< Luke 21 >

1 Then Jesus looked up and saw the rich putting their gifts into the treasury,
Yesu alitazama akawaona wanaume matajiri waliokuwa wanaweka zawadi zao kwenye hazina.
2 and He saw a poor widow put in two small copper coins.
Akamuona mjane mmoja masikini akiweka senti zake mbili.
3 “Truly I tell you,” He said, “this poor widow has put in more than all the others.
Hivyo akasema, “Kweli nawaambieni, huyu Mjane maskini ameweka nyingi kuliko wengine wote.
4 For they all contributed out of their surplus, but she out of her poverty has put in all she had to live on.”
Hawa wote wametoa hizi zawadi kutoka katika vingi walivyonavyo. Lakini huyu mjane, katika umaskini wake, ametoa fedha zote alizokuwa nazo kwa ajili ya kuishi kwake.”
5 As some of the disciples were remarking how the temple was adorned with beautiful stones and consecrated gifts, Jesus said,
Wakati wengine walipokuwa wakisema juu ya hekalu, namna lilivyokuwa limepambwa na mawe mazuri na matoleo, alisema,
6 “As for what you see here, the time will come when not one stone will be left on another; every one will be thrown down.”
“Kwa habari ya mambo haya mnayoyaona, siku zitakuja ambazo hakuna jiwe moja ambalo litaachwa juu ya jiwe jingine ambalo halitabomolewa.”
7 “Teacher,” they asked, “when will these things happen? And what will be the sign that they are about to take place?”
Hivyo wakamuuliza, wakasema, “Mwalimu, mambo haya yatatokea lini? Na nini ni itakuwa ishara kwamba haya mambo yako karibu kutokea?”
8 Jesus answered, “See to it that you are not deceived. For many will come in My name, claiming, ‘I am He,’ and, ‘The time is near.’ Do not follow them.
Yesu akajibu, “Muwe waangalifu kwamba msidanganywe. Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, 'Mimi ndiye, 'na 'Muda umekaribia'. Msiwafuate.
9 When you hear of wars and rebellions, do not be alarmed. These things must happen first, but the end is not imminent.”
Mkisikia vita na vuruguvurugu msiogope, kwa sababu haya mambo lazima yatokee kwanza, lakini mwisho hautatokea upesi.”
10 Then He told them, “Nation will rise against nation, and kingdom against kingdom.
Kisha akawaambia, “Taifa litainuka kupigana na taifa jingine, na ufalme juu ya ufalme mwingine.
11 There will be great earthquakes, famines, and pestilences in various places, along with fearful sights and great signs from heaven.
Kutakuwa na matetemeko makubwa, na njaa na tauni katika maeneo mbalimbali. Kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara za kutisha kutoka mbinguni.
12 But before all this, they will seize you and persecute you. On account of My name they will deliver you to the synagogues and prisons, and they will bring you before kings and governors.
Lakini kabla ya mambo haya yote, wataweka mikono yao juu yenu na kuwatesa, kuwapeleka kwenye masinagogi na magereza, kuwaleta mbele za wafalme na wenye mamlaka kwa sababu ya jina langu.
13 This will be your opportunity to serve as witnesses.
Hii itawafungulia fursa kwa ushuhuda wenu.
14 So make up your mind not to worry beforehand how to defend yourselves.
Kwahiyo amueni mioyoni mwenu kutoandaa utetezi wenu mapema,
15 For I will give you speech and wisdom that none of your adversaries will be able to resist or contradict.
kwa sababu nitawapa maneno na hekima, ambayo adui zenu wote hawataweza kuipinga au kuikana.
16 You will be betrayed even by parents and brothers and relatives and friends, and some of you will be put to death.
Lakini mtakataliwa pia na wazazi wenu, ndugu zenu, jamaa zenu na rafiki zenu, na watawaua baadhi yenu.
17 And you will be hated by everyone because of My name.
Mtachukiwa na kila mmoja kwa sababu ya jina langu.
18 Yet not even a hair of your head will perish.
Lakini hakuna hata unywele mmoja wa vichwa vyenu utakaopotea.
19 By your patient endurance you will gain your souls.
Katika kuvumilia mtaziponya nafsi zenu.
