Preface
Read
+
Publisher
Nainoia, Inc.
PO Box 462, Bellefonte, PA 16823
(814) 470-8028
Nainoia Inc, Publisher
LinkedIn/NAINOIA-INC
Third Party Publisher Resources
Request Custom Formatted Verses
Please contact us below
Submit your proposed corrections
I understand that the Aionian Bible republishes public domain and Creative Commons Bible texts and that volunteers may be needed to present the original text accurately. I also understand that apocryphal text is removed and most variant verse numbering is mapped to the English standard. I have entered my corrections under the verse(s) below. Proposed corrections to the Swahili Contemporary Version, Psalms Chapter 44 https://www.AionianBible.org/Bibles/Swahili---Contemporary/Psalms/44 1) Kwa mwimbishaji. Utenzi wa wana wa Kora. Ee Mungu, tumesikia kwa masikio yetu, baba zetu wametueleza yale uliyotenda katika siku zao, siku za kale. 2) Kwa mkono wako uliwafukuza mataifa na ukawapanda baba zetu, uliangamiza mataifa na kuwastawisha baba zetu. 3) Sio kwa upanga wao waliipata nchi, wala si mkono wao uliwapatia ushindi; ilikuwa ni kitanga cha mkono wako wa kuume, na nuru ya uso wako, kwa kuwa uliwapenda. 4) Wewe ni mfalme wangu na Mungu wangu, unayeamuru ushindi kwa Yakobo. 5) Kwa uwezo wako tunawasukuma nyuma watesi wetu; kwa jina lako tunawakanyaga adui zetu. 6) Siutumaini upinde wangu, upanga wangu hauniletei ushindi; 7) bali wewe unatupa ushindi juu ya adui zetu, unawaaibisha watesi wetu. 8) Katika Mungu wetu tunajivuna mchana kutwa, nasi tutalisifu jina lako milele. 9) Lakini sasa umetukataa na kutudhili, wala huendi tena na jeshi letu. 10) Umetufanya turudi nyuma mbele ya adui, nao watesi wetu wametuteka nyara. 11) Umetuacha tutafunwe kama kondoo na umetutawanya katika mataifa. 12) Umewauza watu wako kwa fedha kidogo, wala hukupata faida yoyote kwa mauzo yao. 13) Umetufanya lawama kwa jirani zetu, dharau na dhihaka kwa wale wanaotuzunguka. 14) Umetufanya kuwa mithali miongoni mwa mataifa, mataifa hutikisa vichwa vyao. 15) Fedheha yangu iko mbele yangu mchana kutwa, na uso wangu umejaa aibu tele, 16) kwa ajili ya dhihaka ya wale wanaonilaumu na kunitukana, kwa sababu ya adui, ambaye anatamani kulipiza kisasi. 17) Hayo yote yametutokea, ingawa tulikuwa hatujakusahau wala hatujaenda kinyume na agano lako. 18) Mioyo yetu ilikuwa haijarudi nyuma; nyayo zetu zilikuwa hazijaiacha njia yako. 19) Lakini ulituponda na kutufanya makao ya mbweha, na ukatufunika kwa giza nene. 20) Kama tungalikuwa tumelisahau jina la Mungu wetu au kunyooshea mikono yetu kwa mungu mgeni, 21) je, Mungu hangaligundua hili, kwa kuwa anazijua siri za moyo? 22) Hata hivyo kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa; tumehesabiwa kama kondoo wa kuchinjwa. 23) Amka, Ee Bwana! Kwa nini unalala? Zinduka! Usitukatae milele. 24) Kwa nini unauficha uso wako na kusahau taabu na mateso yetu? 25) Tumeshushwa hadi mavumbini, miili yetu imegandamana na ardhi. 26) Inuka na utusaidie, utukomboe kwa sababu ya upendo wako usio na mwisho. Additional comments?
Refresh Captcha
The world's first Holy Bible un-translation!