< 1 Samuel 1 >
1 There was a certain man from Ramah of Zophim, on Mount Ephraim, and his name was Elkanah, the son of Jeroham, the son of Elihu, the son of Tohu, the son of Zuph, an Ephraimite.
Kulikuwepo na mtu mmoja kutoka Rama, Msufi kutoka nchi ya vilima vya Efraimu, ambaye jina lake aliitwa Elikana mwana wa Yerohamu, mwana wa Elihu mwana wa Tohu, mwana wa Sufu, Mwefraimu.
2 And he had two wives: the name of one was Hannah, and the name of the second was Peninnah. And Peninnah had sons. But Hannah did not have children.
Alikuwa na wake wawili, mmoja aliitwa Hana na mwingine Penina. Penina alikuwa na watoto, lakini Hana hakuwa na mtoto.
3 And this man went up from his city, on the established days, so that he might adore and sacrifice to the Lord of hosts at Shiloh. Now the two sons of Eli, Hophni and Phinehas, priests of the Lord, were in that place.
Kila mwaka mtu huyu alikwea kutoka mji wake ili kuabudu na kutoa dhabihu kwa Bwana Mwenye Nguvu Zote huko Shilo, ambapo Hofni na Finehasi, wana wawili wa Eli, walikuwa makuhani wa Bwana.
4 Then the day arrived, and Elkanah immolated. And he gave portions to his wife Peninnah, and to all her sons and daughters.
Kila mara ilipofika siku ya Elikana kutoa dhabihu, aliwapa mafungu Penina mkewe na wanawe wote pamoja na binti zake.
5 But to Hannah he gave one portion with sorrow. For he loved Hannah, but the Lord had closed her womb.
Lakini alimpa Hana fungu maradufu kwa sababu alimpenda, ingawa Bwana alikuwa amemfunga tumbo.
6 And her rival afflicted her and vehemently distressed her, to a great extent, for she rebuked her that the Lord had closed her womb.
Kwa sababu Bwana alikuwa amemfunga tumbo, mke mwenzake alikuwa anamchokoza ili kumuudhi.
7 And she did so every year, when the time returned for them to ascend to the temple of the Lord. And she provoked her in this way. And so, she wept and did not take food.
Hili liliendelea mwaka baada ya mwaka. Kila mara Hana alipokwenda katika nyumba ya Bwana, mke mwenzake alikuwa akimkasirisha mpaka analia na kushindwa kula.
8 Therefore, her husband Elkanah said to her: “Hannah, why are you weeping? And why do you not eat? And for what reason do you afflict your heart? Am I not better to you than ten sons?”
Elikana mumewe akawa anamwambia, “Hana, kwa nini unalia? Kwa nini huli? Kwa nini kuvunjika moyo? Je, mimi si bora zaidi kwako kuliko watoto kumi?”
9 And so, after she ate and drank at Shiloh, Hannah rose up. And Eli, the priest, was sitting on the seat before the door of the temple of the Lord.
Siku moja walipokuwa wamemaliza kula na kunywa huko Shilo, Hana alisimama. Wakati huo kuhani Eli alikuwa ameketi kwenye kiti pembeni mwa mwimo wa mlango wa Hekalu la Bwana.
10 And since Hannah was bitter in soul, she prayed to the Lord, weeping greatly.
Kwa uchungu wa rohoni Hana alilia sana na akamwomba Bwana.
11 And she made a vow, saying, “O Lord of hosts, if, in looking with favor, you will see the affliction of your servant and will remember me, and will not forget your handmaid, and if you will give to your servant a male child, then I will give him to the Lord all the days of his life, and no razor shall pass over his head.”
Naye akaweka nadhiri, akisema, “Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, laiti ungeangalia huzuni kuu ya mtumishi wako na kunikumbuka mimi, wala usimsahau mtumishi wako nawe ukampa mwana, basi huyo mwana nitamtoa kwa Bwana kwa siku zote za maisha yake, wala wembe hautapita kichwani mwake.”
12 Then it happened that, while she multiplied prayers before the Lord, Eli observed her mouth.
Alipokuwa anaendelea kumwomba Bwana, Eli alichunguza kinywa chake.
13 For Hannah was speaking in her heart, and only her lips moved, and her voice was barely heard. Therefore, Eli considered her to be drunk,
Hana alikuwa akiomba moyoni mwake, midomo yake ikiwa inachezacheza lakini sauti haikusikika. Eli akafikiri alikuwa amelewa
14 and so he said to her: “How long will you be inebriated? You should take only a little wine, but instead you are drenched.”
naye akamwambia, “Utaendelea kulewa mpaka lini? Achilia mbali mvinyo wako.”