20 But when you see Jerusalem surrounded by armies, you will know that her desolation is near.
Mtakapoona Yerusalemu imezungukwa na majeshi, basi jueni kwamba uharibifu wake umekaribia.
21 Then let those who are in Judea flee to the mountains, let those in the city get out, and let those in the country stay out of the city.
Hapo wale walioko Yudea wakimbilie milimani, na wale walioko katikati ya jiji waondoke, na msiwaache walioko vijijini kuingia.
22 For these are the days of vengeance, to fulfill all that is written.
Maana hizi ni siku za kisasi, ili kwamba mambo yote yaliyoandikwa yapate kutimilika.
23 How miserable those days will be for pregnant and nursing mothers! For there will be great distress upon the land and wrath against this people.
Ole ni kwa wale walio na mimba na kwa wale wanyonyeshao katika siku hizo! Kwa maana kutakuwa na adha kuu juu ya nchi, na ghadhabu kwa watu hawa.
24 They will fall by the edge of the sword and be led captive into all the nations. And Jerusalem will be trodden down by the Gentiles, until the times of the Gentiles are fulfilled.
Na wataanguka kwa ncha ya upanga na watachukuliwa mateka kwa mataifa yote, na Yerusalem itakanyagwa na watu wa mataifa, mpaka wakati wa watu wa mataifa utakapotimilika.
25 There will be signs in the sun and moon and stars, and on the earth dismay among the nations, bewildered by the roaring of the sea and the surging of the waves.
Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Na katika nchi kutakuwa na dhiki ya mataifa, katika kukata tamaa kutokana na mlio wa bahari na mawimbi.
26 Men will faint from fear and anxiety over what is coming upon the earth, for the powers of the heavens will be shaken.
Kutakuwa na watu wakizimia kwa hofu na katika kutarajia mambo yatakoyo tokea juu ya dunia. Kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
27 At that time they will see the Son of Man coming in a cloud with power and great glory.
Kisha watamwona Mwana wa Adamu akija mawinguni katika nguvu na utukufu mkuu.
28 When these things begin to happen, stand up and lift up your heads, because your redemption is drawing near.”
Lakini mambo haya yatakapoanza kutokea, simameni, inueni vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umesogea karibu.”
29 Then Jesus told them a parable: “Look at the fig tree and all the trees.
Yesu akawaambia kwa mfano, “Uangalieni mtini, na miti yote.
30 When they sprout leaves, you can see for yourselves and know that summer is near.
Inapotoa machipukizi, mnajionea wenyewe na kutambua kwamba kiangazi tayari kiko karibu.
31 So also, when you see these things happening, know that the kingdom of God is near.
Vivyo hivyo, mnapoona mambo haya yanatokea, ninyi tambueni ya kwamba ufalme wa Mungu umekaribia.
32 Truly I tell you, this generation will not pass away until all these things have happened.
Kweli, nawaambieni, kizazi hiki hakitapita, mpaka mambo haya yote yatakapotokea.
33 Heaven and earth will pass away, but My words will never pass away.
Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
34 But watch yourselves, or your hearts will be weighed down by dissipation, drunkenness, and the worries of life—and that day will spring upon you suddenly like a snare.
Lakini jiangalieni wenyewe, ili kwamba mioyo yenu isije ikalemewa na ufisadi, ulevi, na mahangaiko ya maisha haya. Kwa sababu ile siku itawajia ghafla
35 For it will come upon all who dwell on the face of all the earth.
kama mtego. Kwasababu itakuwa juu ya kila mmoja aishiye katika uso wa dunia nzima.
36 So keep watch at all times, and pray that you may have the strength to escape all that is about to happen and to stand before the Son of Man.”
Lakini mwe tayari wakati wote, mwombe kwamba mtakuwa imara vya kutosha kuyaepuka haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu.”
37 Every day Jesus taught at the temple, but every evening He went out to spend the night on the Mount of Olives.
Hivyo wakati wa mchana alikuwa akifundisha hekaluni na usiku alitoka nje, na kwenda kukesha katika mlima unaoitwa wa Mzeituni.
38 And early in the morning all the people would come to hear Him at the temple.
Watu wote walimjia asubuhi na mapemaili kumsikiliza ndani ya hekalu.

< Luke 21 >