< 1 Samuel 14 >

1 And it happened that, on a certain day, Jonathan, the son of Saul, said to the youth who bore his armor, “Come, and let us go over to the garrison of the Philistines, which is across from that place.” But he did not reveal this to his father.
Siku moja, Yonathani mwana wa Sauli alimwambia mbeba silaha wake aliye mdogo, “Njoo, hebu twende hadi upande mwingine kwenye ngome ya Wafilisti.” Lakini hakumjulisha baba yake.
2 Moreover, Saul was staying in the furthermost part of Gibeah, below the pomegranate tree that was at Migron. And the people with him were about six hundred men.
Sauli alikuwa akikaa nje ya mji wa Gibea chini ya mti wa mkomamanga ulio katika Migroni. Takribani watu mia sita walikwa pamoja naye,
3 And Ahijah, the son of Ahitub, the brother of Ichabod, the son of Phinehas, who had been born of Eli, the priest of the Lord at Shiloh, wore the ephod. But the people did not know where Jonathan had gone.
akiwemo Ahiya mwana wa Ahitubu (nduguye Ikabodi) mwana wa Finehasi, mwana wa Eli, kuhani wa BWANA huko Shilo, aliyevaa naivera. Watu hao hawakujua kwamba Yonathani ameondoka.
4 Now there were, between the ascents along which Jonathan strove to cross to the garrison of the Philistines, rocks projecting from both sides, and, in the manner of teeth, boulders breaking out from one side and the other. The name of one was Shining, and the name of the other was Thorny.
Katikati ya vichochoro, ambavyo Yonathani alinuia kuvipita hadi ngome ya Wafilisti, kulikuwa na mwamba wenye mteremko mkali upande mmoja, na mteremko mkali upande mwingine. Jabali moja liliitwa Bosesi, na jingine liliitwa Sene.
5 One boulder projected toward the north, opposite Michmash, and the other toward the south, opposite Gibeah.
Lile jabali lenye mteremko mkali zaidi liliinuka upande wa kaskazini mbele ya Mikmashi, na jingine upande wa kusini mbele ya Geba.
6 Then Jonathan said to the youth who bore his armor: “Come, let us go across to the garrison of these uncircumcised. And perhaps the Lord may act on our behalf. For it is not difficult for the Lord to save, either by many, or by few.”
Yonathani akamwambia kijana mbeba silaha, “Njoo, na tuvuke hadi ngome ya hawa wasiotahiriwa. Pengine BWANA atatenda kwa niaba yetu, kwa maana hakuna kitu kiwezacho kumzuia BWANA asiokoe kwa wengi au kwa watu wachache.”
7 And his armor bearer said to him: “Do all that is pleasing to your soul. Go wherever you wish, and I will be with you, wherever you will choose.”
Mbeba silaha wake akajibu, “Fanya kila kitu kilicho ndani ya moyo wako. Songa mbele, tazama, niko pamoja nawe, nitatii maagizo yako yote.”
8 And Jonathan said: “Behold, we will cross over to these men. And when we will be seen by them,
Ndipo Yonathani akasema, “Tutavuka twende kwa watu hao, na tutajionesha wenyewe kwao.
9 if they have spoken to us in this way, ‘Stay until we come to you,’ let us stand still in our place, and not ascend to them.
Kama watatuambia, 'Subirini hapo hadi tutakapokuja kwenu' - basi tutabaki katika sehemu yetu na hatutavuka kwenda kwao.
10 But if they will say, ‘Ascend to us,’ let us ascend. For the Lord has delivered them into our hands. This will be the sign to us.”
Lakini kama watajibu, 'Njoni kwetu,' ndipo tutavuka; kwa sababu BWANA amewaweka mkononi mwetu. Hii ndiyo itakuwa ishara yetu.”
11 And so, both of them appeared before the garrison of the Philistines. And the Philistines said, “See, the Hebrews have come out from the holes in which they had been hiding.”
