< Psalmi 107 >

1 Hvalite Jahvu jer je dobar, jer je dovijeka ljubav njegova!
Mshukuruni Yahwe, maana ni mwema, na uaminifu wa agano lake wadumu milele.
2 Tako nek' reknu svi otkupljenici koje Jahve otkupi iz ruke dušmanske
Waseme hivi waliokombolewa na Yahwe, wale aliowaokoa toka mkononi mwa adui.
3 i koje skupi iz svih zemalja, s istoka i sa zapada, sa sjevera i s juga.
Yeye amewakusanya kutoka nchi za kigeni, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
4 Lutahu pustinjom, u samoći pustoj, puta ne nalazeć' do naseljena grada.
Walitanga-tanga janwani katika njia ya nyika hawakuona mji wa kuishi.
5 Gladni su bili, žeđu izmoreni, duša je klonula u njima.
Kwa sababu walikuwa na njaa na kiu, walikata tamaa kutokana na uchovu.
6 Tada zavapiše Jahvi u svojoj tjeskobi, i on ih istrže iz svih nevolja.
Kisha walimuita Yahwe katika shida yao, naye aliwaokoa toka katika dhiki yao.
7 Pravim ih putem pÓovede da stignu ka gradu naseljenu.
Aliwaongoza kupitia njia ya moja kwa moja waweze kwenda mjini kuishi humo.
8 Neka hvale Jahvu za dobrotu njegovu, za čudesa njegova sinovima ljudskim!
Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliowatendea wanadamu!
9 Jer gladnu dušu on nasiti, dušu izgladnjelu on napuni dobrima.
Maana hutosheleza shauku za walio na kiu, na hamu ya wale wenye njaa yeye huwashibisha kwa mambo mema.
10 U mraku sjeđahu i u tmini, sputani bijedom i gvožđima,
Baadhi walikaa katika giza na uvuli wa mauti, walifungwa katika mateso na minyororo.
11 jer su prkosili besjedama Božjim i prezreli naum Svevišnjega.
Hii ni kwa sababu walikuwa wameliasi neno la Mungu na walikataa maelekezo ya Aliye Juu.
12 Srce im stoga skrši patnjama: posrtahu, a ne bješe nikog da im pomogne.
Aliinyenyekesha mioyo yao kupitia magumu; walipata mashaka na hakukuwa na mmoja wa kuwasaidia.
13 Tada zavapiše Jahvi u svojoj tjeskobi i on ih istrže iz svih nevolja.
Kisha wakamwita Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
14 Izvede ih iz tmina i mraka, raskide okove njihove.
Aliwatoa gizani na kwenye uvuli wa mauti na kuvunja vifungo vyao.
15 Neka hvale Jahvu za dobrotu njegovu, za čudesa njegova sinovima ljudskim!
Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
16 Jer razbi vrata mjedena i gvozdene polomi zasune.
Kwa maana amevunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
17 Zbog svojih bezakonja bolovahu oni, ispaštajuć' svoje opačine:
Walikuwa wapumbavu katika njia zao za uasi na kuteswa kwa sababu ya dhambi zao.
18 svako se jelo gadilo duši njihovoj, do vrata smrti oni dođoše.
Walipoteza hamu yao ya kula chakula chochote, na waliyakaribia malango ya kifo.
19 Tada zavapiše Jahvi u svojoj tjeskobi i on ih istrže iz svih nevolja.
Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
20 Riječ svoju posla da ih ozdravi i život im spasi od jame grobne.
Alituma neno lake na likawaponya, na akawaokoa kutoka katika uharibifu wao.
21 Neka hvale Jahvu za dobrotu njegovu, za čudesa njegova sinovima ljudskim!
Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
22 Nek' prinose žrtve zahvalnice i kličući nek' djela njegova kazuju!
Na watoe dhabihu ya shukrani na kutangaza matendo yake kwa kuimba.
23 Oni koji lađama zaploviše morem da po vodama silnim trguju:
Baadhi husafiri baharini katika meli na kufanya biashara juu ya bahari.
24 oni vidješe djela Jahvina, čudesa njegova na pučini.
Hawa huona matendo ya Yahwe na maajabu yake baharini.
25 On reče i olujni se vjetar uzvitla što u visinu diže valove mora.
Kwa maana aliamuru na alivumisha upepo wa dhoruba ambao uliyainua juu mawimbi ya baharini.
26 Do neba se dizahu, u bezdan se spuštahu, u nevolji duša im ginula.
Walipanda juu mawinguni na kushuka vilindini. Nafsi zao ziliyeyuka katika dhiki.
27 Teturahu i posrtahu kao pijani, sva ih je mudrost izdala.
Waliyumba-yumba na kupepesuka kama walevi na hawakujua la kufanya.
28 Tada zavapiše Jahvi u svojoj tjeskobi i on ih istrže iz svih nevolja.
Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
29 Smiri oluju u tih povjetarac, valovi morski umukoše.
Aliituliza dhoruba, na mawimbi yakatulia.
30 Obradovaše se tišini, u željenu luku on ih povede.
Ndipo walifurahia kwa sababu bahari ilikuwa shwali, na aliwaleta kwenye bandari waliyoitamani.
31 Neka hvale Jahvu za dobrotu njegovu, za čudesa njegova sinovima ljudskim!
Oh, ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyowatendea wanadamu!
32 Neka ga uzvisuju u narodnom zboru, neka ga hvale u vijeću staraca!
Wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu na wamsifu yeye katika baraza la viongozi.
33 On pretvori rijeke u pustinju, a izvore vodene u žednu zemlju;
Aligeuza mito ikwa jangwa, chemchem ya maji ikawa nchi kame,
34 plodonosnu zemlju u slanu pustaru zbog zloće žitelja njezinih.
na nchi ya matunda mengi ikawa nchi isiyozaa kwa sababu ya uovu wa watu wake.
35 On obrati pustinju u jezero, a zemlju suhu u vodene izvore
Aligeuza jangwa likawa ziwa la maji na nchi kame ikawa chemchem ya maji.
36 i naseli ondje izgladnjele te podigoše grad gdje će živjeti.
Aliwakalisha huko wenye njaa, nao walijenga mji na kuishi humo.
37 Zasijaše njive, posadiše vinograde što im doniješe obilnu ljetinu.
Walijenga mji ili kupanda mimea shambani, kupanda mizabibu, na kuleta humo mazao tele.
38 I on ih blagoslovi te se namnožiše silno i stada im se ne smanjiše.
Yeye huwabariki wameongezeka sana katika hesabu. Haachi mifugo yao ipungue katika hesabu.
39 Prorijeđeni bjehu i prezreni pod teretom patnja i nevolja.
Kisha wakapungua na kudhilika kwa dhiki na mateso.
40 Onaj što izlijeva prezir na knezove pusti ih da po bespuću pustom lutaju.
Akawamwagia viongozi dharau na akawafanya wazunguke katika jangwa, mahali pasipo na njia.
41 Iz nevolje pÓodiže ubogog i obitelji k'o stada ÓumnožÄi.
Lakini aliwalinda wahitaji dhidi ya mateso na kujali kwa ajili ya familia yake kama kundi la kondoo.
42 Videć' to, čestiti neka se raduju, a zloća neka sebi usta začepi!
Wenye haki wataona hili na kufurahi, na uovu wote utaona na kufunga kinya chake.
43 Tko je mudar nek' o svemu tom razmišlja i nek' uvidi dobrotu Jahvinu!
Yeyote mwenye hekima anapaswa kuyaangalia haya na kutafakari juu ya matendo ya uaminifu wa agano la Yahwe.

< Psalmi 107 >