< 1 Samuel 13 >

1 When he began to reign, Saul was the son of one year, and he reigned over Israel for two years.
Sauli alikwa na umri wa miaka [thelathini] alipoanza kutawala; alipokuwa ametawala Israeli kwa miaka [arobaini],
2 And Saul chose for himself three thousand men of Israel. And two thousand were with Saul at Michmash and at mount Bethel. Then one thousand were with Jonathan at Gibeah of Benjamin. But the remainder of the people, he sent back, each one to his own tent.
aliwachagua wanaume elfu tatu wa Israeli. Elfu mbili walikuwa pamoja naye huko Mikmashi na katika nchi ya milima ya Betheli, wakati huo wale elfu moja walikuwa pamoja na Yonathani katika Gibea ya Benyamini. Askari waliobaki aliwarudisha nyumbani, kila mtu hemani kwake.
3 And Jonathan struck the garrison of the Philistines, which was in Gibeah. And when the Philistines had heard about it, Saul sounded the trumpet over all the land, saying, “Let the Hebrews listen.”
Yonathani akaishinda ngome ya jeshi la Wafilisti iliyokuwa Geba na Wafilisti wakasikia habari hiyo. Baadaye Sauli alipiga tarumbeta katika nchi yote, akisema, “Sikieni enyi Waebrania.”
4 And all of Israel heard this report, that Saul had struck the garrison of the Philistines. And Israel raised himself up against the Philistines. Then the people cried out to Saul at Gilgal.
Israeli yote imesikia kwamba Sauli ameipiga ngome ya Wafilisti, na pia kwamba Israeli imekuwa uvundo kwa Wafilisti. Ndipo askari wakaitwa kwa pamoja kuungana na Sauli huko Gilgali.
5 And the Philistines gathered to do battle against Israel, thirty thousand chariots, and six thousand horsemen, and the remainder of the common people, who were very many, like the sand that is on the shore of the sea. And ascending, they encamped at Michmash, toward the east of Bethaven.
Wafilisti walijikusanya pamoja kupigana dhidi ya Waisraeli: magari elfu tatu, watu elfu sita wakuendesha magari, na majeshi mengi kama mchanga ufukoni mwa bahari. Wakapanda na kupiga kambi huko Mikimashi, mashariki mwa Beth aveni.
6 And when the men of Israel had seen themselves to be in a narrowed position, they hid themselves in caves, and in out of the way places, and in rocks, and in hollows, and in pits (for the people were distressed).
Watu wa Israeli walipoona kuwa wapo katika matatizo -kwa maana watu walikata tamaa, wakajificha kwenye mapango, kwenye vichaka, kwenye miamba, kwenye visima na katika mashimo.
7 Then some of the Hebrews crossed over the Jordan, into the land of Gad and Gilead. And while Saul was still at Gilgal, the entire people who followed him were terrified.
Baadhi ya Waebrania walipanda kwenda Yordani katika nchi ya Gadi na Gileadi. Lakini Sauli alibaki Gilgali, na watu waliomfuata wakitetemeka.
8 But he waited for seven days, in accord with what was agreed with Samuel. But Samuel did not arrive at Gilgal, for the people were scattering away from him.
Alisubiri kwa siku saba, muda uliopangwa na Samweli. Lakini Samweli hakufika huko Gilgali, na watu wakatawanyika mbali na Sauli.
9 Therefore, Saul said, “Bring me the holocaust and the peace offerings.” And he offered the holocaust.
Sauli akasema, “Nileteeni sadaka ya kuteketezwa na sdaka ya amani.” Kisha akatoa sadaka ya kuteketezwa.
10 And when he had completed the offering of the holocaust, behold, Samuel arrived. And Saul went out to meet him, so that he might greet him.
Mara tu alipomaliza kutoa sadaka ya kuteketezwa Samweli akawasili. Sauli akatoka nje wakutane na kumsalimia.