Kwa hiyo wote wawili wakajifunua mbele ya ngome ya Wafilisti. Wafilisti wakasema, “Angalia, Webrania wanakuja kutokea kwenye mashimo walimojificha.”
12 And the men of the garrison spoke to Jonathan and to his armor bearer, and they said, “Ascend to us, and we will show you something.” And Jonathan said to his armor bearer: “Let us ascend. Follow me. For the Lord has delivered them into the hands of Israel.”
Ndipo watu wa ile ngome wakamwita Yonathani na mbeba silaha wake, wakisema, “Njoni huku kwetu, tutawaonesha jambo fulani.” Na Yonathani akamwambia mbeba silaha wake; “Nifuate nyuma yangu, kwa sababu BWANA amewaweka katika mkono wa Israeli.”
13 Then Jonathan ascended, crawling on his hands and feet, and his armor bearer after him. And then, some fell before Jonathan, others his armor bearer killed as he was following him.
Yonathani alipanda juu kwa mikono na miguu yake, na mbeba silaha akimfuata nyuma yake. Wafilisti waliuwawa mbele ya Yonathani, na mbeba silaha wake akiwaua baadhi nyuma yake.
14 And the first slaughter was made when Jonathan and his armor bearer struck down about twenty of the men, in the midst of an area of land that a yoke of oxen would usually plow in a day.
Hilo shambulio la kwanza walilofanya Yonathani na mbeba silaha wake, waliua watu wapatao ishirini katika urefu wa nusu handaki kwenye eka moja ya ardhi.
15 And a miracle occurred in the camp, out in the fields. And all of the people of their garrison, who had gone out in order to plunder, were stupefied. And the earth trembled. And it happened as a miracle from God.
Kukawa na hofu kubwa katika kambi, uwandani, na katika watu. Hata ngome ya jeshi na watekaji nyara nao wakawa na hofu kubwa
16 And the watchmen of Saul, who were at Gibeah of Benjamin, looked out, and behold, a multitude was thrown down and dispersed, this way and that.
Ndipo walinzi wa Sauli huko Gibea ya Benyamini wakaona kundi la askari wa Wafilisti likitawanyika, wakienda kule na huku.
17 And Saul said to the people who were with him, “Inquire and see who has gone out from us.” And when they had inquired, it was found that Jonathan and his armor bearer were not present.
Kisha Sauli akawaambia watu aliokuwa nao, “Mjihesabu ili muone nani hayupo hapa.”Walipokuwa wamehesabu, wakagundua kuwa Yonathani na mbebaji wa silaha zake hawapo.
18 And Saul said to Ahijah, “Bring the ark of the God.” (For the ark of God was, in that day, with the sons of Israel in that place.)
Sauli akamwambia Ahiya, “Lete hapa naivera ya Mungu”- kwa maana siku hiyo Ahiya alivaa naivera akiwa pamoja na askari wa Israeli.
19 And while Saul spoke to the priest, there arose a great tumult in the camp of the Philistines. And it was increasing, little by little, and it was being heard more clearly. And Saul said to the priest, “Withdraw your hand.”
Wakati Sauli akiongea na kuhani, kelele na ghasia kubwa iliendelea na kuongezeka katika kambi ya Wafilisti. dipo sauli akamwambia kuhani, “Acha kazi unayofanya.”
20 Then Saul, and all the people who were with him, cried out together, and they went to the place of the conflict. And behold, each one’s sword had been turned against his neighbor, and there was a very great slaughter.
Sauli na watu wote aliokuwa nao wakajipanga na kwenda kwenye mapigano. Upanga wa kila Mfilisti ulikwa juu ya Mfilisti mwenzake, na kulikuwa na ghasia kubwa.
21 Moreover, the Hebrews who had been with the Philistines yesterday and the day before, and who had ascended with them into the camp, turned back so that they might be with those of Israel who were with Saul and Jonathan.
Basi Waebrania ambao mwanzoni walijiunga na Wafilisti, na kwenda kwenye kambi yao, wao pia waliungana na Waisraeli waliokuwa pamoja na Sauli na Yonathani.
