, they would stand in the sight of the king.
Mfalme akawaagizia kiasi cha chakula na divai ya kila siku kutoka meza ya mfalme. Walikuwa wafundishwe kwa miaka mitatu, na hatimaye waingie kwenye utumishi wa mfalme.
6 Now, among those of the sons of Judah, there were Daniel, Hananiah, Mishael, and Azariah.
Baadhi ya hawa vijana walitoka Yuda: nao ni Danieli, Hanania, Mishaeli na Azaria.
7 And the chief of the eunuchs assigned names to them: to Daniel, Belteshazzar; to Hananiah, Shadrach; to Mishael, Meshach; and to Azariah, Abednego.
Mkuu wa maafisa akawapa majina mapya: Danieli akamwita Belteshaza, Hanania akamwita Shadraki, Mishaeli akamwita Meshaki, na Azaria akamwita Abednego.
8 But Daniel resolved in his heart that he would not be polluted with the king’s meal, nor with the wine he drank, and he requested of the chief of the eunuchs that he might not be contaminated.
Lakini Danieli alikusudia kuwa hatajitia unajisi kwa chakula cha mfalme na divai, naye akamwomba mkuu wa maafisa ruhusa ili asijinajisi kwa njia hii.
9 And so God gave Daniel grace and mercy in the sight of the leader of the eunuchs.
Basi Mungu alikuwa amemfanya huyo mkuu wa maafisa kuonyesha upendeleo na huruma kwa Danieli,
10 And the leader of the eunuchs said to Daniel, “I am afraid of my lord the king, who has appointed food and drink for you, who, if he should see that your faces are leaner than those of the other youths your age, you would condemn my head to the king.”
lakini huyo mkuu wa maafisa akamwambia Danieli, “Ninamwogopa bwana wangu mfalme, aliyeagizia chakula na kinywaji chenu. Kwa nini aone nyuso zenu zikiwa mbaya kuliko za vijana wengine wa rika lenu? Mfalme atakata kichwa changu kwa sababu yenu.”
11 And Daniel said to Malasar, whom the leader of the eunuchs had appointed over Daniel, Hananiah, Mishael, and Azariah,
Ndipo Danieli akamwambia mlinzi aliyeteuliwa na huyo mkuu wa maafisa kuwasimamia Danieli, Hanania, Mishaeli na Azaria,
12 “I beg you to test us, your servants, for ten days, and let roots be given to us to eat and water to drink,
“Tafadhali wajaribu watumishi wako kwa siku kumi. Usitupe chochote ila nafaka na mboga za majani tule, na maji ya kunywa.
13 and then observe our faces, and the faces of the children who eat the king’s food, and then deal with your servants according to what you see.”
Baadaye ulinganishe sura zetu na vijana wanaokula chakula cha mfalme, ukawatendee watumishi wako kulingana na unachoona.”
14 When he had heard these words, he tested them for ten days.
Basi akakubali jambo hili, akawajaribu kwa siku kumi.
15 But, after ten days, their faces appeared better and fatter than all the children who had eaten from the king’s food.
Mwisho wa zile siku kumi, walionekana kuwa na afya na kunawiri zaidi kuliko yeyote kati ya wale vijana waliokula chakula cha mfalme.
16 Thereafter, Malasar took away their portions and their wine for drinking, and he gave them roots.
Hivyo mlinzi wao akaondoa chakula chao na divai yao waliopangiwa kula na kunywa, akawapa nafaka na mboga za majani badala yake.
17 Yet, to these children, God gave knowledge and instruction in every book, and wisdom, but to Daniel, also the understanding of all visions and dreams.
Mungu akawapa hawa vijana wanne maarifa na ufahamu wa kila aina ya maandiko na elimu. Naye Danieli aliweza kufahamu maono na aina zote za ndoto.
18 And when the time was completed, after which the king had said that they would be brought in, the chief of the eunuchs brought them in before the sight of Nebuchadnezzar.
Mwisho wa muda uliowekwa na mfalme kuwaingiza kwake, mkuu wa maafisa akawaleta mbele ya Mfalme Nebukadneza.
19 And, when the king conversed with them, there had not been found any so great in all the world as Daniel, Hananiah, Mishael, and Azariah; and so they stood in the sight of the king.
Mfalme akazungumza nao, akaona hakuna aliyelingana na Danieli, Hanania, Mishaeli na Azaria. Hivyo wakaingia katika utumishi wa mfalme.
20 And in every concept of wisdom and understanding, about which the king consulted with them, he found them to be ten times better than all the seers and astrologers put together, who were in his entire kingdom.
Katika kila jambo la hekima na ufahamu kuhusu kile mfalme alichowauliza, aliwaona bora mara kumi zaidi kuliko waganga na wasihiri wote katika ufalme wake wote.
21 And so Daniel remained, even until the first year of king Cyrus.
Naye Danieli akabaki huko mpaka mwaka wa kwanza wa utawala wa Mfalme Koreshi.