11 And Samuel said to him, “What have you done?” Saul responded: “Since I saw that the people were scattering away from me, and you had not arrived after the agreed upon days, and yet the Philistines had gathered together at Michmash,
Basi Samweli akasema, “Umefanya nini?” Sauli akajibu, “Nilipoona kwamba watu wanaiacha, na kwamba umechelewa hukufika kwa muda uliopangwa, na kwamba Wafilisti wamekwisha jikusanya huko Mikmashi,
12 I said: ‘Now the Philistines will descend to me at Gilgal. And I have not appeased the face of the Lord.’ Compelled by necessity, I offered the holocaust.
nikasema, 'Sasa Wafilisti watashuka dhidi yangu huko Gilgali, na sijaomba kibali cha BWANA.' Kwa hiyo nikajilazimisha mwenyewe kutoa sadaka ya kuteketezwa.”.
13 And Samuel said to Saul: “You have acted foolishly. You have not kept the commandments of the Lord your God, which he instructed to you. And if you had not acted in this way, the Lord would, here and now, have prepared your kingdom over Israel forever.
Ndipo Samweli akamwambia Sauli, “Umetenda mambo ya kipumbavu. Hukuheshimu amri ya BWANA Mungu wako aliyokupatia. Kwa maana BWANA angeutengeneza utawala wako juu ya Israeli milele.
14 But by no means shall your kingdom rise up any more. The Lord has sought for himself a man according to his own heart. And him the Lord has instructed to be the leader over his people, because you have not kept what the Lord has instructed.”
Lakini sasa utawala wako hautaendelea. BWANA ametafuta mtu anayekubaliwa na moyo wake, kwa sababu wewe hukutii alichokuamuru.”
15 Then Samuel rose up and ascended from Gilgal to Gibeah of Benjamin. And the remainder of the people ascended after Saul, to meet the people who were fighting against them, going from Gilgal into Gibeah, to the hill of Benjamin. And Saul took a census of the people, who had been found to be with him, about six hundred men.
Ndipo Samweli akasimama akapanda kutoka Gilgali hadi Gibea ya Benyamini. Basi Sauli akawahesabu watu waliokuwapo pamoja naye, idadi yao ilikuwa kama watu mia sita.
16 And Saul, and his son Jonathan, and the people who had been found to be with them, were at Gibeah of Benjamin. But the Philistines had settled in at Michmash.
Sauli, mtoto wake Yonathani, na watu waliokuwa pamoja nao, wakabaki Geba ya Benyamimni. Lakini Wafilisti wakapiga kambi huko Mikmashi.
17 And three companies went out from the camp of the Philistines, in order to plunder. One company was traveling toward the way of Ophrah, to the land of Shual.
Wateka nyara makundi matatu wakaja kutoka kambi ya Wafilisti. Kundi moja likapinda kuelekea Ofra, hadi nchi ya Shuali.
18 Then another entered along the way of Beth-horon. But the third turned itself to the way of the border, overhanging the valley of Zeboim, opposite the desert.
Kundi jingine likageuka kuelekea Bethholoni, na kundi jingine likaelekea katika mpaka kulikabili bonde la Seboimu kuelekea jangwani.
19 Now there was no worker of iron to be found in all the land of Israel. For the Philistines had been cautious, lest perhaps the Hebrews might make swords or spears.
Hakuna hata mhunzi aliyeonekana katika nchi yote ya Israeli, kwa sababu Wafilisti walisema, “Waebrania wasije wakajitengenezea mapanga au mikuki.”
20 Therefore, all of Israel descended to the Philistines, so that each man could sharpen his plowshare, or pick axe, or hatchet, or hoe.
Lakini Waisraeli wote huwa wakiteremka kwa Wafilisti, kila mtu kunoa jembe lake, sululu yake, shoka lake na mundu wake.
21 For their plow blades, and pick axes, and pitch forks, and axes had become blunt, and even the handles needed to be repaired.
Gharama za kunoa ncha za majembe, sululu, mashoka na kunyoosha michokoo ilikuwa theluthi moja ya shekeli.
22 And when the day of battle had arrived, there was found neither sword nor spear in the hand of the entire people who were with Saul and Jonathan, except for Saul and his son Jonathan.
Hivyo siku ya vita, hakukuwa na mapanga au mikuki iliyoonekana katika mikono yoyote ya askali waliokuwa na Sauli na Yonathani; Ni Sauli na mtoto wake tu ndio walikuwa nazo.
23 Then the army of the Philistines went out in order to go across Michmash.
Vikosi vya Wafilisti wakatokeza katika nija ya Mikmashi.

< 1 Samuel 13 >