22 Likewise, all the Israelites who had hidden themselves on mount Ephraim, hearing that the Philistines had fled, joined themselves with their own in the battle. And there were with Saul about ten thousand men.
Waisraeli wote waliokuwa wamejificha katika milima karibu na Efraimu waliposikia kwamba Wafilisti wamekimbia, nao pia wakawafuata Wafilisti nakuwafukuza kwenye hiyo vita.
23 And the Lord saved Israel on that day. But the fight continued as far as Bethaven.
Hivyo siku hiyo BWANA aliwaokoa Israeli, na mapigano yalivuka kupitiliza Beth aveni.
24 And the men of Israel were joined together on that day. And Saul made the people swear, saying, “Cursed be the man who will eat bread, until evening, until I am avenged of my enemies.” And the entire people did not consume bread.
Siku hiyo watu wa Israeli walifadhaika kwa sababu Sauli aliwaweka watu chini ya kiapo akasema, “Na alaaniwe mtu atakaye kula chakula kabla ya jioni na kabla sijalipiza kisasi kwa maadui zangu.” Hivyo hakuna hata mmoja kati ya watu wote aliyeonja chakula.
25 And all the common people went into a forest, in which there was honey on the surface of the field.
Ndipo watu wote wakaingia msituni na kuona asali ikiwa juu ya ardhi.
26 And so the people entered the forest, and there appeared flowing honey, but no one drew his hand near his mouth. For the people were afraid of the oath.
Watu walipoingia humo msituni, asali ilitiririka, lakini hakuna aliyeweka mkono wake kinywani kwa maana watu waliogopa kiapo.
27 But Jonathan had not heard that his father had bound the people to an oath. And so he extended the top of the staff that he was holding in his hand, and he dipped it in a honeycomb. And he turned his hand to his mouth, and his eyes were brightened.
Lakini Yonathani alikuwa hajasikia kwamba baba yake amewaagiza watu kwa kiapo. Akanyoosha ncha ya fimbo iliyokuwa mkononi mwake na kuichovya kwenye sega la asali. Kisha akanyoosha mkono wake hadi kinywani mwake, na macho yake yakaangaziwa.
28 And in response, one of the people said, “Your father has bound the people by an oath, saying: ‘Cursed be the man who will eat any bread this day.’” (For the people were faint.)
Ndipo mmoja wa watu hao, akamwambia, “Baba yako aliwaagiza watu kwa mkazo na kwa kiapo, kwa kusema, 'Alaaniwe mtu atakaye kula chakula kwa siku ya leo,' ingawa watu wamedhoofika kwa ajili ya njaa.”
29 And Jonathan said: “My father has troubled the land. You have seen for yourselves that my eyes were brightened, because I tasted a little of this honey.
Baadaye Yonathani alisema, “Baba yangu amefanya matatizo katika nchi. Angalia jinsi macho yangu alivyotiwa nuru kwa sababu nilionja asali hii kidogo.
30 How much more so, if the people had eaten from the plunder that they find with their enemies? Would not a greater slaughter have been accomplished among the Philistines?”
Je, siyo vivuri sana kama leo watu wangekula bila kizuizi nyara walizopata kutoka kwa maadui zao? Kwa sababu sasa mauaji hayakuwa makubwa katikati ya Wafilisti.”
31 Therefore, on that day, they struck down the Philistines, from Michmash as far as Aijalon. But the people were exceedingly wearied.
Siku hiyo waliwashambulia Wafilisti kutoka Mikmashi hadi Aiyaloni. Na watu walikuwa wamechoka sana.
32 And turning to the spoils, they took sheep, and oxen, and calves, and they slew them on the ground. And the people ate with blood.
Hivyo watu wakazivamia nyara na kuchukua kondoo, ng'ombe na ndama na kuwachinja hapo chini. Watu walikula nyama zao pamoja na damu.
