< Romans 4 >

1 What then will we say Abraham, our father according to flesh, to have found?
Tuseme nini basi, kuhusu Abrahamu baba yetu kwa jinsi ya mwili: yeye alipataje kujua jambo hili?
2 For if Abraham was made righteous from works, he has a boast, but not before God.
Kwa maana ikiwa Abrahamu alihesabiwa haki kwa matendo, basi, anacho kitu cha kujivunia, lakini si mbele za Mungu.
3 For what does the scripture say? And Abraham believed God, and it was reckoned to him for righteousness.
Kwa maana Maandiko yasemaje? “Abrahamu alimwamini Mungu na ikahesabiwa kwake kuwa haki.”
4 Now to the man being employed, the wage is not reckoned according to grace, but according to obligation.
Basi mtu afanyapo kazi, mshahara wake hauhesabiwi kwake kuwa ni zawadi, bali ni haki yake anayostahili.
5 But to the man not being employed, but who believes in him who makes the impious man righteous, his faith is reckoned for righteousness.
Lakini kwa mtu ambaye hafanyi kazi na anamtumaini Mungu, yeye ambaye huwahesabia waovu haki, imani yake inahesabiwa kuwa haki.
6 Just as David also tells the blessedness of the man to whom God imputes righteousness independent of works,
Daudi pia alisema vivyo hivyo aliponena juu ya baraka za mtu ambaye Mungu humhesabia haki pasipo matendo:
7 saying, Blessed are those whose iniquities are forgiven, and whose sins are covered.
“Wamebarikiwa wale ambao wamesamehewa makosa yao, ambao dhambi zao zimefunikwa.
8 Blessed is a man to whom the Lord does, no, not impute sin.
Heri mtu yule Bwana hamhesabii dhambi zake.”
9 Is this blessedness therefore upon men of circumcision, or also upon men of uncircumcision? For we say, Faith was reckoned to Abraham for righteousness.
Je, huku kubarikiwa ni kwa wale waliotahiriwa peke yao, au pia na kwa wale wasiotahiriwa? Tunasema, “Imani ya Abrahamu ilihesabiwa kwake kuwa haki.”
10 How then was it reckoned? When he was in circumcision, or in uncircumcision? Not in circumcision, but in uncircumcision.
Je, ni lini basi ilipohesabiwa kwake kuwa haki? Je, ilikuwa kabla au baada ya kutahiriwa kwake? Haikuwa baada, ila kabla hajatahiriwa.
11 And he received the sign of circumcision, as a seal of the righteousness of his faith during uncircumcision, for him to be father of all those who believe during uncircumcision (for righteousness to also be imputed to them),
Alipewa ishara ya tohara kuwa muhuri wa haki aliyokuwa nayo kwa imani hata alipokuwa bado hajatahiriwa. Kusudi lilikuwa kumfanya baba wa wote wale waaminio pasipo kutahiriwa na ambao wamehesabiwa haki.
12 and father of those of circumcision, to those not only of circumcision, but also to those who march in the steps of faith-of that during the uncircumcision of our father Abraham.
Vivyo hivyo awe baba wa wale waliotahiriwa ambao si kwamba wametahiriwa tu, bali pia wanafuata mfano wa imani ambayo Baba yetu Abrahamu alikuwa nayo kabla ya kutahiriwa.
13 For the promise to Abraham or to his seed, for him to be heir of the world, was not through law, but through a righteousness of faith.
Kwa maana ile ahadi kwamba angeurithi ulimwengu haikuja kwa Abrahamu au kwa wazao wake kwa njia ya sheria bali kwa njia ya haki ipatikanayo kwa imani.
14 For if those from law are heirs, faith has been made void, and the promise has been made useless.
Kwa maana ikiwa wale waishio kwa sheria ndio warithi, imani haina thamani na ahadi haifai kitu,
15 For the law works wrath. For where there is no law, neither is there transgression.
kwa sababu sheria huleta ghadhabu. Mahali ambapo hakuna sheria hakuna makosa.
16 Because of this it is from faith, so that it is according to grace, in order for the promise to be sure to all the seed, not only to the seed from the law, but also to the seed from the faith of Abraham, who is father of us all
Kwa hiyo, ahadi huja kwa njia ya imani, ili iwe ni kwa neema, na itolewe kwa wazao wa Abrahamu, si kwa wale walio wa sheria peke yao, bali pia kwa wale walio wa imani ya Abrahamu. Yeye ndiye baba yetu sisi sote.
17 (as it is written, I have made thee a father of many nations), before him whom he believed, of God who makes the dead alive, and who calls things not existing, as existing.
Kama ilivyoandikwa: “Nimekufanya wewe kuwa baba wa mataifa mengi.” Yeye ni baba yetu mbele za Mungu, ambaye yeye alimwamini, yule Mungu anaye fufua waliokufa, na kuvitaja vile vitu ambavyo haviko kana kwamba vimekwisha kuwako.
18 Who, against hope, believed in hope, in order for him to become father of many nations according to that which was spoken, So thy seed will be.
Akitarajia yasiyoweza kutarajiwa, Abrahamu akaamini, akawa baba wa mataifa mengi, kama alivyoahidiwa kwamba, “Uzao wako utakuwa mwingi mno.”
19 And not being weak in faith he did not regard his body, which was now deadened (being about a hundred years old), and the deadness of Sarah's womb.
Abrahamu hakuwa dhaifu katika imani hata alipofikiri juu ya mwili wake, ambao ulikuwa kama uliokufa, kwani umri wake ulikuwa unakaribia miaka mia moja, au alipofikiri juu ya ufu wa tumbo la Sara.
20 And he did not waver in unbelief at the promise of God, but became strong in faith, giving glory to God,
Lakini Abrahamu hakusitasita kwa kutokuamini ahadi ya Mungu, bali alitiwa nguvu katika imani yake na kumpa Mungu utukufu,
21 and being fully assured that what he promised, he was able also to perform.
akiwa na hakika kabisa kwamba Mungu alikuwa na uwezo wa kutimiza lile aliloahidi.
22 And therefore it was reckoned to him for righteousness.
Hii ndio sababu, “ilihesabiwa kwake kuwa haki.”
23 Now it was not written because of him alone that it was imputed to him,
Maneno haya “ilihesabiwa kwake kuwa haki,” hayakuandikwa kwa ajili yake peke yake,
24 but also because of us to whom it is going to be imputed, to those who believe in him who raised Jesus our Lord from the dead,
bali kwa ajili yetu sisi pia ambao Mungu atatupa haki, sisi tunaomwamini yeye aliyemfufua Yesu Bwana wetu kutoka kwa wafu.
25 who was delivered up for our offenses, and was raised up for our justification.
Alitolewa afe kwa ajili ya dhambi zetu, naye alifufuliwa kutoka mauti ili tuhesabiwe haki.

< Romans 4 >