< 2 Chronicles 1 >

1 Then Solomon, the son of David, was strengthened in his reign, and the Lord his God was with him, and he magnified him on high.
Selemani mwana wa Daudi, aliimariswa katika utawala wake, na Yahwe Mungu wake alikuwa pamoja naye na alimpa nguvu nyingi sana.
2 And Solomon instructed the whole of Israel, the tribunes, and the centurions, and the rulers, and the judges over all of Israel, and the leaders of the families.
Sulemani akasema kwa Israleli wote, na maakida wa maelfu na wa mamia, na kwa waamuzi, na kwa kila mfalme kiongozi katika Israeli yote, wakuu wa kaya.
3 And he went away with the entire multitude to the high place of Gibeon, where the tabernacle of the covenant of the Lord was, which Moses, the servant of God, made in the wilderness.
Hivyo Sulemani na kusanyiko lote wakaenda pamoja naye sehemu ya juu iliyokuwa Gibeoni, maana ndipo palikuwepo hema ya kukutania ya Mungu, ambayo Musa mtumishi wa Yahwe, alikuwa ameitengeneza jangwani.
4 For David had brought the ark of God from Kiriath-jearim, to the place that he had prepared for it, and where he had pitched a tabernacle for it, that is, in Jerusalem.
Lakini Daudi alikuwa ameleta pale sanduku la Mungu kutoka Kiriath yeriam hadi sehemu ambayo alikuwa ametayarisha, maana alikuwa ameliandalia hema huko katika Yerusalemu.
5 Also, the altar of brass, which Bezalel, the son of Uri, the son of Hur, had constructed, was there before the tabernacle of the Lord. And so Solomon sought it, with the entire assembly.
Zaidi ya hayo, madhabahu ya shaba iliyotengenezwa na Bezaleli mwana wa uri mwana wa Huri ilikuwepo huko kabla ya mbele ya madhabahu ya Yahwe; Sulemani na kusanyiko wakaenda ilikokuwa. (Maandiko ya zamani yanasema
6 And Solomon ascended to the bronze altar, before the tabernacle of the covenant of the Lord, and he offered upon it one thousand victims.
Selemani akaenda huko kwenye kwenye madhabahu ya shaba mbele za Yahwe, ambayo ilikuwepo mahali pa hema ya kukutamia, na akatoa sadaka elfu za kuteketezwa juu yake.
7 But behold, during that night God appeared to him, saying, “Request what you wish, so that I may give it to you.”
Mungu akamtokea Selemani usiku huo na akasema kwake, “Omba! Nikupe nini?”
8 And Solomon said to God: “You have shown great mercy to my father David. And you have appointed me as king in his place.
Selemani akasema kwa Mungu, “Umeonesha agano la uaminifu mkuu kwa Daudi baba yangu, na umenifanya mfalme katika nafasi yaye.
9 Now therefore, O Lord God, let your word be fulfilled, which you promised to my father David. For you have made me king over your great people, who are as innumerable as the dust of the earth.
Sasa, Yahwe Mungu, ahadi yako kwa Daudi baba yangu itimie, maana umenifanya mfalme juu ya watu wengi kama mavumbi ya dunia.
10 Give to me wisdom and understanding, so that I may enter and depart before your people. For who is able worthily to judge this, your people, who are so great?”
Sasa nipe hekima na maarifa, ili niweze kuwaongoza watu hawa, maana ni nani anayeweza kuwaamua watu wako, ambao ni wengi sana kwa idadi?”
11 Then God said to Solomon: “Since this is the choice that pleased your heart, and you did not request wealth and substance and glory, nor the lives of those who hate you, nor even many days of life, since instead you requested wisdom and knowledge so that you may be able to judge my people, over whom I have appointed you as king:
Mungu akasema kwa Selemani, “Kwa kuwa hili lilikuwa kwenye moyo wako, na kwa kuwa hujaomba mali, utajiri, au heshima, wala maisha ya wale wanaokuchukia, wala maish marefu kwa jili yako binafsi, lakini umeomba hekima na maarifa kwa ajili yako, ili uwatawale watu wangu, ambao juu yao nimekufanya mfame, na hivi ndivyo nitafanya.
12 wisdom and knowledge are granted to you. And I will give to you wealth and substance and glory, so that none of the kings either before you or after you will be similar to you.”
Sasa nitakupa hekima na maarifa, pia nitakupa mali na utajiri, na heshima, kuliko wafalme wote waliokuwepo kabla yako walivyokuwa, na baada yako hakuna yeyote atakayekuwa navyo.”
13 Then Solomon went from the high place of Gibeon to Jerusalem, before the tabernacle of the covenant, and he reigned over Israel.
Kwa hiyo Selemani akaenda Yerusalemu kutoka sehemu ya juu iliyokuwepo Gibeoni, kutoka mbele ya hema ya kukutania; akatawala juu ya Israeli.
14 And he gathered to himself chariots and horsemen. And they brought to him one thousand four hundred chariots, and twelve thousand horsemen. And he caused them to be in the cities of the chariots, and with the king in Jerusalem.
Selemani akakusanya magari na wanaume waendesha farasi, naye alikuwa na magari 1, 400 na waendesha farasi kumi na mbili elfu ambao aliwaweka katika miji ya magari, pamoja naye, mfalme katika Yerusalemu.
15 And the king offered silver and gold in Jerusalem as if they were stones, and cedar trees as if they were sycamores, which grow in the plains in a great multitude.
Mfalme akatengeneza fedha na dhahabu kuwa vitu vya kawaida kama mawe katika Yerusalemu, na mbao za mierezi kuwa kama miti ya mikuyu iliyomo katika nyanda za chini.
16 Then horses were brought to him from Egypt and from Kue, by the negotiators of the king, who went and bought for a price:
Selemani katika uagizaji wa farasi kutoka Misiri, wafanya biashara wake walinunua farasi kutoka Misiri kwa bei stahiki.
17 a four-horse chariot for six hundred pieces of silver, and a horse for one hundred fifty. A similar offer to purchase was made known among all the kingdoms of the Hittites, and among the kings of Syria.
Waliagiza gari kutoka Misiri kwa shekeli mia sita za fedha, na farasi mmoja kwa shekeli 150. Pia walinunua kutoka kwa wafalme wa Wahiti na wafalme wa Washamu.

< 2 Chronicles 1 >