33 Then they reported to Saul, saying that the people had sinned against the Lord, eating with blood. And he said: “You have transgressed. Roll a great stone to me, here and now.”
KIsha wakamwambia Sauli, “Tazama, watu wanamtenda BWANA dhambi kwa kula pamoja na damu.” Sauli akasema, “Mmetenda isivyo haki. Sasa, viringisheni jiwe kubwa kwangu.” Sauli akasema,
34 And Saul said: “Disperse yourselves among the common people, and tell each one of them to bring to me his ox and his ram, and to slay them upon this stone, and to eat, so that you will not sin against the Lord, in eating with blood.” And so, each one, out of all the people, brought his ox, by his own hand, throughout the night. And they slew them there.
“Nendeni kati watu, na muwaambie, 'Kila mtu alete ng'ombe na kondoo wake, wawachinje hapa, na kuwala. Msimtende BWANA dhambi kwa kula na damu.”' Kwa hiyo watu wote wakaleta kila mtu na ng'ombe wake usiku huo na kuwachinja mahali hapo.
35 Then Saul built an altar to the Lord. And so, it was then that he first began to build an altar to the Lord.
Sauli akamjengea BWANA madhabahu, ambayo ilikuwa ya kwanza kwake kumjengea BWANA.
36 And Saul said: “Let us fall upon the Philistines by night, and lay waste to them even until the morning light. And let us not leave behind a man among them.” And the people said, “Do all that seems good in your eyes.” And the priest said, “Let us draw near to God in this place.”
Ndipo Sauli akasema, “Haya tuwafukuze Wafilisti usiku na kuwateka nyara hadi asubuhi; tusimwache hata mtu mmoja akiwa hai.” Nao wakamjibu, “Fanya unaloona linakupendeza.” Lakini kuhani akasema, “Hebu na tumkaribie Mungu mahali hapa.”
37 And Saul consulted the Lord: “Shall I pursue the Philistines? Will you deliver them into the hands of Israel?” And he did not respond to him on that day.
Sauli alitaka kumuuliza Mungu maswali zaidi, “Je, inanipasa kuwafukuza Wafilisti? Je, utawaweka katika mkono wa Israeli?” Lakini siku hiyo BWANA hakumjibu kitu.
38 And Saul said: “Bring here every single leader of the people. And we shall know and see by whom this sin was committed this day.
Ndipo Sauli akasema, “Njoni hapa, viongozi wote wa watu; mjue na kuona jinsi dhambi hii ilivyotokea leo.
39 As the Lord lives, who is the Savior of Israel, even if it were done by my son Jonathan, without retraction he shall die.” In this, no one among all the people contradicted him.
Kwa maana, kama BWANA aishivyo, aliyewaokoa Israeli, hata kama angekuwa mwanangu Yonathani, atapaswa kufa.” Lakini hakuna hata mtu mmoja miongoni mwa watu aliye mjibu neno.
40 And he said to all of Israel, “Separate yourselves on one side, and I, with my son Jonathan, will be on the other side.” And the people responded to Saul, “Do what seems good in your eyes.”
Basi akawaambia Waisraeli wote, “Simameni upande mmoja, na mimi na Yonathani tutasimama upande mwingine.” Kisha watu wakamwambia Sauli, “Fanya lile unaloona jema kwako.”
41 And Saul said to the Lord, the God of Israel: “O Lord, God of Israel, grant a sign: Why is it that you will not respond to your servant this day? If this iniquity is in me, or in my son Jonathan, grant an indication. Or if this iniquity is in your people, grant a sanctification.” And Jonathan and Saul were discovered, but the people were released.
Kwa hiyo, Sauli akamwambia BWANA, Mungu wa Israeli, “Tuoneshe Thumimu.” Yonathani na Sauli wakatwaliwa, lakini watu walinusurika kuchaguliwa.
42 And Saul said, “Cast lots between myself and Jonathan, my son.” And Jonathan was caught.
Basi Sauli akasema, “Tupa mawe ya bahati nasibu tuone kati yangu na mwanangu Yonathani.” Ndipo Yonathani akatwaliwa.
