< 箴言 6 >
Mwanangu, kama umekuwa mdhamini wa jirani yako, ikiwa umeshika mikono kwa kuweka ahadi kwa ajili ya mwingine,
2 你如果為你口中說的話所連累,為你口中的言詞所束縛,
kama umetegwa na ulichosema, umenaswa kwa maneno ya kinywa chako,
3 那麼,我兒,你既然已陷在你友人的手中,你就該逃脫,該這樣做:火速前去,央求你的友人,
basi fanya hivi mwanangu, ili ujiweke huru, kwa kuwa umeanguka mikononi mwa jirani yako: Nenda ukajinyenyekeshe kwake; msihi jirani yako!
Usiruhusu usingizi machoni pako, usiruhusu kope zako zisinzie.
5 應急速解救自己,如羚羊掙脫羅網,飛鳥逃脫獵人的圈套。
Jiweke huru, kama swala mkononi mwa mwindaji, kama ndege kutoka kwenye mtego wa mwindaji.
6 懶漢,你去看看螞蟻,觀察牠的作風,便可得些智識:
Ewe mvivu, mwendee mchwa; zitafakari njia zake ukapate hekima!
Kwa maana yeye hana msimamizi, wala mwangalizi, au mtawala,
lakini hujiwekea akiba wakati wa kiangazi na hukusanya chakula chake wakati wa mavuno.
Ewe mvivu, utalala hata lini? Utaamka lini kutoka usingizi wako?
Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
11 這樣貧窮就要如同竊賊,困乏也要如同武士,向你侵襲。
hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.
Mtu mbaya sana na mlaghai, ambaye huzungukazunguka na maneno ya upotovu,
ambaye anakonyeza kwa jicho lake, anayetoa ishara kwa miguu yake na kuashiria kwa vidole vyake,
ambaye hupanga ubaya kwa udanganyifu moyoni mwake: daima huchochea fitina.
15 為此,他的喪亡必突然來臨,霎時間全被毀滅,無法挽救。
Kwa hiyo maafa yatamkumba ghafula; ataangamizwa mara, pasipo msaada.
16 上主憎恨的事,共有六件,連他心裏最厭惡的事,共有七件:
Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana, naam, viko saba vilivyo chukizo kwake:
macho ya kiburi, ulimi udanganyao, mikono imwagayo damu isiyo na hatia,
moyo uwazao mipango miovu, miguu iliyo myepesi kukimbilia uovu,
shahidi wa uongo ambaye humwaga uongo, na mtu ambaye huchochea fitina kati ya ndugu.
20 我兒,應堅守你父親的命令,不要放棄你母親的教訓;
Mwanangu, zishike amri za baba yako, wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
Yafunge katika moyo wako daima, yakaze kuizunguka shingo yako.
22 她們在你行路時引領你,在你躺臥時看護你;在你醒來時與你交談。
Wakati utembeapo, yatakuongoza; wakati ulalapo, yatakulinda; wakati uamkapo, yatazungumza nawe.
23 因為父命是盞燈,母教是光明,嚴格的勸告是生命的道路,
Kwa maana amri hizi ni taa, mafundisho haya ni mwanga na maonyo ya maadili ni njia ya uzima,
yakikulinda na mwanamke aliyepotoka, kutokana na maneno laini ya mwanamke aliyepotoka.
25 不讓你的心貪戀她的美色,不讓她的秋波迷惑你,
Moyo wako usitamani uzuri wake wala macho yake yasikuteke,
26 因為娼妓所求的只是一塊餅,有夫之婦卻獵取寶貴的生命。
kwa maana kahaba atakufanya uwe maskini, hata ukose kipande cha mkate, naye mwanamke mzinzi huwinda maisha yako hasa.
Je, mtu aweza kuchotea moto kwenye paja lake bila nguo zake kuungua?
Je, mtu aweza kutembea juu ya makaa ya moto yanayowaka bila miguu yake kuungua?
29 與他人妻子通姦的人就是這樣:凡接近她的,必難免受罰。
Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa mwanaume mwingine; hakuna yeyote amgusaye huyo mwanamke ambaye hataadhibiwa.
Watu hawamdharau mwizi kama akiiba kukidhi njaa yake wakati ana njaa.
31 但若被擒獲了,他仍須七倍償還,交出家中所有的財物。
Pamoja na hayo, kama akikamatwa, lazima alipe mara saba, ingawa inamgharimu utajiri wote wa nyumba yake.
32 與婦人通姦的人,實屬愚眛,他這樣做,卻是毀滅自己。
Lakini mwanaume aziniye na mwanamke hana akili kabisa; yeyote afanyaye hivyo hujiangamiza mwenyewe.
33 他必遭受可恥的打擊,並且他的恥辱,永不得拭去,
Mapigo na aibu ni fungu lake na aibu yake haitafutika kamwe;
34 因為妒火能激怒男人,使他在報復時,決不留情;
kwa maana wivu huamsha ghadhabu ya mume, naye hataonyesha huruma alipizapo kisasi.
35 任何的賠償,他都不理睬;即便你多送禮品,他也不肯罷休。
Hatakubali fidia yoyote; atakataa malipo, hata yakiwa makubwa kiasi gani.