< Psalmi 63 >

1 Psalam. Davidov. Dok David bijaše u Judejskoj pustinji. O Bože, ti si Bog moj: gorljivo tebe tražim; tebe žeđa duša moja, tebe želi tijelo moje, kao zemlja suha, žedna, bezvodna.
Mungu, wewe ni Mungu wangu! Ninakutafuta wewe kwa bidii, moyo wangu unakiu yako, mwili wangu unakutamani sana wewe, katika ukame na nchi iliyochoka mahali ambapo hakuna maji.
2 U Svetištu sam tebe motrio gledajuć' ti moć i slavu.
Hivyo nimekutafuta wewe katika watu watakatifu kuona nguvu zako na utukufu wako.
3 Ljubav je tvoja bolja od života, moje će te usne slavit'.
Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakusifu wewe.
4 Tako ću te slavit' za života, u tvoje ću ime ruke dizati.
Hivyo nitakutukuza wewe niwapo hai; kwa jina lako nitainua mikono yangu juu.
5 Duša će mi biti kao sala i mrsa sita, hvalit ću te kliktavim ustima.
Itakuwa kana kwamba nilikula mlo wa mafuta na wenye kunona, kwa midomo ya furaha kinywa changu kitakusifu wewe,
6 Na postelji se tebe spominjem, u bdjenjima noćnim mislim na tebe.
nikufikiripo kitandani mwangu na kukutafakari wewe wakati wa saa za usiku.
7 Ti postade meni pomoć, kličem u sjeni krila tvojih.
Kwa maana umekuwa msaada wangu, na katika uvuli wa mbawa zako ninafurahia.
8 Duša se moja k tebi privija, desnica me tvoja drži.
Ninashikamana nawe; mkono wako wa kuume unanisaidia.
9 Oni što dušu u propast guraju neka siđu u dubinu zemlje,
Lakini wale watafutao kuuharibu uhai wangu wataenda chini kwenye sehemu ya chini kabisa ya nchi;
10 nek' vlasti mača predani budu, nek' postanu plijen šakalima.
watakabidhiwa kwa wale ambao mikono yao hutumia upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
11 A kralj će se radovat' u Bogu, slavit će se tko se kune njime, jer će lašcima biti začepljena usta.
Bali mfalme atashangilia katika Mungu; yeyote anaye apa kupitia yeye atajivunia yeye, lakini vinywa ya wale wasemao uongo watanyamazishwa.

< Psalmi 63 >