< Приповісті 17 >

1 Ліпший черствий кусок зо споко́єм, ніж дім, повний у́чти м'ясної зо сваркою.
Afadhali kula ukoko mkavu ukiwa na amani na utulivu kuliko kukaa kwenye nyumba ya karamu kukiwa na magomvi.
2 Раб розумний панує над сином безпутнім, і серед братів він поділить спа́док.
Mtumishi mwenye hekima atatawala juu ya mwana aaibishaye, naye atashirikiana katika urithi kama mmoja wa hao ndugu.
3 Для срі́бла — топи́льна посу́дина, а го́рно — для золота, Господь же серця випробо́вує.
Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu, bali Bwana huujaribu moyo.
4 Лиходій слухається уст безбожних, слухає неправдомо́в язика лиході́йного.
Mtu mwovu husikiliza midomo mibaya; mwongo husikiliza kwa makini ulimi wa madhara.
5 Хто сміється з убогого, той ображає свого Творця, хто радіє з нещастя, — не буде такий без вини.
Yeye anaye mdhihaki maskini huonyesha dharau kwa Muumba wake; yeyote afurahiaye maafa hataepuka kuadhibiwa.
6 Корона для ста́рших — ону́ки, а пишно́та дітей — їхні батьки́.
Wana wa wana ni taji la wazee, nao wazazi ni fahari ya watoto wao.
7 Не присто́йна безумному мова поважна, а тим більше шляхе́тному — мова брехли́ва.
Midomo yenye uwezo wa ushawishi haimfai mpumbavu: je, ni mibaya kiasi gani zaidi midomo ya uongo kwa mtawala!
8 Хабар в о́чах його власника́ — самоцві́т: до всьо́го, до чого пове́рнеться, буде щасти́ти йому́.
Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho; kokote kigeukiapo, hufanikiwa.
9 Хто шукає любови — провину ховає, хто ж про неї повто́рює, розго́нює дру́зів.
Yeye anayesamehe kosa hudumisha upendo, bali yeyote arudiaye jambo hutenganisha marafiki wa karibu.
10 На розумного більше впливає одне остере́ження, як на глупака́ сто ударів.
Karipio humwingia sana mtu mwenye kutambua kuliko mapigo mia kwa mpumbavu.
11 Злий шукає лише неслухня́ности, та вісник жорстокий на нього пошлеться.
Mtu mbaya hupenda kuasi tu; mjumbe asiye na huruma atatumwa dhidi yake.
12 Ліпше спітка́ти обезді́тнену ведмедицю, що кидається на люди́ну, аніж нерозумного в глупо́ті його.
Ni afadhali ukutane na dubu aliyenyangʼanywa watoto wake, kuliko mpumbavu katika upumbavu wake.
13 Хто відплачує злом за добро, — не відступить лихе з його дому.
Ikiwa mtu atalipa baya kwa jema, kamwe ubaya hautaondoka katika nyumba yake.
14 Почин сварки — то про́рив води, тому перед ви́бухом сварки покинь ти її!
Kuanzisha ugomvi ni kama kutoboa bwawa la maji; kwa hiyo acha jambo hilo kabla mabishano hayajaanza.
15 Хто оправдує несправедливого, і хто засуджує праведного, — оби́два вони Господе́ві оги́дні.
Yeye asemaye kuwa asiye na haki ana haki, naye asemaye kuwa mwenye haki hana haki: Bwana huwachukia sana wote wawili.
16 На́що ті гроші в руці нерозумного, щоб мудрість купити, як мо́зку нема?
Fedha ina faida gani mikononi mwa mpumbavu, wakati yeye hana haja ya kupata hekima?
17 Правдивий друг любить за всякого ча́су, в недолі ж він робиться братом.
Rafiki hupenda wakati wote naye ndugu amezaliwa kwa ajili ya wakati wa shida.
18 Люди́на, позба́влена розуму, ру́читься, — пору́ку дає за друга свого.
Mtu mjinga hupana mkono ili kuweka rehani, naye huweka dhamana kwa jirani yake.
19 Хто сварку кохає, той любить гріх; хто ж підвищує уста свої, той шукає нещастя.
Yeye apendaye ugomvi apenda dhambi; naye ainuaye sana lango lake hutafuta uharibifu.
20 Люди́на лукавого серця не зна́йде добра, хто ж лука́вить своїм язико́м, упаде в зло.
Mtu mwenye moyo mpotovu hawezi kufanikiwa; naye ambaye ulimi wake ni mdanganyifu huanguka kwenye taabu.
21 Хто родить безумного, родить на смуток собі, і не поті́шиться батько безглуздого.
Kuwa na mwana mpumbavu huleta huzuni; hakuna furaha kwa baba wa mpumbavu.
22 Серце радісне добре лікує, а пригно́блений дух сушить ко́сті.
Moyo wenye furaha ni dawa nzuri, bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.
23 Безбожний таємно бере хабара́, щоб зігнути путі правосу́ддя.
Mtu mwovu hukubali rushwa kwa siri ili kupotosha njia ya haki.
24 З обличчям розумного — мудрість, а очі глупця́ — аж на кінці землі.
Mtu wa ufahamu huitazama hekima, lakini macho ya mpumbavu huhangaika hadi kwenye miisho ya dunia.
25 Нерозумний син — смуток для батька, для своєї ж родительки — гі́ркість.
Mwana mpumbavu huleta huzuni kwa baba yake na uchungu kwa yeye aliyemzaa.
26 Не добре карати справедливого, бити шляхе́тних за щирість!
Si vizuri kumwadhibu mtu asiye na hatia, au kuwapiga sana maafisa kwa ajili ya uadilifu wao.
27 Хто слова́ свої стримує, той знає пізна́ння, і холоднокро́вний — розумна люди́на.
Mtu mwenye maarifa hutumia maneno kwa kujizuia, naye mtu mwenye ufahamu ana moyo wa utulivu.
28 І глупа́к, як мовчить, уважається мудрим, а як у́ста свої закриває — розумним.
Hata mtu mpumbavu hudhaniwa kuwa na hekima kama akinyamaza, na mwenye ufahamu kama akiuzuia ulimi wake.

< Приповісті 17 >