< 1 Chronicles 24 >

1 Now these were the divisions of the sons of Aaron. The sons of Aaron: Nadab, and Abihu, and Eleazar, and Ithamar.
Makundi vya kazi kulingana na uzao wa Aroni yalikuwa haya: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari.
2 But Nadab and Abihu died before their father, and without children. And so Eleazar and Ithamar exercised the priestly office.
Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao kufa. Walikuwa hawana watoto, kwahiyo Eleazari na Ithamari walitumika kama makuhani.
3 And David distributed them, that is, Zadok of the sons of Eleazar, and Ahimelech of the sons of Ithamar, according to their courses and ministry.
Daudi pamoja na Zadoki, uzao wa Eleazari, na Ahimeleki, uzao wa Ithamari, waliwagawanya katika makundi yao ya kazi kama makuhani.
4 And there were found many more of the sons of Eleazar among the leading men, than of the sons of Ithamar. Therefore, he divided them so that there were, of the sons of Eleazar, sixteen leaders by their families, and of the sons of Ithamar eight by their families and houses.
Kulikuwa na wanaume viongozi zaidi kati ya uzao wa Eleazari kuliko kati ya uzao wa Ithamari, kwahiyo waligawanya uzao wa Eleazari katika makundi kumi na sita. Walifanya hivyo na viongozi wa ukoo na uzao wa Ithamari. Magawanyo haya yalikuwa nane kwa idadi, sambamba na koo zao.
5 Then he divided among them, in both families, by lot. For there were leaders of the sanctuary and leaders of God, as much from the sons of Eleazar as from the sons of Ithamar.
Waliwagawanya bila upendeleo kwa kura, kwa kuwa walikuwa waamuzi watakatifu na waamuzi wa Mungu, kutoka pande zote uzao wa Eleazari na uzao wa Ithamari.
6 And the scribe Shemaiah, the son of Nethanel, a Levite, wrote these down before the king and the leaders, with Zadok, the priest, and Ahimelech, the son of Abiathar, and also the leaders of the priestly and Levitical families. And there was one house, which was preeminent over the others, that of Eleazar; and there was another house, which had the others under it, that of Ithamar.
Shemaia mwana wa Nethaneli mwandishi, Mlawi, aliandika majina yao mbele ya mfalme, muamuzi, kuhani Zadoki, Ahimeleki mwana wa Abiathari, na viongozi wa makuhani na familia za Walawi. Ukoo mmoja ulichaguliwa kwa kura kutoka uzao wa Eleazari, na kisha uliofata utachaguliwa kutoka uzao wa Ithhamari.
7 Now the first lot went forth to Jehoiarib, the second to Jedaiah,
Kura ya kwanza ilienda kwa Yehoiaribu, ya pili kwa Yedaia,
8 the third to Harim, the fourth to Seorim,
ya tatu kwa Harimu, ya nne kwa Seorimu,
9 the fifth to Malchijah, the sixth to Mijamin,
ya tano kwa Malikija, ya sita kwa Mijamini,
10 the seventh to Hakkoz, the eighth to Abijah,
ya saba kwa Hakozi, ya nane kwa Abija,
11 the ninth to Jeshua, the tenth to Shecaniah,
ya tisa kwa Yeshua, ya kumi kwa Shekania,
12 the eleventh to Eliashib, the twelfth to Jakim,
ya kumi na moja kwa Eliashibu, ya kumi na mbili kwa Yakimu,
13 the thirteenth to Huppah, the fourteenth to Jeshebeab,
ya kumi na tatu kwa Hupa, ya kumi na nne kwa Yesheheabu,
14 the fifteenth to Bilgah, the sixteenth to Immer,
ya kumi na tano kwa Biliga, ya kumi na sita kwa Imma,
15 the seventeenth to Hezir, the eighteenth to Happizzez,
ya kumi na saba kwa Heziri, ya kumi na nane kwa Hapizezi,
16 the nineteenth to Pethahiah, the twentieth to Jehezkel,
ya kumi na tisa kwa Pethaia, ya ishirini kwa Yehezikeli,
17 the twenty-first to Jachin, the twenty-second to Gamul,
ya ishirini na moja kwa Yakini, ya ishirini na mbili kwa Gamuli,
18 the twenty-third to Delaiah, the twenty-fourth to Maaziah.
ya ishirini na tatu kwa Delaia, na ya ishirini na nne kwa Maazia.
19 These were their courses according to their ministries, so that they would enter into the house of the Lord in accord with their practice, under the hand of Aaron, their father, just as the Lord, the God of Israel, had instructed.
Hii ilikuwa taratibu ya utumishi wao, walipo kuja kwenye nyumba ya Yahweh, wakifuata utaratibu waliopewa na Aruni babu yao, kama Yahweh, Mungu wa Israeli, alivyo waagiza.
20 Now of the sons of Levi who were remaining, there were Shubael, from the sons of Amram, and Jehdeiah, from the sons of Shubael.
Hawa walikuwa Walawi waliobakia: Wana wa Amiramu, Shebueli; wana wa Shebaeli, Yedeia.
21 Also, there were Isshiah, the leader from the sons of Rehabiah,
Wana wa Rehabia: wana wa Rehabia, Ishia kiongozi.
22 and truly Shelomoth, the son of Izhar, and Jahath, the son of Shelomoth,
Wa Waizari, Shelomothi; mwana wa Shelomothi, Yahathi.
23 and his son, Jeriah the first, Amariah the second, Jahaziel the third, Jekameam the fourth.
Wana wa Hebroni: Yeria kiongozi, Amaria wapili, Yahazieli watatu, na Yekameamu wanne.
24 The son of Uzziel was Micah. The son of Micah was Shamir.
Wana wa uzao wa Uzieli ulimjumuisha Mika. Uzao wa Mika ulimjumuisha Shamiri.
25 The brother of Micah was Isshiah. And the son of Isshiah was Zechariah.
Kaka wa Mika alikuwa Ishia. Wana wa Ishia akijumuishwa Zakaria.
26 The sons of Merari were Mahli and Mushi. The son of Uzziah was Beno.
Wana na Merari: Mahli na Mushi. Mwana wa Yaazia, Beno.
27 Also, the son of Merari: Uzziah, and Shoham, and Zaccur, and Hebri.
Wana wa Merari: Yaazia, Beno, Shohamu, Zakuri, na Ibrri.
28 In addition, the son of Mahli was Eleazar, who had no children.
Wana wa Mahili: eleazari, ambaye alikuwa hana wana.
29 Truly, the son of Kish was Jerahmeel.
Wana wa Kishi: Yerameli
30 The sons of Mushi were Mahli, Eder, and Jerimoth. These were the sons of Levi according to the houses of their families.
wana wa Mushi: Mahli, Eda, na yerimothi. Walikuwa walawi, walio orodheshwa na familia zao.
31 And they also cast lots concerning their brothers, the sons of Aaron, before David the king, and Zadok, and Ahimelech, and the leaders of the priestly and Levitical families, as much concerning the elder as the younger. The lot divided all things equitably.
Wanaume hawa ambao walikuwa vichwa katika nyumba za baba zao na kila wadogo zao, walipiga kura katika uwepo wa Mfalme Daudi, na Zadoki na Ahimeleki, pamoja na viongozi wa familia wa makuhani na Walawi. Walirusha kura kama uzao wa Aroni walivyofanya.

< 1 Chronicles 24 >