15 Responding, Hannah said: “By no means, my lord. For I am an exceedingly unhappy woman, and I drank neither wine, nor anything that can inebriate. Instead, I have poured out my soul in the sight of the Lord.
Hana akajibu, “Si hivyo bwana wangu, mimi ni mwanamke mwenye huzuni kubwa. Mimi sijanywa mvinyo wala kileo, nilikuwa ninaumimina moyo wangu kwa Bwana.
16 You should not repute your handmaid as one of the daughters of Belial. For I have been speaking from the abundance of my sorrow and grief, even until now.”
Usimdhanie mtumishi wako kuwa mwanamke mwovu; nimekuwa nikiomba hapa katika wingi wa uchungu mkuu na huzuni.”
17 Then Eli said to her: “Go in peace. And may the God of Israel grant to you your petition, which you have begged of him.”
Eli akamjibu, “Nenda kwa amani, naye Mungu wa Israeli na akujalie kile ulichomwomba.”
18 And she said, “I wish that your handmaid may find grace in your eyes.” And the woman went on her way, and she ate, and her countenance was no longer changed for the worse.
Hana akasema, “Mtumishi wako na apate kibali machoni pako.” Kisha akaondoka zake na kula chakula, wala uso wake haukuwa na huzuni tena.
19 And they rose up in the morning, and they worshipped before the Lord. And they returned and arrived at their own house at Ramah. Then Elkanah knew his wife Hannah. And the Lord remembered her.
Kesho yake asubuhi na mapema waliamka wakaabudu mbele za Bwana na kisha wakarudi nyumbani kwao huko Rama. Elikana akakutana kimwili na mkewe Hana, naye Bwana akamkumbuka.
20 And it happened that, in the course of days, Hannah conceived and bore a son. And she called his name Samuel, because she had requested him from the Lord.
Hivyo wakati ulipotimia, Hana akapata mimba na akamzaa mwana. Hana akamwita jina lake Samweli, akasema, “Kwa kuwa nilimwomba kwa Bwana.”
21 Now her husband Elkanah ascended with his entire house, so that he might immolate to the Lord a solemn sacrifice, with his vow.
Wakati huyo mtu Elikana alipanda pamoja na jamaa yake yote kutoa dhabihu ya mwaka kwa Bwana na kutimiza nadhiri yake,
22 But Hannah did not go up. For she said to her husband, “I will not go, until the infant has been weaned, and until I may lead him, so that he may appear before the sight of the Lord, and may remain always there.”
Hana hakwenda. Alimwambia mume wake, “Baada ya mtoto kuachishwa kunyonya, nitamchukua na kumpeleka mbele za Bwana, naye ataishi huko wakati wote.”
23 And her husband Elkanah said to her: “Do what seems good to you, and stay until you wean him. And I pray that the Lord may fulfill his word.” Therefore, the woman remained at home, and she breastfed her son, until she withdrew him from milk.
Elikana mumewe akamwambia, “Fanya lile unaloona ni bora zaidi kwako. Ukae hapa mpaka utakapomwachisha kunyonya, Bwana na akujalie kutimiza nadhiri yako.” Hivyo huyo mwanamke akakaa nyumbani na kumnyonyesha mwanawe mpaka alipomwachisha kunyonya.
24 And after she had weaned him, she brought him with her, along with three calves, and three measures of flour, and a small bottle of wine, and she led him to the house of the Lord at Shiloh. But the boy was still a young child.
Baada ya mtoto kuachishwa kunyonya, Hana akamchukua huyo mtoto, akiwa mdogo hivyo hivyo, pamoja na fahali wa miaka mitatu, efa ya unga na kiriba cha divai, naye akamleta mtoto kwenye nyumba ya Bwana huko Shilo.
25 And they immolated a calf, and they presented the boy to Eli.
Walipokwisha kumchinja yule fahali, wakamleta mtoto kwa Eli,
26 And Hannah said: “I beg you, my lord, as your soul lives, my lord: I am that woman, who stood before you here, praying to the Lord.
naye Hana akamwambia Eli, “Hakika kama uishivyo, bwana wangu, mimi ndiye yule mama ambaye alisimama hapa karibu nawe akiomba kwa Bwana.
27 I prayed for this child, and the Lord granted to me my petition, which I asked of him.
Niliomba mtoto huyu, naye Bwana amenijalia kile nilichomwomba.
28 Because of this, I have also lent him to the Lord, for all the days when he shall be lent to the Lord.” And they adored the Lord in that place. And Hannah prayed, and she said:
Hivyo sasa ninamtoa kwa Bwana. Kwa maana maisha yake yote atakuwa ametolewa kwa Bwana.” Naye akamwabudu Bwana huko.