43 Then Saul said to Jonathan, “Tell me what you have done.” And Jonathan revealed to him, and said: “Truly, I tasted a little honey with the top of the staff that was in my hand. And behold, I shall die.”
Kisha Sauli akamwambia Yonathani, “Niambie umefanya nini.” Yonathani akamwambia baba yake, “Nilionja asali kidogo kwa kutumia ncha ya fimbo iliyokuwa mkononi mwangu. Niko hapa; Nitakufa.”
44 And Saul said, “May God do these things to me, and may he add these other things, for you shall surely die, Jonathan!”
Sauli akasema, “Mungu afanye hivyo na kuzidi hata kwangu, kama Yonathani hautakufa.”
45 And the people said to Saul: “Why should Jonathan have to die, who has accomplished this great salvation in Israel? This is wrong. As the Lord lives, not one hair of his head should fall to the ground. For he has wrought with God this day.” Therefore, the people freed Jonathan, so that he would not die.
Basi watu wakamuuliza Sauli, “Je, inampasa Sauli afe, ni nani aliyetekeleza ushindi huu mkubwa kwa ajili ya Israeli? Mbali na hayo! Kama BWANA aishivyo, hata unywele mmoja wa kichwa chake hautaanguka chini, kwa maana leo amefanya kazi pamoja na Mungu.” Hivyo hao watu walimuokoa Yonathani ili asife.
46 And Saul withdrew, and he did not pursue the Philistines. And the Philistines went away to their own places.
Basi Sauli akasita kuwafuatia Wafilisti, nao wakarudi katika makao yao.
47 And Saul, his kingdom having been confirmed over Israel, was fighting against all his enemies on all sides: against Moab, and the sons of Ammon, and Edom, and the kings of Zobah, and the Philistines. And wherever he turned himself, he was successful.
Sauli alipoanza kutawala juu ya Israeli, alipigana na adui zake wote kila upande. Alipigana dhidi ya Moabu, dhidi ya watu wa Amoni, Edomu, wafalme wa Zoba, na Wafilisti. Popote alipogeukia aliwapiga kwa adhabu adui zake.
48 And gathering together an army, he struck Amalek. And he rescued Israel from the hand of those who would lay waste to them.
Alitenda kwa ushujaa mkubwa na kuwashinda Waamaleki. Aliwaokoa Israeli kutoka mikono ya watu ambao waliwateka nyara.
49 Now the sons of Saul were Jonathan, and Ishvi, and Malchishua. And as for the names of his two daughters: the name of the firstborn daughter was Merab, and the name of the younger one was Michal.
Basi wana wa Sauli walikuwa ni hawa Yonathani, Ishvi, na Malkishua. Na majina ya binti zake wawili yalikuwa ni haya, Merabu mzaliwa wa kwanza, na mdogo aliitwa Mikali.
50 And the name of the wife of Saul was Ahinoam, the daughter of Ahimaaz. And the name of the first ruler of his military was Abner, the son of Ner, the first cousin of Saul.
Jina la mke wa Sauli aliitwa Ahinoamu; naye alikuwa binti Ahimaasi. Na jina la Jemedari wa jeshi lake aliitwa Abneri mwana wa Neri, baba mdogo wa Sauli.
51 For Kish was the father of Saul, and Ner was the father of Abner, and the son of Abiel.
Kishi alikuwa baba yake Sauli; na Neri alikuwa baba yake na Abneri, wote walikuwa wana wa Abieli.
52 Now there was a powerful war against the Philistines during all the days of Saul. And so, whomever Saul had seen to be a strong man, and fit for battle, he joined him to himself.
Kulikuwa na mapigano makali dhidi ya Wafilisti katika siku zote za Sauli. Naye alipomwona mtu yeyote mwenye nguvu, au mtu yeyote jasiri, alimuunganisha kwake.

< 1 Samuel 14 >