< Ester 1 >

1 Ahashwérosh (Hindistandin Hebeshistan’ghiche bir yüz yigirme yette ölkige hökümranliq qilghan Ahashwérosh)ning texttiki künliride shundaq bir weqe boldi: —
Hili ndilo lililotokea wakati wa utawala wa Mfalme Ahasuero, yule aliyetawala juu ya majimbo mia na ishirini na saba tangu Bara Hindi hadi Kushi.
2 Shu künlerde, u padishah Ahashwérosh Shushan qel’esidiki shahane textide olturghinida,
Wakati huo Mfalme Ahasuero alitawala katika kiti chake cha enzi katika ngome ya mji wa Shushani.
3 u seltenet sürüp üchinchi yili barliq emirliri we beg-hakimlirigha ziyapet berdi; Pars we Médianing qoshuni, shuningdek herqaysi ölkilerning ésilzadiliri we beglirining hemmisi uning huzurigha hazir boldi.
Katika mwaka wa tatu wa utawala wake, alifanya karamu kwa ajili ya wakuu wake wote pamoja na maafisa. Akawaalika viongozi wa jeshi wa Uajemi na Umedi, wana wa wafalme na wakuu wa majimbo.
4 U seltenitining bayliqining shanu-shewkiti we heywitining katta julasini köp künler, yeni bir yüz seksen kün körgezme qildi.
Kwa siku zote 180 mfalme alionyesha utajiri mwingi wa ufalme wake, fahari na utukufu wa enzi yake.
5 Bu künler ötüp ketkendin kéyin padishah yene Shushan qel’esidiki barliq xelqqe chong-kichik démey, ordining charbéghidiki hoylida yette kün ziyapet berdi.
Siku hizo zilipopita, mfalme alifanya karamu kwa muda wa siku saba, katika bustani ya ndani katika jumba la kifalme, kwa ajili ya watu wote kuanzia mdogo hadi mkubwa, waliokuwa katika ngome ya mji wa Shushani.
6 U yer aq we kök kendir yiptin toqulghan perdiler bilen bézelgen bolup, bu perdiler mermer tash tüwrüklerge békitilgen kümüsh halqilargha aq renglik kendir yip we sösün yungluq shoynilar bilen ésilghanidi; aq qashtash we aq mermer tashlar, sedep we qara mermer tashlar yatquzulghan meydan üstige altun-kümüshtin yasalghan diwanlar qoyulghanidi.
Bustani ilikuwa na mapazia ya kitani nyeupe na buluu, yaliyofungiwa kamba za kitani nyeupe na kitambaa cha zambarau, kwenye pete za fedha juu ya nguzo za marmar. Kulikuwepo viti vya dhahabu na vya fedha vilivyokuwa vimewekwa kwenye ile sakafu iliyotengenezwa kwa mawe ya rangi, marmar, lulumizi na mawe mengine ya thamani.
7 Ichimlikler altun jamlarda tutup ichiletti; jamlar bir-birige oxshimaytti; shahane mey-sharablar padishahning seltenitige yarisha mol idi.
Vyombo vya dhahabu vilitumika kwa watu kunywea mvinyo, kila kimoja tofauti na kingine, naye mfalme akatoa mvinyo kwa wingi kwa kadiri ya ukarimu wake.
8 Sharab ichish qaidisi boyiche, zorlashqa ruxset qilinmaytti; chünki padishah ordidiki barliq ghojidarlargha, herkimning ichishi öz xahishi boyiche bolsun, dep békitip bergenidi.
Kwa amri ya mfalme kila mgeni aliruhusiwa kunywa alichotaka, kwa kuwa mfalme alitoa maagizo kwa watumishi wote wa kuhudumu mvinyo kumhudumia kila mtu kwa jinsi alivyotaka.
9 Xanish Washtimu padishah Ahashwéroshning ordisida ayallar üchün ziyapet berdi.
Malkia Vashti pia akawafanyia wanawake karamu katika jumba la kifalme la Mfalme Ahasuero.
10 Yettinchi küni Ahashwérosh padishah sharabtin keypi chagh bolghinida, aldida xizmitide turghan Mehuman, Bizta, Harbona, Bigta, Abagta, Zétar, Karkas dégen yette heremaghisini
Siku ya saba, wakati Mfalme Ahasuero alikuwa amesisimka roho yake kwa mvinyo, aliamuru matowashi saba waliokuwa wakimhudumia, yaani, Mehumani, Biztha, Harbona, Bigtha, Abagtha, Zethari na Karkasi,
11 xanish Washtining puqralar we emirlerning aldida güzellikini körsetsun dep, uni xanishliq tajini kiyip kélishke charqirghili ewetti; chünki u tolimu chirayliq idi.
kumleta Malkia Vashti mbele ya mfalme akiwa amevaa taji lake la kifalme, ili aonyeshe uzuri wake kwa watu na wakuu, kwa kuwa alikuwa ni mzuri wa kupendeza.
12 Lékin heremaghiliri xanish Washtigha padishahning emrini yetküzgende, u kélishni ret qildi; shuning bilen padishah intayin ghezeplinip, uning qehri örlidi.
Lakini wakati watumishi walipotoa amri ya mfalme, Malkia Vashti alikataa kuja. Ndipo mfalme alighadhibika, na hasira yake ikawaka.
