< Mudre Izreke 1 >

1 Mudre izreke Salomona, sina Davidova, kralja izraelskog:
Mithali za Sulemani mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli.
2 da se spozna mudrost i pouka, da se shvate razumne riječi;
Mithali hizi zinafundisha hekima na maarifa, kufundisha maneno ya busara,
3 da se primi umna pouka, pravda i pravica i nepristranost;
ili mpate maarifa kwa ajili ya kuishi kwa kutenda wema, haki na adili.
4 da se dade pamet neiskusnima, mladiću znanje i umijeće;
Mithali hizi zinatoa hekima kwa wale ambao hawakufunzwa, na kuwapa vijana maarifa na hadhari.
5 kad mudar čuje, da umnoži znanje, a razuman steče mudrije misli;
Watu wenye busara wasikie na kuongeza elimu yao na watu wenye ufahamu wapate mwongozo,
6 da razumije izreke i prispodobe, riječi mudraca i njihove zagonetke.
kwa kuelewa mithali, misemo, vitendawili na maneno ya wenye busara.
7 Strah je Gospodnji početak spoznaje, ali ludi preziru mudrost i pouku.
Hofu ya Yehova ni chanzo cha maarifa- wapumbavu hudharau hekima na nidhamu.
8 Poslušaj, sine moj, pouku oca svoga i ne odbacuj naputka svoje majke!
Mwanangu, sikia fundisho la baba yako na wala usiziache kanuni za mama yako;
9 Jer će ti biti ljupki vijenac na glavi i ogrlica oko tvoga vrata.
zitakuwa kilemba cha neema katika kichwa chako na jebu zinazoning'inia kwenye shingo yako.
10 Sine moj, ako te grešnici mame, ne pristaj;
Mwanangu wenye dhambi wakikushawishi katika dhambi zao, kataa kuwafuata.
11 ako bi rekli: “Hodi s nama, da vrebamo krv, čekamo u zasjedi nevina ni za što;
Kama watasema, “haya tufuatae, tuvizie ili kufanya mauaji, tujifiche ili tuwashambulie watu wasio na hatia, pasipo sababu.
12 da ih progutamo žive kao carstvo smrti i cijele kao one koji silaze u grob; (Sheol h7585)
Haya tuwameza wakiwa hai, kama kuzimu inavyowachukua wenye afya, na kuwa kama wale waangukao kwenye shimoni. (Sheol h7585)
13 naplijenit ćemo svakojaka blaga, napuniti svoje kuće plijenom;
Tutapata vitu vyote vya thamani; tutazijaza nyumba zetu vile tunavyoiba kwa wengine.
14 bacat ćeš s nama svoj ždrijeb, svi ćemo zajedno imati jednu kesu.”
Weka vitu vyako kwetu; tutakuwa na mfuko moja kwa pamoja.”
15 Sine moj, ne idi s njima na put, makni nogu od njihove staze.
Mwanangu, usitembee katika njia moja pamoja nao; usiruhusu mguu wako kugusa katika mapito yao;
16 Jer na zlo trče svojim nogama i hite prolijevati krv.
miguu ya hukimbilia mabaya na huharakisha kumwaga damu.
17 Jer uzalud je razapinjati mrežu pred očima svima pticama.
Kwa kuwa haina maana kumtegea ndege mtego wakati ndege anaona.
18 A oni vrebaju vlastitu krv, postavljaju zasjedu svojemu životu.
Watu hawa huvizia kujiua wenyewe—wanatega mtego kwa ajili yao wenyewe.
19 Takva je sudba svih lakomih na ružan dobitak: on ih života stane.
Ndivyo zilivyo njia za kila ambaye hupata utajiri kwa udhalimu; mapato ya udhalimu huondoa uhai wa wenye utajiri.
20 Mudrost glasno uzvikuje na ulici, na trgovima diže svoj glas;
Hekima inalia kwa sauti mtaani, inapaza sauti katika viwanja;
21 propovijeda po bučnim uglovima, na otvorenim gradskim vratima govori svoje riječi:
katika mitaa inalia kwa sauti kuu, kwenye maingilio ya milango ya mji inasema “
22 “Dokle ćete, vi glupi, ljubiti glupost i dokle će podsmjevačima biti milo podsmijevanje, i dokle će bezumnici mrziti znanje?
Mpaka lini enyi wajinga mtapenda kuwa wajinga? Mpaka lini enyi wenye dhihaka mtapenda dhihaka, na hadi lini enyi wapumbavu, mtachukia maarifa?
23 Poslušajte moju opomenu! Gle, svoj duh pred vas izlijevam, hoću vas poučiti svojim riječima.
Zingatia karipio langu; nitatoa mawazo yangu kwa ajili yenu; nitawafahamisha maneno yangu.
24 Koliko sam vas zvala, a vi ste odbijali; pružala sam ruku, ali je nitko ne opazi.
Nimeita, nanyi mkakataa kusikiliza; nimeunyosha mkono wangu, wala hakuna aliyezingatia.
25 Nego ste odbacili svaki moj savjet i niste poslušali moje opomene;
Lakini mumedharau mafundisho yangu yote na wala hamkuzingatia maelekezo yangu.
26 zato ću se i ja smijati vašoj propasti, rugat ću se kad vas obuzme tjeskoba:
Nitacheka katika taabu yenu, nitawadhihaki wakati wa kupatwa taabu-
27 kad navali na vas strah kao nevrijeme i zgrabi vas propast kao vihor, kad navali na vas nevolja i muka.
hofu ya kutisha itawapata kama tufani na maafa yatawakumba kama upepo wa kisulisuli, taabu na uchungu vitawapata.
28 Tada će me zvati, ali se ja neću odazvati; tražit će me, ali me neće naći.
Halafu wataniita, nami sitawajibu; wataniita katika hali ya kukata tamaa lakini hawataniona.
29 Jer su mrzili spoznaju i nisu izabrali Gospodnjeg straha
Kwa sababu wamechukia maarifa na hawakuchagua kuwa na hofu ya Yehova,
30 niti su poslušali moj savjet, nego su prezreli svaku moju opomenu.
hawakufuata mafundisho yangu na wakayadharau masahihisho yangu yote.
31 Zato će jesti plod svojeg vladanja i nasititi se vlastitih savjeta.
Watakula matunda ya njia zao, na watashibishwa kwa matunda ya hila zao wenyewe.
32 Jer glupe će ubiti njihovo odbijanje, a nemar će upropastiti bezumne.
kwa maana wajinga hufa wanaporudi nyuma, na kutojali kwa wapumbavu kutawaangamiza.
33 A tko sluša mene, bezbrižan ostaje i spokojno živi bez straha od zla.”
Bali kila anisikilizaye ataishi kwa usalama na atapumzika salama pasipo hofu ya maafa.

< Mudre Izreke 1 >