< 2 Samuel 21 >
1 And a famine occurred, during the days of David, for three years continuously. And David consulted the oracle of the Lord. And the Lord said: “This is because of Saul, and his house of bloodshed. For he killed the Gibeonites.”
Wakati wa utawala wa Daudi kulikuwa na njaa kwa miaka mitatu mfululizo, kwa hiyo Daudi akautafuta uso wa Bwana. Bwana akasema, “Ni kwa sababu ya Sauli na nyumba yake iliyotiwa madoa ya damu, kwa sababu aliwaua Wagibeoni.”
2 Therefore, the king, calling for the Gibeonites, spoke to them. Now the Gibeonites were not of the sons of Israel, but were the remnant of the Amorites. And the sons of Israel had sworn an oath to them, but Saul wished to strike them in zeal, as if on behalf of the sons of Israel and Judah.
Mfalme akawaita Wagibeoni na kuzumgumza nao. (Wagibeoni hawakuwa wa wana wa Israeli, ila walikuwa mabaki ya Waamori. Waisraeli walikuwa wameapa kuwaacha hai, lakini Sauli katika wivu wake kwa ajili ya Israeli na Yuda, alikuwa amejaribu kuwaangamiza.)
3 Therefore, David said to the Gibeonites: “What shall I do for you? And what shall be your satisfaction, so that you may bless the inheritance of the Lord?”
Daudi akawauliza Wagibeoni, “Niwatendee nini? Nitawaridhishaje ili mbariki urithi wa Bwana?”
4 And the Gibeonites said to him: “There is no quarrel for us over silver or gold, but against Saul and against his house. And we do not desire that any man of Israel be put to death.” The king said to them, “Then what do you wish that I should do for you?”
Wagibeoni wakamjibu, “Hatuna haki ya kudai fedha wala dhahabu kutoka kwa Sauli au jamaa yake, wala hatuna haki ya kumuua mtu yeyote katika Israeli.” Daudi akawauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
5 And they said to the king: “The man who unjustly afflicted and oppressed us, we ought to destroy in such manner that not even one of his stock may be left behind in all the parts of Israel.
Wakamjibu mfalme, “Kwa habari ya mtu aliyetuangamiza na kufanya hila mbaya dhidi yetu ili kwamba tuangamizwe na tusiwe na yeyote katika Israeli,
6 Let seven men from his sons be given to us, so that we may crucify them to the Lord in Gibeon of Saul, formerly the chosen place of the Lord.” And the king said, “I will give them.”
tupatieni wazao wake saba wa kiume tuwaue hadharani mbele za Bwana huko Gibea ya Sauli, aliyekuwa amechaguliwa na Bwana.” Basi mfalme akasema, “Nitawakabidhi kwenu.”
7 But the king spared Mephibosheth, the son of Jonathan, the son of Saul, because of the oath of the Lord which had been made between David and Jonathan, the son of Saul.
Mfalme akamhifadhi Mefiboshethi mwana wa Yonathani, mwana wa Sauli, kwa sababu ya kile kiapo mbele za Bwana kati ya Daudi na Yonathani.
8 And so the king took the two sons of Rizpah, the daughter of Aiah, whom she bore to Saul, Armoni and Mephibosheth, and the five sons of Michal, the daughter of Saul, whom she conceived of Adriel, the son of Barzillai, who was from Meholath,
Lakini mfalme akamchukua Armoni na Mefiboshethi, wana wawili wa Rispa binti Aiya, ambao alikuwa amemzalia Sauli, pamoja na wana watano wa Merabu binti Sauli, aliokuwa amemzalia Adrieli mwana wa Barzilai, Mmeholathi.
9 and he gave them into the hands of the Gibeonites. And they crucified them on a hill in the sight of the Lord. And these seven fell together in the first days of the harvest, when the barley is beginning to be reaped.
Akawakabidhi kwa Wagibeoni, ambao waliwaua na kuwaweka wazi juu ya kilima mbele za Bwana. Wote saba walianguka kwa pamoja; waliuawa katika siku za kwanza za mavuno, mara tu uvunaji wa shayiri ulipokuwa unaanza.
10 Then Rizpah, the daughter of Aiah, taking a haircloth, spread it under herself on a rock, from the beginning of the harvest until water dropped from heaven upon them. And she did not permit the birds to tear them by day, nor the beasts by night.
Rispa binti Aiya akachukua nguo ya gunia, akajitandikia juu ya mwamba. Kuanzia mwanzo wa mavuno mpaka mvua ziliponyesha juu ya miili ya hao waliouawa, Rispa hakuruhusu ndege wa angani kuwagusa wakati wa mchana, wala wanyama wa mwitu wakati wa usiku.
