< Romans 5 >
1 Therefore having been made righteous from faith, we have peace toward God through our Lord Jesus Christ,
Kwa hiyo, kwa kuwa tumekwisha kuhesabiwa haki kwa imani, tuna amani na Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,
2 through whom also we have access by faith for this grace in which we stand, and we take pride in hope of the glory of God.
ambaye kwa kupitia kwake tumepata kwa njia ya imani kuifikia neema hii ambayo ndani yake sasa tunasimama, nasi twafurahia katika tumaini letu la kushiriki utukufu wa Mungu.
3 And not only so, but we also take pride in our tribulations, knowing that tribulation produces perseverance,
Si hivyo tu, bali twafurahi pia katika mateso, kwa sababu tunajua kuwa mateso huleta saburi,
4 and perseverance, character, and character, hope.
nayo saburi huleta uthabiti wa moyo, na uthabiti wa moyo huleta tumaini,
5 And hope does not disappoint, because the love of God has been poured out in our hearts through the Holy Spirit that was given to us.
wala tumaini halitukatishi tamaa, kwa sababu Mungu amekwisha kumimina pendo lake mioyoni mwetu kwa njia ya Roho Mtakatifu ambaye ametupatia.
6 For while we were yet weak, in due time Christ died for the impious.
Kwa maana hata tulipokuwa dhaifu, wakati ulipowadia, Kristo alikufa kwa ajili yetu sisi wenye dhambi.
7 For scarcely for a righteous man will some man die, indeed perhaps for the good man some man would even dare to die.
Hakika, ni vigumu mtu yeyote kufa kwa ajili ya mwenye haki, ingawa inawezekana mtu akathubutu kufa kwa ajili ya mtu mwema.
8 But God commends his love toward us, that, while we were still sinners, Christ died for us.
Lakini Mungu anaudhihirisha upendo wake kwetu kwamba: Tulipokuwa tungali wenye dhambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu.
9 Much more then, now having been made righteous by his blood, we will be saved from the wrath through him.
Basi, kwa kuwa sasa tumehesabiwa haki kwa damu yake, si zaidi sana tutaokolewa kutoka ghadhabu ya Mungu kupitia kwake!
10 For if, while being enemies, we were reconciled to God through the death of his Son, much more having been reconciled we will be saved by his life.
Kwa kuwa kama tulipokuwa adui wa Mungu tulipatanishwa naye kwa njia ya kifo cha Mwanawe, si zaidi sana tukiisha kupatanishwa, tutaokolewa kwa uzima wake.
11 And not only so, but also taking pride in God through our Lord Jesus Christ, through whom we have now received the reconciliation.
Lakini zaidi ya hayo, pia tunafurahi katika Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye kupitia kwake tumepata upatanisho.
12 Because of this, just as through one man sin entered into the world, and death through sin, so also death passed to all men, in that all sinned.
Kwa hiyo kama vile dhambi ilivyoingia ulimwenguni kupitia kwa mtu mmoja, na kupitia dhambi hii mauti ikawafikia watu wote, kwa sababu wote wamefanya dhambi:
13 For until law sin was in the world, but sin is not imputed when there is no law.
kwa maana kabla sheria haijatolewa, dhambi ilikuwepo ulimwenguni. Lakini dhambi haihesabiwi wakati hakuna sheria.
14 Nevertheless death reigned from Adam until Moses, even over those who did not sin in the likeness of Adam's transgression, who is a type of the coming man.
Hata hivyo, tangu wakati wa Adamu hadi wakati wa Mose, mauti ilitawala watu wote, hata wale ambao hawakutenda dhambi kwa kuvunja amri, kama alivyofanya Adamu, ambaye alikuwa mfano wa yule atakayekuja.
15 But in this way also, the gift is not as the transgression. For if by the trespass of the one man the many died, much more the grace of God, and the gift in grace of the one man, Jesus Christ, abounded for the many.
Lakini ile karama iliyotolewa haikuwa kama lile kosa. Kwa maana ikiwa watu wengi walikufa kwa sababu ya kosa la mtu mmoja, zaidi sana neema ya Mungu na ile karama iliyokuja kwa neema ya mtu mmoja, yaani, Yesu Kristo, imezidi kuwa nyingi kwa ajili ya wengi.
16 And the gift is not as through one man who sinned, for indeed the judgment from one man was for condemnation, but the gift from many offenses is for righteousness.
Tena, ile karama ya Mungu si kama matokeo ya ile dhambi. Hukumu ilikuja kwa njia ya mtu mmoja, ikaleta adhabu, bali karama ya neema ya Mungu ilikuja kwa njia ya makosa mengi, ikaleta kuhesabiwa haki.
17 For if, by the offense of the one man, death reigned through the one man, much more those who receive the abundance of grace and of the gift of righteousness will reign in life through the one man, Jesus Christ.
Kwa maana ikiwa kutokana na kosa la mtu mmoja, mauti ilitawala kupitia huyo mtu mmoja, zaidi sana wale wanaopokea wingi wa neema ya Mungu na karama yake ya kuhesabiwa haki, watatawala katika uzima kwa njia ya huyo mtu mmoja, yaani, Yesu Kristo.
18 So then, as through an offense of one man was for condemnation for all men, so also through a righteousness of one man was for justification of life for all men.
Kwa hiyo, kama vile kosa la mtu mmoja lilivyoleta adhabu kwa watu wote, vivyo hivyo pia kwa tendo la haki la mtu mmoja lilileta kuhesabiwa haki ambako huleta uzima kwa wote.
19 For as through the one man's disobedience the many were led sinful, so also through the obedience of the one man the many will be led righteous.
Kwa maana kama vile kwa kutokutii kwa yule mtu mmoja wengi walifanywa wenye dhambi, vivyo hivyo kwa kutii kwa mtu mmoja wengi watafanywa wenye haki.
20 And the law entered so that the offense might abound. But where sin abounded, grace was more abundant,
Zaidi ya hayo, sheria ilikuja, ili uvunjaji wa sheria uongezeke. Lakini dhambi ilipoongezeka, neema iliongezeka zaidi,
21 so that, as sin reigned in death, so also grace might reign, through righteousness, for eternal life through Jesus Christ our Lord. (aiōnios )
ili kwamba kama vile dhambi ilivyotawala kwa njia ya mauti, vivyo hivyo neema iweze kutawala kwa njia ya kuhesabiwa haki hata kuleta uzima wa milele katika Yesu Kristo Bwana wetu. (aiōnios )