13 Shu waqitlarda padishahning ishliri toghruluq qanun-ehkamlarni pishshiq bilgenlerdin meslihet sorash aditi bar idi; shunga padishah weziyetni pishshiq chüshinidighan danishmenlerdin soridi
Kwa kuwa ilikuwa desturi ya mfalme kupata ushauri kwa wataalamu katika mambo ya sheria na haki, alizungumza na watu wenye busara, ambao walijua nyakati,
14 (u chaghda danishmenlerdin uning yénida Karshina, Shétar, Admata, Tarshish, Meres, Marséna, Memukan qatarliq yette Pars bilen Médianing emirliri bar idi; ular daim padishah bilen körüshüp turatti, padishahliqta ular aldinqi qatarda turatti).
nao waliokuwa karibu na mfalme ni Karshena, Shethari, Admatha, Tarshishi, Meresi, Marsena na Memukani, wakuu saba wa Uajemi na Umedi waliokuwa na nafasi ya pekee kwa mfalme nao walikuwa na vyeo vya juu kabisa katika utawala wake.
15 Padishah ulardin: — Xanish Washti menki padishah Ahashwéroshning heremaghilar arqiliq yetküzgen emrim boyiche ish qilmighini üchün uni qanun boyiche qandaq bir terep qilish kérek? — dep soridi.
Mfalme akauliza, “Kulingana na sheria, Malkia Vashti anapaswa kutendewa nini? Malkia hakutii amri ya Mfalme Ahasuero ambayo matowashi walimpelekea.”
16 Memukan padishah we emirlerning aldida jawap bérip: — Xanish Washti aliylirining zitigha tégipla qalmay, belki padishahimiz Ahashwéroshning herqaysi ölkiliridiki barliq emirler we barliq puqralarningmu zitigha tegdi.
Kisha Memukani akajibu mbele ya mfalme na wakuu, “Malkia Vashti si kwamba amemkosea mfalme tu bali pia amewakosea wakuu wote na watu wa himaya yote ya Mfalme Ahasuero.
17 Chünki xanishning shu qilghini barliq ayallarning quliqigha yetse, ular «Padishah Ahashwérosh: «Xanishi Washtini yénimgha élip kélinglar» dep emr qilsa, u kelmeptu!» dep öz erlirini mensitmeydighan qilip qoyidu.
Kwa maana tendo hili la malkia litajulikana kwa wanawake wote, kwa hiyo watawadharau waume zao na kusema, ‘Mfalme Ahasuero aliagiza Malkia Vashti aletwe mbele yake, lakini alikataa.’
18 Pars we Médiadiki melike-xanimlar xanishning bu ishini anglap, bügünla padishahning barliq beg-emirlirige shuninggha oxshash deydighan bolidu, shuning bilen mensitmeslik we xapiliq üzülmeydu.
Leo hii wanawake wa wakuu wa Uajemi na Umedi ambao wamesikia juu ya tabia ya malkia watawatendea wakuu wote wa mfalme vivyo hivyo. Hapatakuwepo na mwisho wa dharau na magomvi.
19 Padishahimgha muwapiq körünse, aliyliridin mundaq bir yarliq chüshürülsun, shuningdek u Parslar we Médialarning menggü özgertilmeydighan qanun-belgilimiliri ichige pütülgeyki, Washti ikkinchi padishah Ahashwéroshning huzurigha kelmigey; uning xanishliq mertiwisi uningdin yaxshi birsige bérilgey.
“Kwa hiyo, kama itampendeza mfalme, atoe amri ya kifalme na iandikwe katika sheria ya Uajemi na Umedi, ambayo haitabadilika, kwamba Vashti kamwe asije tena mbele ya Mfalme Ahasuero. Pia mfalme na atoe hiyo nafasi yake ya umalkia kwa mwanamke mwingine aliye bora kumliko yeye.
20 Aliylirining jakarlighan yarliqi pütün seltenitige yétip anglan’ghan haman (uning seltenitining zémini bipayan bolsimu), ayallarning herbiri öz érige, meyli chong bolsun kichik bolsun ulargha hörmet qilidighan bolidu, — dédi.
Kisha mbiu hii ya mfalme itakapotangazwa katika himaya yake iliyo kubwa sana, wanawake wote watawaheshimu waume zao, kuanzia mdogo hadi mkubwa.”
21 Memukanning bu gépi padishah bilen emirlirini xush qildi; padishah uning gépi boyiche ish kördi.
Mfalme na wakuu wake walipendezwa na shauri hili, hivyo basi mfalme akafanya kama Memukani alivyopendekeza.
22 U padishahning barliq ölkilirige, herbir ölgige öz yéziqi bilen, herqaysi el-milletke öz tili bilen xetlerni ewetip: «Herbir er kishi öz ailisi ichide xojayin bolsun, shundaqla öz ana tili bilen sözlisun» dégen emrni chüshürdi.
Alipeleka barua katika sehemu zote za ufalme wake, kwa kila jimbo kwa maandishi yake mwenyewe na kwa kila watu katika lugha yao wenyewe, akitangaza kwa msemo wa kila watu kwamba inampasa kila mwanaume kuwa mtawala wa nyumba yake mwenyewe.

< Ester 1 >