11 And it was reported to David what Rizpah, the daughter of Aiah, the concubine of Saul, had done.
Daudi alipoambiwa kile Rispa binti Aiya, suria wa Sauli, alichokuwa amekifanya,
12 And David went and took the bones of Saul, and the bones of his son Jonathan, from the men of Jabesh Gilead, who had stolen them from the street of Bethshan, where the Philistines had suspended them after they had slain Saul at Gilboa.
alikwenda akachukua mifupa ya Sauli na mwanawe Yonathani kutoka kwa watu wa Yabeshi-Gileadi. (Walikuwa wameichukua kwa siri kutoka uwanja wa watu wote huko Beth-Shani, mahali ambapo Wafilisti walikuwa wamewatundika baada ya kumuua Sauli huko Gilboa.)
13 And he brought the bones of Saul, and the bones of his son Jonathan, from there. And they collected the bones of those who had been crucified.
Daudi akaileta mifupa ya Sauli na ya mwanawe Yonathani kutoka huko, pia mifupa ya wale waliokuwa wameuawa na kutupwa ilikusanywa.
14 And they buried them with the bones of Saul and his son Jonathan, in the land of Benjamin, to the side of the sepulcher of his father Kish. And they did all that the king had instructed. And after these things, God showed favor again to the land.
Wakazika mifupa ya Sauli na ya mwanawe Yonathani katika kaburi la Kishi, babaye Sauli, huko Sela katika nchi ya Benyamini, nao wakafanya kila kitu mfalme alichoagiza. Baada ya hayo, Mungu akajibu maombi kwa ajili ya nchi.
15 Then the Philistines again undertook a battle against Israel. And David descended, and his servants with him, and they fought against the Philistines. But when David grew faint,
Kwa mara nyingine tena kulikuwa na vita kati ya Wafilisti na Israeli. Daudi akashuka pamoja na watu wake ili kupigana dhidi ya Wafilisti, naye akawa amechoka sana.
16 Ishbibenob, who was of the ancestry of Arapha, the iron of whose spear weighed three hundred ounces, who had been girded with a new sword, strove to strike down David.
Naye Ishbi-Benobu, mmoja wa wazao wa Warefai, ambaye mkuki wake ulikuwa na uzito wa shekeli 300 za shaba, alikuwa amejifunga upanga mpya, naye alisema angemuua Daudi.
17 And Abishai, the son of Zeruiah, defended him, and striking the Philistine, he killed him. Then David’s men swore an oath to him, saying, “You shall no longer go out to war with us, lest you extinguish the lamp of Israel.”
Lakini Abishai mwana wa Seruya akaja kumwokoa Daudi; akampiga huyo Mfilisti, akamwangusha chini na kumuua. Ndipo watu wakamwapia Daudi, wakisema, “Kamwe hutakwenda tena nasi vitani, ili kwamba taa ya Israeli isije ikazimwa.”
18 Also, a second war occurred in Gob against the Philistines. Then Sibbecai from Hushah struck down Saph, from the stock of Arapha, of the ancestry of the giants.
Baada ya muda, kukawa na vita nyingine na Wafilisti, huko Gobu. Wakati huo Sibekai, Mhushathi, akamuua Safu, mmoja wa wazao wa Warefai.
19 Then there was a third war in Gob against the Philistines, in which Adeodatus, a son of the forest, a weaver from Bethlehem, struck down Goliath the Gittite, the shaft of whose spear was like the beam used by a cloth maker.
Katika vita vingine na Wafilisti huko Gobu, Elhanani mwana wa Yaare-Oregimu, Mbethlehemu, alimuua nduguye Goliathi, Mgiti, ambaye mkuki wake ulikuwa na mpini kama mti wa mfumaji.
20 A fourth battle was in Gath. In that place, there was a lofty man, who had six digits on each hand and each foot, that is, twenty-four in all, and he was from the origins of Arapha.
Katika vita vingine tena, vilivyopiganwa huko Gathi, kulikuwako na mtu mmoja mkubwa mwenye vidole sita katika kila mkono na vidole sita kila mguu, jumla vidole ishirini na vinne. Yeye alikuwa pia mzao wa Mrefai.
21 And he blasphemed Israel. So Jonathan, the son of Shimei, the brother of David, struck him down.
Alipowadhihaki Israeli, Yonathani mwana wa Shimea, nduguye Daudi, akamuua.
22 These four men were born of Arapha in Gath, and they fell by the hand of David and his servants.
Hawa wanne walikuwa wazao wa Warefai huko Gathi, nao walianguka kwa mikono ya Daudi na watu wake.