< 詩篇 114 >

1 當以色列出離埃及時,雅各伯家離開蠻夷時,
Wakati Israeli walipotoka Misri, nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,
2 猶大成了上主的聖所,以色列成了祂的王國;
Yuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu, Israeli akawa milki yake.
3 海洋見了,頓時逃溜,約旦立即回轉倒流。
Bahari ilitazama ikakimbia, Yordani ulirudi nyuma,
4 山嶽跳躍如公羊,丘陵舞蹈似羔羊。
milima ilirukaruka kama kondoo dume, vilima kama wana-kondoo.
5 海洋,什麼使您逃溜。約旦,什麼叫您倒流?
Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia, nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,
6 山嶽,您們為什麼跳躍像公羊?丘陵,您們為什麼舞蹈似羔羊?
enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume, enyi vilima, kama wana-kondoo?
7 大地,您應該在上主的面前,在雅各伯的天主面前搖撼,
Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana, mbele za Mungu wa Yakobo,
8 祂使磐石變為水潭,祂使礁石變成水泉。
aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji, mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.

< 詩篇 114 >