< Job 6 >
1 Så tog Job til Orde og svarede:
Kisha Ayubu akajibu:
2 "Gid man vejed min Harme og vejed min Ulykke mod den!
“Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa, nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
3 Thi tungere er den end Havets Sand, derfor talte jeg over mig!
Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote, kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
4 Thi i mig sidder den Almægtiges Pile, min Ånd inddrikker deres Gift; Rædsler fra Gud forvirrer mig.
Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
5 Skriger et Vildæsel midt i Græsset, brøler en Okse ved sit Foder?
Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani, au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula?
6 Spiser man ferskt uden Salt, smager mon Æggehvide godt?
Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi, au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
7 Min Sjæl vil ej røre derved, de Ting er som Lugt af en Løve.
Ninakataa kuvigusa; vyakula vya aina hii hunichukiza.
8 Ak, blev mit Ønske dog opfyldt, Gud give mig det, som jeg håber
“Laiti ningepata haja yangu, kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
9 vilde d dog knuse mig, række Hånden ud og skære mig fra,
kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda, kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
10 så vilde det være min Trøst - jeg hopped af Glæde trods skånselsløs Kval at jeg ikke har nægtet den Helliges Ord.
Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
11 Hvad er min Kraft, at jeg skal holde ud, min Udgang, at jeg skal være tålmodig?
“Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini? Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
12 Er da min Kraft som Stenens, er da mit Legeme Kobber?
Je, mimi nina nguvu za jiwe? Je, mwili wangu ni shaba?
13 Ak, for mig er der ingen Hjælp, hver Udvej lukker sig for mig.
Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe, wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
14 Den, der nægter sin Næste Godhed, han bryder med den Almægtiges Frygt.
“Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.
15 Mine Brødre sveg mig som en Bæk, som Strømme, hvis Vand svandt bort,
Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika
16 de, der var grumset af os, og som Sneen gemte sig i,
wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo, ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
17 men som svandt ved Solens Glød, tørredes sporløst ud i Hede;
lakini hukauka majira ya ukame, na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
18 Karavaner bøjer af fra Vejen, drager op i Ørkenen og går til Grunde;
Misafara hugeuka kutoka njia zake; hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
19 Temas Karavaner spejder, Sabas Rejsetog håber på dem,
Misafara ya Tema inatafuta maji, wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri hutazama kwa matarajio.
20 men de beskæmmes i deres Tillid, de kommer derhen og skuffes!
Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini; wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
21 Ja, slige Strømme er I mig nu, Rædselen så I og grebes af Skræk!
Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote; mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
22 Har jeg mon sagt: "Giv mig Gaver, løs mig med eders Velstand,
Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu, au mnilipie fidia kutoka mali zenu,
23 red mig af Fjendens Hånd, køb mig fri fra Voldsmænds Hånd!"
au niokoeni mikononi mwa adui, au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
24 Lær mig, så vil jeg tie, vis mig, hvor jeg har fejlet!
“Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya; nionyesheni nilikokosea.
25 Redelig Tale, se, den gør Indtryk; men eders Revselse, hvad er den værd?
Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli! Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
26 Er det jer Hensigt at revse Ord? Den fortvivledes Ord er dog Mundsvejr!
Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema, na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
27 Selv om en faderløs kasted I Lod og købslog om eders Ven.
Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali.
28 Men vilde I nu dog se på mig! Mon jeg lyver jer op i Ansigtet?
“Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi. Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
29 Vend jer hid, lad der ikke ske Uret, vend jer, thi end har jeg Ret!
Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu; angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.
30 Er der Uret på min Tunge, eller skelner min Gane ej, hvad der er ondt?
Je, pana uovu wowote midomoni mwangu? Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?