< Приповісті 10 >
1 Син мудрий — потіха для батька, а син нерозумний — то смуток для неньки його.
Mithali za Sulemani. Mwana mwenye hekima humfurahisha baba yake lakini mwana mpumbavu huleta majonzi kwa mama yake.
2 Не поможуть неправедні скарби, а справедливість від смерти визво́лює.
Hazina zilizolimbikizwa kwa uovu hakosa thamani, bali kwa kutenda haki hujilinda mbali na kifo.
3 Не допустить Господь голодува́ти душу праведного, а набу́ток безбожників згине.
Yehova hawaachi wale watendao haki wapate njaa, bali hamu ya waovu huizuia.
4 Ледача рука до убо́зтва веде, рука ж роботя́ща збагачує.
Mkono mlegevu humfanya mtu awe masikini, bali mkono wa mtu mwenye bidii hupata utajiri.
5 Хто літом збирає — син мудрий, хто ж дрімає в жнива́ — син безпутній.
Mwana mwenye busara hukusanya mazao wakati wa kiangazi, bali ni aibu kwake alalaye wakati wa mavuno.
6 Благослове́нства на голову праведного, а уста безбожним прикриє наси́льство.
Zawadi kutoka kwa Mungu zipo juu ya kichwa cha wale watendao haki; bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
7 Пам'ять про праведного — на благослове́ння, а йме́ння безбожних загине.
Mtu atendaye haki anatufurahisha tunapomkumbuka, bali jina la mwovu litaoza.
8 Заповіді мудросердий приймає, але́ дурногу́бий впаде́.
Wale wenye akili hukubali maagiza, bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataangamia.
9 Хто в невинності ходить, той ходить безпечно, а хто кривить дороги свої, буде ви́явлений.
Yeye anayetembea katika uadilifu hutembea katika usalama, bali yule anayepotosha njia zake, ataonekana.
10 Хто оком моргає, той смуток дає, але дурногу́бий впаде́.
Yeye ambaye hukonyeza kwa jicho lake huleta majonzi, bali mpumbavu mwenye maneno mengi atatupwa chini.
11 Уста праведного — то джерело життя, а уста безбожним прикриє насильство.
Kinywa cha mwenye kutenda haki ni kama chemchemi ya maji ya uzima, bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
12 Нена́висть побуджує сва́рки, а любов покриває всі ви́ни.
Chuki huchochea mafarakano, bali upendo hufunika juu ya makwazo yote.
13 В устах розумного мудрість знахо́диться, а різка — на спину безтя́много.
Hekima inapatikana kwenye kinywa cha mtu mwenye ufahamu, bali fimbo ni kwa ajili ya mgongo wa yule asiye na akili.
14 Прихо́вують мудрі знання́, а уста нерозумного — близькі́ до загибелі.
Watu wenye hekima hutunza maarifa, bali kinywa cha mpumbavu huleta uharibifu karibu.
15 Маєток багатого — місто тверди́нне його, поги́біль убогих — їхні зли́дні.
Mali ya mtu tajiri ni mji wake mwenye ngome; ufukara wa masikini ni uharibifu wao.
16 Дорібок праведного — на життя, прибу́ток безбожного — в гріх.
Mshahara wa watenda haki huelekea kwenye uzima; manufaa ya waovu huelekea dhambini.
17 Хто напу́чування стереже́ — той на сте́жці життя, а хто нехту́є карта́ння, той блу́дить.
Kuna njia kwenda kwenye uzima kwa yule anayefuata maongozo, bali anayekataa maonyo hupotea.
18 Хто нена́висть ховає, в того губи брехли́ві, а хто на́клепи ширить, той дурнове́рхий.
Yeye afichaye chuki anamidomo ya uongo, na yeye anayesambaza kashfa ni mpumbavu.
19 Не бракує гріха в многомо́вності, а хто стримує губи свої, той розумний.
Katika maneno mengi, hapakosi uhalifu, bali aliyemwangalifu katika usemi wake ni mwenye busara.
20 Язик праведного — то добі́рне срібло́, а розум безбожних — мізе́рний.
Ulimi wa yule atendaye haki ni fedha safi; kuna thamani ndogo katika moyo wa mbaya.
21 Пасу́ть багатьох губи праведного, безглузді ж умирають з неро́зуму.
Midomo ya yule atendaye haki huwastawisha wengi, bali wapumbavu hufa kwa sababu ya kukosa akili.
22 Благослове́ння Господнє — воно збагачає, і сму́тку воно не прино́сить з собою.
Zawadi njema za Yehova huleta utajiri na haweki maumivu ndani yake.
23 Нешляхе́тне робити — заба́ва неві́гласа, а мудрість — люди́ні розумній.
Uovu ni mchezo achezao mpumbavu, bali hekima ni furaha kwa mtu mwenye ufahamu.
24 Чого нечести́вий боїться, те при́йде на нього, а пра́гнення праведних спо́вняться.
Hofu ya mwenye uovu humkumba ghafla, bali shauku ya mwenye haki itatimizwa.
25 Як буря, яка пронесе́ться, то й гине безбожний, а праведний має дові́чну осно́ву.
Waovu ni kama dhoruba inayopita, na hawapo tena, bali mwenye haki ni msingi unaodumu milele.
26 Як о́цет зубам, і як дим для оче́й, так лінивий для тих, хто його посилає.
Kama siki kwenye meno na moshi kwenye macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
27 Страх Господній примножує днів, а ро́ки безбожних вкоро́тяться.
Hofu ya Yehova huongeza maisha, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
28 Сподіва́ння для праведних — радість, а наді́я безбожних загине.
Matumaini ya wale watendao haki ndiyo furaha yao, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
29 Дорога Господня — тверди́ня неви́нним, а заги́біль — злочинцям.
Njia ya Yehova huwalinda wale wenye uadilifu, bali kwa waovu ni uhalibifu.
30 Повік праведний не захита́ється, а безбожники не поживуть на землі.
Wale watendao haki hawataondolewa, bali waovu hawatabaki katika nchi.
31 Уста праведного дають мудрість, а лукавий язик буде втятий.
Katika kinywa cha wale watendao haki hutoka tunda la hekima, bali ulimi wa kupotosha utakatwa.
32 Уста праведного уподо́бання знають, а уста безбожних — лука́вство.
Midomo ya wale watendao mema huyajua yanayokubalika, bali kinywa cha waovu, huyajua yanayopotosha.